News/Stories

‘FAKE’

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
 

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinapenda kukanusha taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zikionyesha kuwa tumelishukuru Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uamuzi wa kumchukulia hatua Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima.

Pia taarifa hizo zimekwenda mbali zaidi zikionyesha TAMWA imemtaka Askofu Gwajima kumuomba radhi Rais Samia  Suluhu na Waziri wa Afya, Doroth Gwajima kwa niaba ya wanawake wote nchini.

Tunapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa taarifa hizo ambazo zimewekwa katika nembo za vyombo vya habari kama ITV, AYO TV na katika tamko linaloonyesha kusainiwa na Mkurugenzi wa TAMWA Dkt. Rose Reuben, si za kweli. 

TAMWA haijafanya mkutano wa kihabari, haijatoa tamko wala kuzungumza na chombo chochote cha habari kuhusu sakata la Askofu Gwajima na Bunge. 

TAMWA inafanya kazi kwa kufuata maadili na taratibu za kiuandishi  na ina taratibu  zake pindi inapotakiwa kuzungumzia masuala ya jinsia, habari na afya.

Latest News and Stories

Search