News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

TAMKO LA ASASI ZA WANAWAKE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Dar –Es- Salaam, Oktoba 23, 2025.
Wakati Watanzania wakielekea katika tukio la kikatiba la kupiga kura mnamo Oktoba 29, muunganiko wa asasi za kiraia zinazotetea makundi maalum ikiwamo wanawake, watoto na vijana wanawake, tumeungana kwa pamoja kuhimiza umma kuhusu ajenda muhimu ya ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi sambamba na kuhimiza ushiriki wa wanawake katika upigaji kura siku ya Oktoba 29 mwaka huu.

Ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi ni miongoni mwa vipaumbele vya asasi za kiraia zenye mrengo wa jinsia. Kwa sababu tunaamini wakiwapo viongozi wanawake, kutakuwa na hatua mahsusi katika kuongeza kipato na maendeleo ya mwanamke.

Hivyo basi sisi muunganiko wa asasi za kiraia, tunawahakikishia kuwa tunakwenda kutimiza wajibu wetu wa kikatiba wa kupiga kura na kadhalika tunahimiza wanawake kwenda kushiriki katika mchakato wa kikatiba wa kupiga kura, ili tunapokwenda kuwachagua viongozi wetu, basi tuwatwike mzigo wa mambo ya msingi yanayowahusu wanawake .

Viongozi hawa tutakaowachagua, tunaamini kuwa baada ya mchakato huo, tutawatwika madai yetu ya kimaendeleo yanayowahusu wanawake, watoto, wanawake vijana na watu wenye ulemavu na ajenda nyinginezo za mrengo wa jinsia.

Tanzania ni miongoni mwa nchi chache za Afrika ambazo zimepiga hatua katika ajenda ya ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi. Kwa mara ya kwanza Tanzania imepata kiongozi mkuu wa nchi mwanamke, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, ambaye pia anawania kiti hicho cha urais kwa tiketi ya CCM.

Kadhalika, mwaka huu kumekuwa na wagombea wengine wanawake wa urais, akiwemo Saumu Rashid kutoka UDP na Mwajuma Mirambo –UMD.

Kwa upande wa wagombea wenza wa urais kutoka vyama vingine ni pamoja na Eveline Wilbard Munis (NCCR), Husna Mohamed Abdallah (CUF), Aziza Haji Selemani (D. MAKINI), Amani Selemani Mzee (TLP), Chausiku Khatibu Mohamed (NLD), Sakia Mussa Debwa (SAU), Chuma Juma Abdallah na Devotha Minja (CHAUMA).

Hii ni hatua kubwa ya kidemokrasia kwa Tanzania na kwa ajenda ya ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi.

Tunapokaribia uchaguzi mkuu, tunapenda kuwakumbusha Watanzania kuwa mwanamke kiongozi anaposhika madaraka asihukumiwe kwa jinsia yake, bali kwa uwezo, uzoefu na dira yake ya maendeleo.

Ikumbukwe kuwa uongozi wa mwanamke si tishio bali ni nyenzo ya kuimarisha demokrasia jumuishi, yenye kusikiliza na kutenda kwa manufaa ya wote.

Tunapenda kuikumbusha jamii kuwa katika kipindi hiki cha kampeni na uchaguzi, ni muhimu kuepuka lugha za kejeli, udhalilishaji na mashambulizi ya kibinafsi — hasa kwa misingi ya kijinsia. Badala yake, mjadala wa kisiasa ujikite katika sera, ilani, na hoja zenye kujenga taifa.

Wanawake wanaowania nafasi kuanzia ngazi ya udiwani hadi urais, wasibezwe, wasitukanwe, na tunakemea vikali lugha dhalili zinazotweza utu kwa wanawake wanasiasa na viongozi wengine wanawake.

Bado tunaamini kuwa kwa kumpata Rais mwanamke Tanzania imepiga hatua kubwa kupitia yeye katika kutekeleza Dira ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDG 5) inayosisitiza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake katika maamuzi.

Kupitia Rais huyu mwanamke tumeona sheria kadhaa zikibadilishwa ikiwamo ya vyama vya siasa na hata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwamo ya afya.

Asasi za kiraia zinasimama imara katika kuhakikisha kuwa mafanikio haya yanaendelezwa, si kwa maneno tu bali kwa vitendo.

