News/Stories

OFISA MAENDELEO RUANGWA AKEMEA NDOA ZA UTOTONI

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
 

Ofisa Maendeleo Wilaya ya Ruangwa, Rashid Namkulala amekemea vikali Mila na desturi zinazochochea ukatili wa wanawake na watoto wilayani humo. Ameyasema hayo juzi wakati wa mdahalo kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Nambilanje na ya Msingi Nambilanje. Chama Cha Wanahabari Wanawake (TAMWA) kimesimamia mafunzo kwa kamati ya ulinzi na usalama ya Kijiji cha Nambilanje na midahalo na majadiliano kwa shule za Msingi na Sekondari kuhusu Mila na desturi zinazochochea mimba za utotoni wilayani humo.

Latest News and Stories

Search