News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Wakati dunia ikisherehekea Siku ya Wanawake Duniani, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA)kinakuletea wanahabari wakongwe waanzilishi wa TAMWA. Hiki ndicho wanachokisema katika maadhimisho haya ya Siku ya Wanawake Duniani.

Halima Shariff, yeye ni mtafiti, kiongozi na mwalimu . Ni miongoni mwa waasisi wa TAMWA aliyezaliwa kutoka katika familia ya kawaida kabisa, mkoani Tanga.
 
Akiwa ni mtaalamu na nguli wa habari nchini, Halima amewahi kuandika katika gazeti la Daily News miaka ya 80 na mtangazaji wa  Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani(Deustche Welle).
 
Pamoja na fani ya habari, Halima amewahi  kushika nafasi kubwa katika taasisi za kimataifa  na kwa sasa ni Mkurugenzi wa Mradi wa Uzazi wa Mpango wa Advanced Family Planning Project(AFP).
 
Ni miongoni mwa wanawake waliosimamia kidete maendeleo ya wanawake na watoto katika masuala ya elimu, afya ya uzazi na Virusi vya Ukimwi. 
 
Amewahi kuongoza miradi mikubwa ya afya  ikiwamo ya Shirika la Misaada la watu wa Marekani USAID. Ameshiriki katika kutetea hadi  kufanikisha kupitishwa kwa muswada wa  masuala ya Ukimwi, kuanzishwa kwa sera ya HIV/AIDS katika maeneo ya kazi. Amewahi pia kuwa Kamishna wa Tume ya Ukimwi Tanzania (TACAIDS). 
 
Anachokisema katika kuadhimisha Sharif katika kuadhimisha Siku ya Wanawake duniani: 
 
“Kuimarisha nafasi ya mwanamke katika nyanja zote katika jamii ni harakati endelevu zinazohitaji jitihada za pamoja zenye kasi inayoongezeka kizazi hadi kizazi. Kwa mantiki hiyo Tanzania tumefanikiwa kujenga uelewe wa jamii kuhusu nafasi muhimu ya mwanamke katika kujenga familia na katika maendeleo kwa ujumla” 
 
“Lakini bado hatujawekeza vya kutosha katika kuhakikisha afya ya mwanamke inapewa kipaumbele ukizingatia kwamba bado wastani wa kuzaa wa taifa ni watoto sita kwa mwanamke wa rika la uzazi (15-49). 
 
“Inatia moyo kwamba serikali imekuwa ikielekeza nguvu huko lakini ni eneo linalohitaji kutazamwa zaidi kwani mara nyingi wanawake hukosa fursa za kujiendeleza kutokana na changamoto za uzazi,”

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Wakati dunia ikisherehekea Siku ya Wanawake Duniani, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA) kinakuletea wanahabari wakongwe waanzilishi wa TAMWA. Hiki ndicho wanachokisema katika maadhimisho haya ya Siku ya Wanawake Duniani.

Ummy Mahfoudh.  Ni mwanahabari mkongwe, Mwanachama wa Chama cha Wanahabari  Wanawake tangu 1988. Amewahi kufanya kazi katika taasisi zisizo za kiserikali za kitaifa na kimataifa katika nchi za Uingereza, Denmark, Tunisia na Afrika Kusini.
Ni miongoni mwa walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika mkutano wa kidunia wa haki za mwanamke, maarufu mkutano wa Beijing mwaka 1995. Amewahi kushiriki utafiti wa chanzo cha mauaji ya wanawake wazee kutokana na imani za kishirikina na mauaji ya albino Tanzania. 
 Kwa sasa ni mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya magazeti Zanzibar
Ni mshairi, ana mume na watoto wanne. 
Anachokisema katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Tanzania;
“Katika kuadhimisha Siku ya Mwanamke  Duniani, tukumbushane kushughulika na kizazi cha sasa. Tupo kisasa kiasi cha kusahau sisi tulilelewa vipi. Watoto wa kike wafundishwe masuala chanya ya kimila badala ya kufikiri kila kitu cha kimila ni kibaya,”
“Mimi watoto wangu wote nawalea sawa bila kujali wa kike au wa kiume. Wale wa kiume wote wakifikisha miaka 14 wanajua kukuna nazi, kupika nk” (Ummie Mahfoudh)
 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na taasisi nyingine nchini kulaani vikali matukio ya mauaji ya wanawake na watoto yaliyotokea hivi karibuni hapa nchini.

