News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Call For the Consultancy Services to Conduct Survey on Current Prevalence and Mechanisms to Prevent or Deal with Sexual Harassment, Sexual Corruption and Efforts of Gender Mainstreaming in the Media of Tanzania

 

1.0 BRIEF DESCRIPTION OF TAMWA

Tanzania Media Women’s association (TAMWA) is a non-partisan, non-profit sharing professional media membership association registered in 1987 under the society’s ordinance cap 337 of 1954 with registration number so 6763. The association also in 2004 complied with the new non-governmental organizations’ (NGO) law of 2002 with 0NGO1886 registration number. Our mission is to advocate for women and children’s rights by conducting awareness raising activities for cultural, policy and legal transformations in the society through the use of media. We envision having peaceful Tanzania environment which respects human rights from a gender perspective.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
1.0. Brief Description of TAMWA

TAMWA is a non-partisan, non-profit sharing professional media membership association registered in 1987 under the society’s ordinance cap 337 of 1954 with registration number so 6763. The association also in 2004 complied with the new non-governmental organizations’ (NGO) law of 2002 with 0NGO1886 registration number. For operational purposes, TAMWA is also registered in Zanzibar under society act no 6 of 1995 with registration number 493. TAMWA has offices in Zanzibar and Dar es Salaam. TAMWA started with 12 media women, but the membership has grown to   more than 160 women journalists. TAMWA has 34 years’ experience in partnership with other organizations, advocating for women and children’s rights through the use of media. TAMWA’S mission - to advocate for women and children’s rights by conducting awareness raising activities for cultural, policy and legal transformations in the society through the use of media. TAMWA visions, to havea peaceful Tanzania environment which respects human rights from a gender perspective.

2.0. Purpose and Objective of the Assignment

The baseline survey Advancing Media advocacy to Rural and Urban Women and Girls’ SRHR in Tanzania aim at enhancing the project towards enriching media practitioners’ skills in promoting sexual and reproductive health rights outcomes in Tanzania. The project focuses on the increasing competencies of media practitioners on reporting SRHR OUTCOMES, targeting the Mainstream Media (TV, Newspapers and Radio) Community radio Online Media in order to increase the proportion of media sensitization on SRHR contents. 

3.0. Strategies to achieve the purpose and the objective of the projects

To come up with scientific ground of the project goals, ensure effectiveness and efficiencies of the project, TAMWA is conducting a baseline survey to inform the current SRHR media contents and the media practitioners understanding of the SRHR but also understanding best media channels for SRHR issues.  The findings will enable the project team to come up with the relevant training manual or tool that will help TAMWA to build capacity, support and motivate media practitioners to cover SRHR issues including training. 

4.0. Terms of Reference 
4.1. Familiarize with the proposal to understanding the goals of the project 
4.2. Develop data collection questionnaires
4.3. Lead in the implementation of high-quality data collection with adequate field testing and supervision of all data collection and data entry, including ensuring consent from all participants.
4.4. Analyze the qualitative data collected, including content/thematic analys
4.5. Facilitate a survey validation meeting with TAMWA staff as well as other identified stakeholders
4.6. Writing draft and final reports as well as incorporating feedback
4.7. Proposing the SRHR training tool for the media practitioners in accordance to the survey results and needs assessments.
 