Ushiriki wa wanawake katika siasa unaongeza uwajibikaji, uwazi, na ustawi wa kijamii, kwa kuwa tafiti nyingi zinaonesha kwamba wanawake viongozi wanapendelea sera zinazogusa elimu, afya, haki za watoto, na usawa wa kiuchumi. Kama zipo changamoto kupitia uongozi wake basi si muda wa kumkashifu kwa kupitia jinsia yake.

Tunapenda pia kuikumbusha Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), vyama vya siasa, na wadau wote kuhakikisha mazingira ya uchaguzi yanakuwa salama, jumuishi, na huru dhidi ya vitisho, udhalilishaji, na ukatili wa kijinsia, ambao mara nyingi huwakatisha tamaa wanawake kushiriki kikamilifu katika siasa.

Tunatoa wito kwa vyombo vya habari kuendelea kutoa nafasi sawa kwa wagombea wanawake kuratibu midahalo, makala, na mijadala inayojenga uelewa wa umma juu ya uwezo na mchango wa wanawake katika maendeleo ya taifa.

Kwa muktadha huu, tunasema: “Uongozi bora hauna jinsia — una maadili, dira, na dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi.”

Tunaamini kuwa taifa lenye usawa wa kijinsia katika uongozi ni taifa lenye amani, ustawi, na maendeleo endelevu.Tanzania ni yetu sote — wanawake na wanaume wanapaswa kushiriki kwa usawa katika kuijenga.

Imetolewa na:
Muunganiko wa Asasi za Wanawake na Watetezi wa Usawa wa Kijinsia – Tanzania

(Oktoba 23, 2025 – Dar es Salaam)

  1. Ulingo Wanawake

  2. Women Walfare Tanzania

  3. TAMWA

  4. Binti Makini-

  5. WAJIKI-

  6. WILDAF-

  7. WFT-

  8. Young and Alive

  9. Generation Act

  10. TAWIA

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Dar es Salaam, Septemba 10, 2025.Chama cha WanahabariWanawake Tanzania (TAMWA) kinatoapongezizadhatikwawanawakewotewaliojitokezakuwanianafasizauongozikuanziangaziyaudiwaniubungehadiuraiskatikamchakatowa uchaguzimkuu wa Oktoba 29, 2025.

Mchakatowauteuzinauchukuajifomuumeonyeshaarinamwamkomkubwa wa wanawakekushirikikwenyenafasimbalimbalizauongozinchiniKwamujibuwatakwimuzaUlingoWanawakejumlayawanawake 231 walichukuafomuzaubungekupitia CCM, nakatiyao 25 waliteuliwanachamananewakiwaniwapyaAidhamwakahuuvyamavingivyasiasavimeongezaidadiyawanawakewagombeawenzakatikanafasiyauraisnamakamu wa Rais.

Kwanamnayakipekee, TAMWA inampapongezizapekeeMheshimiwaSamiaSuluhu Hassan, aliyeteuliwana CCM kuwamgombea wa kwanza mwanamke wa uraiskatikahistoriayachamatawala.Hiinihatuakubwanayakihistoriainayoashiriamapinduzinamwelekeompya wa ushiriki wa wanawakekatikauongozi wa juunchini

PiatunawatambuawanawakewenginewalioteuliwakugombeauraispamojanawagombeawenzaakiwamoMwajumaNotyMiramboaliyechukuafomuyakuwaniauraiskupitia Chama cha Union for Multiparty Democracy (UMD), akiwanamgombeamwenzaMashavuAlawiHaji.Wagombeawenza w niEvelineWilbardMunis- NCCR, Husna Mohamed Abdallah-CUF, Aziza Haji Selemani-MAKINI, Amani Selemani Mzee-TLP, ChausikuKhatibu Mohamed-NLD, Sakia Mussa Debwa-SAU,  ChumaJumaAbdallahnaDevothaMinja- CHAUMA. 

TAMWA inatambuanakuthaminiujasirinakujitumakwawanawakewotewaliojitokeza au kujaribukugombeanafasihizilichayachangamotombalimbalizinazowakabili.

Kwamudamrefu, TAMWA imekuwamstariwambelekuhamasishaushiriki wa wanawakekatikasiasanauongozikupitiawarshamakongamanomijadalanavyombovyahabariilikuondoavikwazovinavyowakabiliwanawakeMafanikiohayanihatuamuhimukuelekealengo la kuonawanawakewakiongozakatikangazizamaamuzinakuchocheausawa wa kijinsia.

RipotiyaOfisiya Taifa yaTakwimu (NBS) inaoneshakuwahadiFebruari 2024, wanawakewalikuwaasilimia 37.4 yawabunge (148 katiya 392), wengiwaowakiwakupitiavitimaalum.RipotizaAprilinaJulai 2024 zinaonyeshaasilimia37.5 yamawaziriniwanawake.