Kwa kadri siku zinavyoendelea mauaji ya wanawake na watoto yanayotokana na sababu mbalimbali yameripotiwa kutokea sehemu mbalimbali hasa katika maeneo ya Njombe, Rombo, Mto wa Mbu na Simiyu. 

Pamoja na matukio ya mauaji ya watoto Njombe na Simiyu, hivi karibuni  kumetokea mauaji ya wanawake Arusha na mikoa mingine.

TAMWA tunasikitishwa na mauaji hayo na tunaikumbusha jamii kuwa kila mtu anayo haki ya kuishi kulingana na sheria na taratibu za nchi yetu. 

Hivyo tukiwa wadau wanaosimamia haki za wanawake na watoto tunakemea haya na kuwataka wadau wengine kuanzia ngazi ya familia hadi serikalini kuwalinda watoto na kuhakikisha kuwa migogoro ya kifamilia inamalizwa kwa mazungumzo ya amani. 

Tumeona na tunapongeza juhudi kubwa zilizofanywa na vyombo vya usalama nchini lakini pamoja na juhudi hizo cha kujiuliza ni kuwa kwanini bado matukio haya ya mauaji yameendelea kuripotiwasiku baada ya siku? 

Tunachelea kwamba, matukio haya yasipoundiwa mifumo ya muda mrefu ili kuyakomesha kabisa, basi tutaendelea kupoteza kinamama na watoto ambao kimsingi ni nguvu kazi ya Taifa.

TAMWA tunapendekeza uwepo wa mfumo endelevu utakaohusisha wadau mbalimbali wakiwemo wananchi, vyombo vya usalama na kampuni za simu kuwezesha waathirika kutoa taarifa za dalili zozote za ukatili kabla haujatokea. 

TAMWA tunaungana na familia za waathirika wa matukio haya tukiwatakia faraja katika kipindi hiki kigumu. 

 

Rose Reuben

Mkurugenzi Mtendaji

TAMWA

 

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na taasisi nyingine nchini kulaani vikali matukio ya mauaji ya wanawake na watoto yaliyotokea hivi karibuni hapa nchini.

Kwa kadri siku zinavyoendelea mauaji ya wanawake na watoto yanayotokana na sababu mbalimbali yameripotiwa kutokea sehemu mbalimbali hasa katika maeneo ya Njombe, Rombo, Mto wa Mbu na Simiyu. 

Pamoja na matukio ya mauaji ya watoto Njombe na Simiyu, hivi karibuni  kumetokea mauaji ya wanawake Arusha na mikoa mingine.

TAMWA tunasikitishwa na mauaji hayo na tunaikumbusha jamii kuwa kila mtu anayo haki ya kuishi kulingana na sheria na taratibu za nchi yetu. 

Hivyo tukiwa wadau wanaosimamia haki za wanawake na watoto tunakemea haya na kuwataka wadau wengine kuanzia ngazi ya familia hadi serikalini kuwalinda watoto na kuhakikisha kuwa migogoro ya kifamilia inamalizwa kwa mazungumzo ya amani. 

Tumeona na tunapongeza juhudi kubwa zilizofanywa na vyombo vya usalama nchini lakini pamoja na juhudi hizo cha kujiuliza ni kuwa kwanini bado matukio haya ya mauaji yameendelea kuripotiwasiku baada ya siku? 

Tunachelea kwamba, matukio haya yasipoundiwa mifumo ya muda mrefu ili kuyakomesha kabisa, basi tutaendelea kupoteza kinamama na watoto ambao kimsingi ni nguvu kazi ya Taifa.