Mode of application: Send your cv to This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. before Thurthday March 09, 2023.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Na Edina Salila
Rushwa ya ngono ni tatizo linalowatesa watu wengi hasa wanawake na wasichana kazini na katika taasisi za elimu yaani vyuo na vyuo vikuu.
Chanzo kikuu cha rushwa hiyo kinatajwa kuwa ni mmomonyoko wa maadili na matumizi mabaya ya madaraka kwa baadhi ya wahadhiri na viongozi na watumishi katika maeneo ya kazi.
Ingawa rushwa hii huwaathiri zaidi wanawake, kumekuwapo madai kutoka kwa watu na vyanzo mbalimbali kuwa, baadhi ya wasichana wamekuwa kichocheo na ushawishi kwa wahusika ili wapate upendeleo kwa malipo ya ngono.
Katika moja ya semina za hivi karibuni zilizoandaliwa na Tamwa kwa wahariri na wandishi wa habari Dar es Salaam, washiriki walisema kutokana na uwezo mdogo kimasomo, baadhi ya wanafunzi wa kike wanajenga mazoea ‘yanayovuka mipaka’ kwa wakufunzi na wahadhiri wa kiume ili wapewe upendeleo wa alama za juu katika mitihani.
Utafiti uliofanywa na Mfuko wa Udhamini wa Wanawake Tanzania (WFT- T) kwa kushirikiana na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) mwaka 2020 katika baadhi ya vyuo vikuu nchini, ulibaini kuwa, zaidi ya asilimia 50 ya waliohojiwa walieleza kuwepo kwa rushwa ya ngono vyuoni.
Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma wa TAKUKURU, Joseph Mwaiselo, anasema kutokana na kuwapo rushwa ya ngono, mwaka 2007 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilitunga Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na katika sheria hiyo, kiliwekwa Kifungu cha 25 ili kuharamisha rushwa ya ngono.
Kwa mujibu wa sheria hiyo, ni kosa kwa mtu mwenye mamlaka kutoa sharti lolote la kutaka rushwa ya ngono katika ili kutoa huduma husika.
“Tuligundua kuna rushwa ya ngono katika vyuo vikuu na kwamba, wapo wanaotumia mamlaka yao vibaya kwa kudai rushwa ya ngono, lakini pia wapo wanafunzi wanaowashawishi wahadhiri ili wapewe alama za kuwafanya wafaulu mitihani,” alisema.
Kwa mujibu wa utafiti huo, mifumo dhaifu na isiyo rafiki kwa waathirika kutoa taarifa na kushughulikia tatizo hilo, ni miongoni mwa mambo yanayokwamisha mafanikio katika vita dhidi ya rushwa ya ngono.
Mkaguzi wa Polisi kutoka Dawati la Jinsia Wilaya ya Ubungo, Evetha John, anasema: “Tumeshapokea kesi za wanafunzi wa vyuo wakilalamikia rushwa ya ngono, lakini kwa sababu tunashirikiana na taasisi nyingine husika ikiwemo Takukuru; waathirika tunawaunganisha na maofisa wa Takukuru ili kupata usaidizi zaidi wa kisheria.”
Mkufunzi wa Masuala ya Mawasiliano ya Jamii, Mary Kafyome, anasema kikwazo kingine katika mafanikio dhidi ya tatizo hilo, ni taasisi nyingine zikiwamo za elimu ya juu kutokuwa na sera zilizo wazi kuhusu masuala ya usawa wa kijinsia.
“Baadhi ya vyuo vikuu havina sera za kuzuia ukatili wa kingono na usawa wa kijinsia, hivyo ni ngumu kuzuia vitendo hivyo vyuoni, lakini pia vyuo vingine tumeona sera wanazo lakini hazijulikani kwa wafanyakazi na wanafunzi, hii huchangia kushamiri kwa vitendo hivyo,'' anasema Kafyome.
Kwa mujibu wa uchunguzi, ukimya wa wanawake wengi katika jambo hili hufanya lisisikike huku waathirika wengine wakiamini kuwa, wakifichua uovu huo, jamii itawanyanyapaa.
“Waathirika wengi wanahofia kusema kwa sababu hawana uhakika wa kupata haki yao na kuhofia mtuhumiwa kusikilizwa zaidi kuliko wao,” anasema Kafyome.
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) aliyeomba jina lake lisitajwe anasema: “Wasichana tunateseka sana na hili tatizo maana sasa kiwango cha juu cha alama ndio dili na si elimu yenyewe… Ndio maana wengine hutumbukia katika huo mtego kwani hata wahadhiri wenyewe wanajali maksi na si elimu hali inayosababisha rushwa hii kuonekana jambo la kawaida vyuoni.”
Anaongeza: “Nashauri tupewe mbinu za kuripoti matukio haya."
Naye Anna Hangwa, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini (TUDARCo) kilichopo Dar es Salaam, anasema: “Tunatakiwa kujithamini, kuwajibika… Mwalimu akitaka kukurudisha nyuma kimasomo, kama umewajibika na kusoma ipasavyo utakuwa na uhakika wa ufaulu wako."
Wadau mbalimbali wa usawa wa kijinsia wanashauri kuwapo madawati ya kjinsia yaliyo rafiki zaidi kwa wanafunzi kuripoti matukio ya unyanyasaji yanayofanyika vyuoni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tamwa, Dk Rose Reuben, anasema: “Ni wakati sasa wa madawati ya kijinsia kuwa hai katika kila upande.”