Lichayamafanikiohayabadojamiiinakabiliwanachangamotozinazotokanana  mfumodumenaudhalilishaji wa wanawakehasakwenyemitandaoyakijamii. TAMWA inaendeleakutoaelimukupitiavyombovyahabarikuhakikishawanawakewanasiasawanashirikikampenikatikamazingirarafikiyenyeusawanausalamakamailivyo wa wagombeawanaumebilakubaguliwakwamisingiyajinsia.

Uwepowawanawakekwenyeuongozinimuhimukwamaendeleoyataifakwanihuletausawa wa kijinsiakatikajamiiuwajibikajinakulindamaslahiyamakundiyotehususanwanawakenawatotoKukosekanakwawanawakekatikanafasizajuukunadhoofishautekelezaji wa sheriana sera zakulindahakizawanawakenawatotoikiwemokupambananaukatili wa kijinsiandoanamimbazautotoniukeketajinaudhalilishaji wa kijinsianamakundiyawatuwenyemahitajimaalum.

TAMWA inasisitizaniwajibu wa jamiivyamavyasiasaserikalinawadau wa maendeleokuhakikishawanawakewanapatanafasisawakwenyesiasanauongoziilikujengataifalenyeusawa wa kijinsiaamaninamaendeleoendelevu.

Kadhalikatunatoawitowakampenisafinajumuishizenyestahazinazolengakujengaustawinautu wa jamiibadalayasiasazamatusinakejeliTamwainafuatilia  kampenikatikangazizotenahaitasitakuripotimgombeayeyote au kundiambalolitakiuka  kanunizauchaguziilisheriaichukuemkondowake.

Dkt. Rose Reuben

Mkurugenzi  Mtendaji.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Dar es Salaam, Septemba 9, 2025Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinawapongeza wanawake wote waliojitokeza kuwania nafasi za uongozi kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na urais.

Mchakato wa uteuzi wa watia nia na uchukuaji fomu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, umefanyika hapa Tanzania, na TAMWA imeona ari kubwa kwa wanawake kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali.

Taasisi ya Ulingo Wanawake, imefanya majumuisho na kupata takwimu zinazoonyesha ongezeko la wanawake waliojitokeza kwenda majimboni.

Takwimu zinaonyesha kuwa,  wanawake 231 walijitokeza kuchukua form za ubunge kupitia chama cha CCM na kati yao walioshinda na kupitishwa na chama ni wanawake 25. Kati ya hao 25, wanane ni wapya. 

Pamoja na ubunge kadhalika, mwaka huu umeona mwamko wa vyama vya siasa kuwateua wanawake kama wagombea wenza,Eveline Wilbard Munis- NCCR, Husna Mohamed Abdallah-CUF, Aziza Haji Selemani-MAKINI, Amani Selemani Mzee-TLP, Chausiku Khatibu Mohamed-NLD, Sakia Mussa Debwa-SAU

Wengine ni Chuma Juma Abdallah na Devotha Minja- CHAUMA. Huku CCM ikiteua mgombea urais mwanamke, ambaye ni Samia Suluhu Hassan. Licha ya baadhi ya watia nia wanawake kuenguliwa na vyama vyao, TAMWA imeona dhamira na ujasiri wao wa kushiriki katika uchaguzi. Kwa wanawake waliopitishwa na vyama vyao kuwania uongozi, tunawapa pongezi kwa kuonyesha moyo wa uthubutu na nia ya kushiriki nafasi za juu za uongozi.

Kwa bahati mbaya, hatukuweza kupata takwimu sahihi za waliojitokeza kuwania ubunge katika vyama vingine. 

Kwa muda mrefu, TAMWA imekuwa mstari wa mbele kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi kupitia warsha, makongamano, mijadala ya wazi pamoja na kutumia vyombo vya habari ili kufikisha ujumbe wa kuondoa vikwazo vinavyowanyima wanawake fursa ya kushiriki kikamilifu katika ngazi za maamuzi.

Kwa nafasi ya Urais, TAMWA inawapongeza wanawake wote waliojitokeza na kuteuliwa na vyama vyao kugombea nafasi ya juu kabisa ya uongozi, akiwamo Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa upande wa CCM, na Bi Saum Rashid wa UDP. Aidha, tumeona pia idadi kubwa ya wanawake waliojitokeza kuwania ubunge katika majimbo mbalimbali ya uchaguzi, jambo linaloashiria mwelekeo chanya wa ushiriki wa wanawake katika siasa.