TAMWA tunapendekeza uwepo wa mfumo endelevu utakaohusisha wadau mbalimbali wakiwemo wananchi, vyombo vya usalama na kampuni za simu kuwezesha waathirika kutoa taarifa za dalili zozote za ukatili kabla haujatokea. 

TAMWA tunaungana na familia za waathirika wa matukio haya tukiwatakia faraja katika kipindi hiki kigumu. 

 

Rose Reuben

Mkurugenzi Mtendaji

TAMWA

 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Mwandishi wetu, Dar es salaam.

Mpiga picha wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Aika Kimaro, ameibuka mshindi wa pili katika shindano la kupiga picha za habari.

Mshindi wa kwanza katika shindano hilo alikuwa mpiga picha wa kujitegemea, Imani Isamula ambaye aliibuka kidedea kwa kura 57 dhidi ya kura 43 alizopata Aika.

Washindi hao walitangazwa juzi jijini Dar es Salaam katika mdahalo katika mdahalo ulioandaliwa na Ubalozi wa Netherland katika mwendelezo wa maonyesho ya picha (World Press Photo 2018) ambayo yanaendelea.

Imani aliibuka kidedea kutokana na picha zake za walemavu wa miguu ambapo mlameavu mmoja ni mwanamke ambaye amekimbiwa na mume wake na kuachiwa watoto ambao anawalea peke yake.

Katika picha nyingine mlemavu wa kiume ambaye licha ya ulemavu wake anaonekana kujishughulisha na shughuli za uvuvi wa samaki.

Kwa upande wa Aika moja kati ya picha zakie mbili zilizoshinda, inamuonyesha mwanamke aliyebeba mzigo wa magunia mawili yaliyofungwa kwa kamba yakiwa na chupa tupu za plastiki huku amebeba mtoto mgongoni anavuka barabara.

Akifafanua kuhusu picha hizo, Aika alisema mama huyo licha ya kuwa na shuguli nyingi nyumbani ambazo hazimuingizii kipato ameamua kumbeba mtoto wake mgongoni na kuamua kuingia mtaani kujitafutia chochote kwa ajili ya watoto wake.

“Katika picha ya pili, hawa ni watoto wanaonekana wakiwa na magunia wanaokota makopo na chupa za maji ili wakauze, picha hii inazungumza mengi, kwanza hawa ni watoto ambao wamekosa haki zao za msingi kama haki ya kusoma na haki ya kucheza,” alisema Aika.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Florence Majani, TAMWA.

Ruangwa, Lindi. Ni Januari 17 mwaka 2018, saa sita mchana. Kundi la wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za Nambilanje, wameketi mbele ya walimu wao, wakijadiliana kuhusu mila na desturi zinazokwamisha maendeleo na kuchochea mimba za utotoni katika kata hiyo.

Walimu walikuwa kimya wakifuatilia kwa umakini majadiliano hayo.  Wanafunzi  nao hawakuwa na hofu bali walitoa ya moyoni na kueleza kinagaubaga kinachoendelea majumbani.

Majadiliano hayo yaliandaliwa na Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA)  ili kuangalia mila na desturi zinazochochea mimba za utotoni na ukatili kwa wanawake na watoto.

Wanafunzi hao waliweka bayana kuwa, baadhi ya  wazazi ndicho  chanzo cha wao kufeli kwani huwalazimisha kufeli na kuwataka kuandika ‘madudu’ ili wasiendelee na masomo ya sekondari.

Mwanafunzi wa kidato cha nne, shule ya Sekondari Nambilanje, Zahara Chigope anaweka bayana  kuwa wapo wanafunzi wenzake ambao wanashurutishwa na wazazi waandike ‘madudu’ kwenye mitihani ya taifa ili wasiendelee na masomo ya sekondari.

“Mzazi wake alimwambia aandike 11111 kila swali, ili afeli na asiendelee na sekondari,” alisema.

Alisema hata kwa wale wanaofaulu darasa la saba, wapo wazazi wanaokataa kwa makusudi kuwapeleka shule wakidai hawajalipwa fedha za korosho lakini kimsingi, ni ujanja tu ili wasiendelee na masomo.