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active
Na Edina Salila
 
“Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikifanya kazi katika mazingira magumu sana huku nikikumbana na majaribu na matokeo yake, nimekuwa mtu wa bosi wangu kukejeli na kukashfu ili nionekane sijui kutafuta wala kuandika stori (habari) kisa, eti nimemkatalia bosi wangu kimapenzi…”
 
“Kinachoniumiza zaidi ni kuwa, licha ya kuwashirikisha wenzangu, nimeushirikisha uongozi ili kukomesha hali hii ambayo ni tatizo kubwa kwangu, lakini sijashirikishwa wala kuona mabadiliko au hatua zozote zikichukuliwa.”
 
Ndivyo anavyosema Kemmy Mang’ombe (si jina halisi), mmoja wa wandishi wa habari wanawake katika gazeti moja la kibinafsi litolewalo kwa Kiswahili kila siku nchini.
 
Kemmy ambaye ni kiwakilisha cha wandishi wa habari wengi wa kike waliopitia madhira hayo anasema, baada ya kuzidiwa na adha huku akisaka ufumbuzi kwa wandishi wenzake wa kike, alibaini kuwa, wengi walikuwa wakimshangaa kwa kuwa nao, wamekumbwa na madhira hayo; wakalegea na kutumbukia kwenye janga la rushwa ya ngono na wakubwa wao wa kazi.
 
Kwa mujibu wa uchunguzi, miongoni mwa hoja zinazotumiwa na watu wanaodai rushwa hii ambayo kwa kiasi kikubwa huwaathiri vibaya wandishi wa habari wa kike, ni ahadi za kuajiriwa hasa kwa wandishi wa kike ambao hawajaajiriwa, ahadi za kuongezwa vyeo na mshahara (kwa waajiriwa), upendeleo wa kupewa safari na kazi kubwa na msaada wa ziada kuhakikisha kazi (stori) za mlengwa zinatoka.
 
Kwa mujibu wa Kemmy, baada ya kumkatalia mhariri wake, mara kadhaa anapowasilisha habari zake kwa mhariri hasa kubwa, huambulia kejeli kuwa hajui kuandika na kutakiwa kutafuta nyingine.
 
“Cha ajabu, kwa kuwa mimi ni correspondent, ninalipwa kadiri ya kazi zangu zinazotoka, anapozikataa nikaamua kupeleka magazeti mengine, zinatoka na mara tatu zimetoka ukurasa wa mbele na nyingine mbili zikawa ‘lead’ (habari kuu katika gazeti).”
 
“Sasa ndipo ujiulize, huku wanasema sijui kuandika, magazeti mengine, habari hiyohiyo inakuwa kuu; tena magazeti yenye heshima maana stori zinajitosheleza,” anasema.
 