Kwa TAMWA, hatua hizi ni mafanikio makubwa kwa sababu ajenda yetu kuu ni kuona wanawake wanashika nafasi za juu za uongozi na maamuzi, ili kuleta mabadiliko yenye kuzingatia usawa wa kijinsia.

Ripoti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) inaonyesha kuwa, hadi kufikia Februari  2024, wanawake walishikilia asilimia 37.4 ya viti vya Bunge nchini Tanzania, ikiwa ni jumla ya wabunge 148 kati ya 392 ambapo uwakilishi mkubwa unatokana na viti maalum. 

Idadi ya wanawake katika nafasi za uwaziri inatofautiana, ambapo ripoti ya NBS Aprili 2024 na Julai 2024 zinaonyesha kuwa kulikuwa na mawaziri saba na kwamba asilimia 37.5 ya mawaziri ni wanawake, mtawalia. 

Licha ya mafanikio haya makubwa lakini bado tunaamini wapo wanawake wanaozuiwa kushiriki nafasi za uongozi kutokana na mfumo dume, wapo wanawake wanaodhalilishwa mitandaoni kutokana na nafasi zao za uongozi. 

Hivyo basi tunapoendelea kupata mafanikio haya, bado juhudi za dhati zinahitajika kuhakikisha wanawake wanasiasa wanafanya siasa kwa usalama  kama wanaume katika mchakato wa uchaguzi ikiwa ni pamoja kupiga kura, kuchagua na wanaotaka kutia nia kwenye uongozi hawabaguliwi kutokana na jinsia zao. 

Tunaamini kwa dhati kwamba uwepo wa wanawake katika ngazi za juu za uongozi ni muhimu kwa maendeleo ya taifa kwa sababu wanawake huleta mtazamo wa kipekee katika uongozi, husimamia kwa uwajibikaji zaidi, na mara nyingi hulinda maslahi ya makundi yote ya jamii, hususan watoto, vijana na wanawake wenzao.

“Kukosekana kwa wanawake katika ngazi za juu za uongozi kunadhoofisha utekelezaji wa sheria na sera zinazolenga kulinda haki za wanawake na watoto. Uwepo wao utahakikisha uimarishaji wa sheria za kuzuia ukatili wa kijinsia, ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, ukeketaji, ubakaji, ulawiti pamoja na udhalilishaji wa kijinsia unaoenea kupitia mitandao ya kijamii.”

Kwa msingi huo, TAMWA inaendelea kusisitiza kuwa ni wajibu wa jamii nzima, vyama vya siasa, serikali na wadau wa maendeleo kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi sawa ya kushiriki kwenye siasa na kushika nafasi za uongozi, ili kujenga taifa lenye usawa, amani na maendeleo endelevu.

Kadhalika wakati tayari kampeni zikiwa zimeanza, TAMWA tunahimiza siasa safi, jumuishi, zenye staha zinazolenga kujenga ustawi, utu wa jamii nzima badala ya kampeni zenye matusi, dhalili na kebehi. 

Mkurugenzi Mtendaji

Dkt Rose Reuben

TAMWA

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

TERMS OF REFERENCE (ToR)

Consultancy to develop gender mainstreaming methodology guidelinesfor the Tanzanian Media Sector

1. Background

Tanzania Media Women’s Association (TAMWA) has played a pivotal role in promoting gender equality and mainstreaming within the media landscape of Tanzania. From 2020 to 2023, TAMWA supported four media housesZanzibar Broadcasting Corporation (ZBC), Zanzibar Leo, Afya FM, and Dodoma Media Group (DMG)to strengthen gender-responsive practicesincluding the development and implementation of gender policies, documentation of sexual harassment cases, and establishment of functional gender desks.

In 2025, TAMWA conducted a follow-up with these media houses to evaluate the progress of the earlier interventions and assess the sustainability of gender mainstreaming efforts. Moreover, TAMWA engaged nine media houses out of the previous one for purpose of making comparison analysis of the state in terms of those supported and those have not been in the project to explore emerging and innovative best practices.

Building on the lessons learned, TAMWA now plans to refine and document its gender mainstreaming methodology,mapping best practices from various media houses and developingcomprehensive, context-specific guidelines to support media houses across Tanzania to adopt transformative and sustainable gender mainstreaming practices.These guidelineswill be shared and discussed with other media stakeholdersfor their validation and buy-in.