Zahara alisema mwenzao mmoja aliyekuwa anafaulu vizuri kwenye masomo wakati wakiwa shule ya msingi, alifeli na alipomdodosa imekuwaje, ndipo alipomtobolea siri hiyo kuwa aliambiwa na mama yake aaandike ‘madudu.’

“Kweli alifeli kwa sababu aliniambia aliandika 11111 katika kila swali na sasa hivi yupo mitaani amezaa na wala hajaolewa,” alisema

Mwanafunzi mwingine wa kidato cha tatu wa shule hiyo, Zena Mitawa anasema mwenzao aliyetakiwa kuwa nao kidato cha tatu, alifeli  darasa la saba kutokana na ushauri wa mama yake.

“Alikuwa anatuambia hata kabla hatujafanya mtihani wa taifa kuwa, mama yake hataki aendelee na shule kwani tayari yupo mwanaume wa kumuoa. Kweli matokeo yalipotoka, hakufaulu na sasa ameolewa huko Lindi mjini,” anasema.

Mwanafunzi mwingine, Nasma Kumkana, alisema suala la wazazi kuwashawishi wanafunzi wafeli kwa makusudi ni kubwa na wanalisikia kutoka kwa wanafunzi wenzao.

“Sio hivyo tu, hata baadhi ya wazazi tunawasikia wanasema bora mtoto afeli kwa sababu hawana hela za kumhudumia atakapoingia sekondari, hata wakiambiwa elimu ni bure watasema hawana fedha za sare za shule,” anasema

Nasma anasema mila hizo zinaambatana na ile ya baadhi ya wazazi kumshauri mtoto atafute mboga kwa jasho lake.

“Hii ina maana kwamba, mama anamwambia mtoto leo zamu yako kutafuta mboga, kwa maana nyingine,  mtoto wa kike anapewa ruhusa ya kuwa na mwanaume ili apate fedha ya kusaidia familia,” anasema.

Akizungumzia suala hilo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nambilanje, Charles Chitawala anasema tatizo hilo ni kubwa kwa kata ya Nambilanje na maeneo mengine ya Ruangwa.

“Sisi kama viongozi suala hilo linatuudhi, inabidi tutoe elimu, ili tabia hizo waziache. Ilifikia mahali ikabidi tuitishe vikao vya wazazi na wazazi wajaze mikataba,” anasema.

Anasema mwaka 2018, wazazi walijaza mikataba na kukubaliana kuwa iwapo mzazi atabainika kuwa alimshauri au kumlazimisha mwanafunzi kufeli kwa namna yoyote ile, basi atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mwalimu Chitawala anasema mikataba hiyo ilitolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na kusainiwa na wazazi wa wanafunzi waliomaliza darasa la saba mwaka jana.

Mratibu wa Elimu kata ya Nambilanje, Lista Mziwanda anasema suala la wazazi kuwalazimisha wanafunzi kuandika  ‘utumbo’ kwenye mitihani ya taifa lipo kwa kiasi kikubwa eneo hilo ingawa hakuna takwimu rasmi.

“Tulizibaini kesi hizo baada ya kuwabana wanafunzi ambao tuliwategemea kufaulu lakini hawakufaulu. Ukikaa na mtoto vizuri anakuambia ukweli kuwa alilazimishwa na mama,” anasema

Anasema kesi hizo ni za wanafunzi ambao walifaulu vizuri kwenye mitihani ya ndani na ile ya kujipima ‘Mock’ lakini mitihani ya taifa walifeli.

“Kinachofanyika sasa ni kutoa elimu lakini na hizo sheria ndogondogo kama kuwasainisha wazazi mikataba kuwa wakibainika kuwalazimisha watoto wafeli, watachukuliwa hatua. Tumeanza suala la mikataba mwaka jana, tutaangalia mwaka huu,”anasema.