Anaongeza: “Kinachosikitisha, huko kwingine baada ya kuona stori zinatoka nikataka kuhamia huko, nikakumbana na yale yale; nikaangukia kwa bosi mmoja anayesisitiza kutaka nihusiane naye kingono eti stori zangu zitakuwa zinatoka kila siku… Kwa kweli, nikaona kama mambo ni haya, uandishi umenishinda; ngoja nikauze maandazi…”
 
Mwaka 2021, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kwa kushirikiana na Mfuko wa Udhamini wa Wanawake Tanzania, (WFT-T) kupitia mradi wa kuangazia rushwa ya ngono kwa wanahabari, walifanya utafiti uliothibitisha kuwapo vitendo vya rushwa ya ngono na udhalilishaji mwingine wa kijinsia katika vyombo vya habari ukiwamo wa kimwili na maneno. 
 
Kwa mujibu wa Ripoti ya Haki za Binadamu na Biashara ya Mwaka 2021/2022 iliyozinduliwa Septemba 30, 2022 na Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC), rushwa ya ngono dhidi ya waandishi wa habari wanawake ni janga kubwa linalokwamisha tasnia.
 
Ripoti inasema wanaotuhumiwa zaidi katika rushwa hiyo ni wahariri na maofisa rasilimaliwatu wakifuatiwa na meneja, wakurugenzi, wamiliki pamoja na vyanzo vya habari. 
 
UKIMYA KIKWAZO KIKUBWA
 
Kwa mujibu wa utafiti huu uliofanywa mkoani Dar es Salaam, asilimia 52 ya wanawake hawapo tayari kuweka wazi adha ya rushwa ya ngono wanayoyapata kazini.
 
Wadau wengi wanasema. licha ya kuwepo sera na miongozo ya kijinsia kwa baadhi ya vyombo vya habari, hakuna uzingatiwaji wala utekelezwaji sera hizo.
 
 
Utafiti uliofanywa na Asasi ya Wanawake katika Habari Afrika (WAN-IFRA) mwaka 2020/21 nao ulibaini kuwa, asilimia 41 ya wanawake wanahabari waliwahi kufanyiwa unyanyasaji wa kingono wakiwa kwenye maeneo ya kazi.
 
Kwamba, asilimia 74.5 ya wanahabari wanawake hawakuweka wazi kuhusu manyanyaso au kero ya rushwa ya ngono wanayokumbana nayo.
 
Mhariri Mkuu wa Vipindi,  Afya radio Ester Baraka anasema: 
“Wanawake tumeumbiwa weledi mkubwa katika kazi, tumeumbiwa kujituma na kufanya kazi kwa mapenzi yote sasa inapokuja madhila hayo ni wepesi sana kukumbwa na mawazo na kuathirika kisaikolojia kwani hujikuta tukitafakari sana namna ya kulikwepa suala hilo.” 
 
 
Naye Mratibu wa Gazeti la HabariLEO Afrika Mashariki, Joseph Sabinus anasema: “Rushwa ya ngono ipo kwa kuwa kwa wanaume wengi katika vyombo vya uamuzi kuliko wanawake na si wahariri pekee, ingawa si wanaune wote wenye kasumba hiyo....”
 
Anasema: “Waathirka wengi wa rushwa ya ngono wanahofia kutoa taarifa kwa kuhisi kwamba mhusika akichukuliwa hatua za haki kali, umma utamgeukia na kumsuta kuwa anafukuzisha watu kazi, hivyo atajidhalilisha na watu watamchukia.”
 
Meneja wa kituo cha redio cha Safari FM, Ashraf Mohamed, anasema tatizo la rushwa ya ngono halikomi kwa kuwa wapo baadhi ya wanahabari wanawake wanaojirahisisha na kutaka kufanya chochote ili wapate kazi.
 
Anasema kutokukoma kwa tatizo hili kunachochewa pia utandawazi unaofanya baadhi ya watu kudhani kuwa, rushwa ya ngono ni kitu cha kawaida kwa kuwa hufanyika kwa siri na kumfanya hata mtu asiye na sifa kupata kazi kirahisi.
 
