News/Stories

TGNP YAMTUNUKIA EDDA SANGA TUZO YA HESHIMA

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
 

Mkurugenzi wa Chama Cha Wanahabari Wanawake (TAMWA) aliyemaliza muda wake, Edda Sanga, amepewa tuzo ya heshima ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake katika Asasi za kiraia. Tuzo hiyo imetolewa leo na Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP), wakati wa tamasha la 14 la Jinsia. 

“Nimefurahi kupokea tuzo hiyo nawashukuru sana na kuwapongeza pia wale ambao wameona nimestahili kupokea tuzo hiyo,” Amesema Edda Sanga. Pia amewataka wengine waliopata tuzo hiyo kuendeleza mapambano ya kumkomboa mtoto wa kike, kumlinda na kumpa haki yake.

TAMWA tunampongeza Edda Sanga kwa kutwaa tuzo hii adhimu na pia tunawapongeza TGNP Mtandao kwa kuona umuhimu wa kuandaa tuzo hizi.

Latest News and Stories

Search