2. Purpose of the Assignment

The purpose of this consultancy is to review, refine, and document a gender mainstreaming methodology guideline document based on evidence gathered from past interventions, follow-up assessments, and comparison between TAMWA supported and othernon-supported media houses. The guideline should be practical, adaptable, and tailored to the Tanzanian media context.It is intended to address both internal operations and content creation within media houses, promoting equal representation and challenging harmful gender stereotypes. 

3. Specific Objectives

i. To assess TAMWA’s gender mainstreaming efforts by reviewing past tools, reports, and institutional practices, complemented by a stakeholder dialogue session to validate findings and identify best practices.
ii. To refine and document a practical Gender Mainstreaming Methodology Guideline tailored to the Tanzanian media context

4. Scope of Work

Under the overall guidance of TAMWA, the consultant will:

• Conduct a review of TAMWA’s previous gender mainstreaming tools, reports, and assessments (2020–2025).
• Analyze existing gender policies, sexual harassment protocols, and related institutional documentation from participating media houses.
• Analyzing qualitative and quantitative data on:
Gender policy implementation
Functionality of gender desks
Sexual harassment reporting and response systems
Editorial and content production approaches from a gender lens
Institutional culture and leadership commitment to gender mainstreaming
Best practices and innovation in gender integration
• Facilitate a stakeholder dialogue session,present preliminary findings and lead discussions to validatefindings, shareexperiences, and document best practiceschallenges and learnings
• Assessing current practices, mapping successful examplesof gender mainstreaming at work in mediaand developing context-specific guidelines
• Draft the gender mainstreaming methodology guidelines for media in Tanzania.
• Ensure the guideline includes:
An elaboration of the context within which gender mainstreaming efforts are being conducted.
Step-by-step guidance on effective gender integration in media houses and newsrooms in particular
Assessment tools that media houses can use to evaluate gender mainstreaming progress.
Case studies and success stories from the media sector, particularly from TAMWA supported media
Implementation roadmap and monitoring framework
• Revise and finalisethe guidelines based on feedback from TAMWA and stakeholders.

5.Key Deliverables and Duration – Summary

The consultancy will run over a period of four weeks and will produce the following key deliverables: an inception report outlining the methodology, tools, and workplan; a desk review summary and assessment tools with accompanying analysis; a dialogue session report; a draft gender mainstreaming methodology guideline; and a final, revised, and validated guideline.

6. Consultant Profile and Qualifications

• Advanced degree in gender studies, media, development studies, or related fields.
• Minimum 5 years of experience in gender mainstreaming, particularly in media.
• Proven ability to develop practical toolkits and policy guidelines.
• Strong skills in qualitative and quantitative survey.
• Experience facilitating stakeholder dialogues or peer learning events.
• Fluency in Kiswahili and English.
• Familiarity with the Tanzanian media environment is essential.

7. Application Process

Interested individual consultants should submit the following:

• Technical proposal outlining understanding of the assignment, proposed methodology, and timeline.
• Financial proposal (inclusive of all costs and taxes).
• CV(s) of lead consultant and any team members.
• Examples of previous similar assignments.
• At least two referees.

Applications should be submitted no later than 07 September2025 to This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.with the subject line: Consultancy – Gender Mainstreaming Methodology Guideline.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Baada ya miaka 6 ya mafanikio makubwa, Joyce Shebe anamaliza muda wake kama Mwenyekiti wa bodi ya TAMWA.

Amewaachia wanachama kumbukumbu ya #TuzozaSamia Kalamu, maadhimisho ya miaka 36 ya TAMWA, na uwekezaji imara wa taasisi.
Asante kwa uongozi uliotukuka! 

#TAMWAAGM #TAMWA #JoyceShebe #WanawakeViongozi #MafanikioYaUongozi #TuzoZaSamiaKalamu

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Dk. Kaanaeli Kaale ameanza rasmi safari ya kuongoza Bodi ya TAMWA kwa miaka mitatu baada ya kuchaguliwa na wanachama wa TAMWA katika Mkutano Mkuu uliofanyika jijini Dsm tarehe 28 June 2025 .

Dk. Kaale ameahidi kuendeleza mafanikio ya waliotangulia na kuhimiza matumizi ya TEHAMA, usawa wa kijinsia na uandishi wa haki kipindi hiki cha uchaguzi. 

#TAMWAAGM2025 #TAMWA #WanawakeViongozi #UsawaWaKijinsia #HabariNaTEHAMA

Page 1 of 21

Latest News and Stories

Search