MATOKEO
Katika utafiti wa TAMWA, Dk Rose anasema: “Tuligundua tatizo hilo lipo na limesababisha baadhi ya wanahabari kufukuzwa kazi, kuacha kazi na wengine wameweza kupingana na kuhimili japokuwa hawana furaha katika kazi hiyo na wengne hawakusema.”
 
Anasema kati ya asilimia 65-84 ya waandishi wa habari walisema tatizo lipo huku watuhumiwa wengi wakiwa ni wahariri wa habari ambao wana mamlaka ya kuamua habari ipi na ya nani itangazwe au ipi ichapishwe.
 
Rose anabainisha makundi yanayoathirika zaidi na rushwa ya ngono kuwa ni wanafunzi walio katika mafunzo kwa vitendo, wandishi wa mikoani na wale wanaotuma habari zao wakiwa hawajaajiriwa maarufu ‘correspondents’.
 
Utafiti uliofanywa na WFT-T kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mwaka 2020 ulibaini kuwa, udhaifu upo katika mfumo wa udhibiti wa rushwa ya ngono kazini huku asilimia 10.7 hadi 38.2 ya watu waliohojiwa wakikubali kuwepo kwa sera, miongozo na taratibu za udhibiti wa rushwa ya ngono. Zaidi ya asilimia 60 hawakufahamu kuwapo kwa mambo hayo.
 
MADHARA YA RUSHWA YA NGONO
 
“Hii ndio sababu wanafunzi wengi wanasoma uandishi wa habari, lakini ni wachache sana wanaoonekana katika vyombo vya habari na upande wa wandishi wa kujitegemea, tukagundua taarifa zao nyingi hazitumiki kwa sababu ya rushwa hiyo,” alisema Dk Rose. 
 
Kwa mujibu wa WAN-IFRA, udhalilishaji wa kingono kwa wanahabari wanawake umewafanya wengi wasioweza kupambana kuamua kuikimbia tasnia ya habari na kupoteza vipaji lukuki.
 
Ripoti inasema: “Ni asilimia 21 tu ya wanahabari wanawake wanaopaza sauti zao pindi wanapofanyiwa ukatili huu.”
 
Naye mkongwe katika tasnia ya habari, Rose Haji anasema: “Kama msichana atakuwa mwoga na asijue kujilinda, ‘atachezewa’ na ofisi nzima na hata kama ana uwezo mkubwa, watamuona si kitu jambo ambalo ni hatari.”
 
“Ukimkubali mwanaume tabu, ukimkataa ndio mara mbili, unapomkataa hasa kiongozi hapo ndipo anakuwekea chuki na kukusingizia mambo mengi, mara hujui kutafuta habari, mvivu hujui kuandika, na visingizo vingi ambavyo vitashusha hadhi yako ya utendaji kazi,” anasema Rose. 
 
Katika mkutano ulioandaliwa na TAMWA jijini Arusha, mei 5, 2022 Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alinukuliwa akisema: “Wanahabari wanawake wanapungua katika tasnia ya habari nchini kutokana na changamoto mbalimbali ikiwamo mazingira yasiyo rafiki, ni wakati sasa wa kuwatia moyo wachache waliopo na kuwapongeza ili wasiondoke katika tasnia." 
 
Mkurugenzi wa Programu katika Shirika la Utu wa Mtu Tanzania ambaye pia ni mwanasaikolojia, Harrieth Baagae, anasema: “Rushwa ya ngono husababisha msongo wa mawazo na mwanamke kuchukia wanaume na kuweka kisasi kutokana na hasira ya umda mrefu.”
Anasema hii ni kwa kuwa mwathirika huendelea kufanya kazi na kukutana na aliyemfanyia kitendo na anapokumbuka, hasira na maumivu ya kiakili humrudia japo hasemi na hali hiyo, hushusha ufanisi katika kazi. 
 
