News/Stories

TAMWA YAFANYA UCHAGUZI WAKE MKUU

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
 
Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) leo Agosti 27, kimefanya uchaguzi wake Mkuu wa mwaka na kumchagua Joyce Shebe kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.
 
Shebe ambaye ni Mhariri Mkuu wa Clouds Media Group, ataongoza kwa miaka mitatu. Huu ni muhula wa pili kwa Shebe baada ya kuongoza miaka mitatu ya mwanzo kuanzia 2019. Katika uchaguzi huo, Shebe alikuwa akichuana na Mwasisi wa TAMWA, Lyela Sheikh.
 
Nafasi nyingine katika uchaguzi huo ni wajumbe wa bodi, ambapo Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Tumaini, Mary Kafyome, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha St Augustine, Dk Kaanaeli Kaale nao walichaguliwa kuwa wajumbe wa bodi ya Tamwa.

Latest News and Stories

Search