Mwalimu Mziwanda anasema kati ya wanafunzi 76 waliomaliza darasa la saba mwaka 2018, 66 walifaulu kwenda Sekondari na wanne wamekwenda Chuo cha ufundi Nkoye. Mwananchi ilibaini kuwa, mazingira ya kielimu wilayani humo ni magumu kwa baadhi ya wanafunzi ambao hulazimika kubaki  peke yao kwa muda mrefu baada ya  wazazi wao kuondoka nyumbani na kwenda kukaa shambani msimu wa kilimo.

 Mwanafunzi wa shule ya msingi Nambilanje Swaumu Ibadi anasema  mazingira ya kielimu kwake  ni magumu kwa sababu mama yake yupo shambani kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.

“Jana usiku sijala, mpaka mchana huu kwa sababu nakaa peke yangu, mama amehamia mashambani na dada yangu niliyeachwa naye, ameondoka,” anasema

Anasema akibahatika kula, basi ni milo miwili tu kwa siku na wakati huo akitembea umbali wa karibu kilometa10 kutoka nyumbani hadi shuleni.

Saumu ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba, anasema hana mahitaji muhimu ya shule kama sare, madaftari na chakula kwa sababu mama yake hajamnunulia.

Kwa mujibu wa Mtendaji wa Kijiji cha Nambilanje, Constatine Odilo, desturi za wazazi kuhamia shambani kipindi cha kilimo zinachangia  kushuka kwa kiwango cha elimu na hata mmomonyoko wa maadili.
“Tunapokea kesi nyingi hapa kijijini za watoto wadogo wa kike kuachwa peke yao nyumbani wakati wazazi wakiwa wamehamia shambani, hili linachangia watoto hawa kuwa huru na hata wasipoenda shule, nani atawajibika?” anasema.

Familia zachangia kushuka kwa elimu, kuvunjika kwa maadili

Pamoja na wazazi kuhujumu elimu ya watoto wao, mambo mengine yanayotajwa kusababisha mimba za utotoni  na kushuka kwa kiwango cha elimu eneo hilo ni wazazi kutengana.

Kwa mfano, Mtendaji wa Kata ya Nambilanje, Abdallah Tamba anasema  kesi nyingi za wazazi kutengana ni nyingi na hali hiyo husababisha watoto kubaki bila malezi.

“Kwa mila za huku, kuachana ni kitu rahisi tu, kama ilivyo kuoa. Kwa hiyo mara nyingi wazazi wanapotengana, watoto ndiyo hupata tabu, wanakosa malezi kabisa,” anasema

Anasema mara nyingi baba anapobaki na watoto, huoa mke mwingine na kama mama huyo hatajali suala la elimu, basi watoto huacha shule.

Lakini watoto wa eneo hilo wanasema wazi kuwa mfumo wa  matrilineal (mama kuwa kichwa cha familia) wa kabila za kusini, ndiyo huchangia changamoto hizo.

Kwa mfano, Nasra Juma, Mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari Nambilanje anasema baadhi ya kinamama ndiyo wanaowaambiwa watoto wao wa kike wasiende shule bali washiriki kuleta mboga nyumbani.

“Sasa mama anamwambia binti yake kuwa leo zamu yako kuleta mboga, hiyo ina maana kuwa anamruhusu kwenda kufanya chochote ili alete mboga nyumbani,” anasema

Mila nyingine zinazotajwa kuchangia kushuka kwa elimu ni unyago ambao hufanyika kipindi cha masomo.

Meneja Ufuatiliaji na Tathmini wa TAMWA, John Ambrose anasema zipo mila na desturi zenye manufaa kwa jamii lakini endapo mila hizo zinachochea mimba, kushuka kwa elimu, zinamzuia mtoto kupata haki yake basi hazina budi kupingwa.

“Ndiyo maana tumeandaa midahalo hii, kwa kushirikiana na Taasisi ya Foundation for Civila Society, ili wanafunzi waeleze wazi yanayowasibu nyumbani, shuleni na katika mazingira yao mengine, tumeshuhudia mengi yanayofanyika kwa watoto na yanachangia ukatili kwao,” anasema Ambrose

Latest News and Stories

Search