Kwa mujibu wa Harrieth, mwathirika wa rushwa ya ngono hutibika kwa ushauri wa kisaikolojia wa muda mrefu ili kujengeka kiimani na kujikubali kuwa alikoseakukubali kutoa rushwa hiyo.
KANUNI ZA KIMAADILI
Miongoni mwa kanuni za kimaadili zilizotolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwa waandishi wa habari ni pamoja na kuheshimu utu na hadhi ya mtu kwa kulinda mambo yote yanayohusu hadhi ya mtu, kuzuia rushwa ya ngono, unyanyasaji, udhalilishaji wa kijinsia, kiumri na udhaifu wa changamoto ya maumbile ukiwemo ulemavu. 
SHERIA DHIDI YA RUSHWA YA NGONO
Kwa mujibu wa Kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na.11 ya Mwaka 2007, rushwa ya ngono ni kitendo anachofanya mtu mwenye mamlaka, katika kutekeleza matakwa yake ya kudai ngono kwa mtu kama kishawishi cha kumpatia huyo mtu ajira, cheo, haki, fursa au upendeleo mwingine. 
 
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma wa TAKUKURU, Joseph Kasongo hiyo inatoa ulinzi kwa mtoa taarifa na mtu yeyote anayebainika kutenda kosa hilo, anaweza kupata ya adhabu ya faini ya Sh5 milioni au kifungo cha miaka mitatu.
Kasongo anasema: “Kutokana na utafiti tulioufanya na WFT mwaka 2020, vyuo vikuu vimeanzisha madawati ya kijinsia, kamati za kinidhamu na maadili, na  TAKUKURU tuimeimarisha klabu za wapinga rushwa katika vyuo ili wawe na mamlaka ya kuhoji vitendo hivyo vinapotokea…”
 
SULUHISHO DHIDI YA JANGA
 
Vyanzo mbalimbali vinasisitiza wandishi wa habari wajengewe uwezo kufichua uhalifu huo na wahusika wachukuliwe hatua kali za kimaadili na kisheria.
Sabinus anasema: “Vyombo vya habari na taasisi ziwe na sera zinazofahamika na zilizo wazi kuhusu masuala ya usawa wa kijinsia na hususan zikitaja nini kinapaswa kufanyika, nini hatua zinapaswa kuchukuliwa dhidi ya anayeoomba au kudai na pia, kuwepo mazingira salama kwa waathirka wanaotoa taarifa kuhusu matukio hayo….” 
 
Anaongeza: “Kuwe na uwiano wa wanawake na wanaume wanaotoa uamuzi katika vyombo vya habari na pia, kuwe na madawati ya jinsia yenye weledi ili iwe rahisi kwa mtu kuelezea tatizo lake ili pia lishughulikiwe kwa siri.”
 
Dk Rose yeye anasema: “TAMWA tunaamini ni wakati sasa wa kuanzisha kamati ama kitengo maalumu kushughulikia masuala ya rushwa ya ngono katika vyombo vya habari ili kuwashauri wanahabari wanawake waliokumbwa na majanga haya pamoja na kufundishwa mbinu mbalimbali za kukabili tatizo hili.”

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) leo Agosti 27, kimefanya uchaguzi wake Mkuu wa mwaka na kumchagua Joyce Shebe kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.
 
Shebe ambaye ni Mhariri Mkuu wa Clouds Media Group, ataongoza kwa miaka mitatu. Huu ni muhula wa pili kwa Shebe baada ya kuongoza miaka mitatu ya mwanzo kuanzia 2019. Katika uchaguzi huo, Shebe alikuwa akichuana na Mwasisi wa TAMWA, Lyela Sheikh.
 
Nafasi nyingine katika uchaguzi huo ni wajumbe wa bodi, ambapo Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Tumaini, Mary Kafyome, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha St Augustine, Dk Kaanaeli Kaale nao walichaguliwa kuwa wajumbe wa bodi ya Tamwa.

Page 1 of 19

Latest News and Stories

Search