News/Stories

TAMWA YAUNGANA NA KISARAWE KUADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA KIKE

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
 

Godwin Assenga, Tamwa

Kisarawe. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kimeadhimisha Siku ya mtoto wa kike  Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. 

Maadhisho hayo yalifanyika kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe na wadau wa masuala ya jinsia.

 Siku ya mtoto wa kike huadhimishwa Oktoba 11 kila mwaka ambapo mwaka huu maadhikisho hayo yamebebwa na kauli mbiu isemayo; “Imarisha uwezo wa mtoto wa kike” Tokomeza Ukeketaji, Mimba na Ndoa za Utotoni.

Maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kazimzumbwe iliyopo Wilaya ya Kisarawe na kuhudhuriwa na mgeni rasmi ambaye  ni Mkurugenzi mtendaji wa halmashari ya Kisarawe, Mussa Gama. 

Katika maadhimisho hayo watoto walipata fursa ya kufikisha ujumbe wao mbele ya mgeni rasmi kwa njia mbalimbali ikiwamo maigizo, ngonjera na risala.

Pia TAMWA kwa kushirikiana na kampuni ya Asas Diary waligawa maziwa kwa wanafunzi walioshiriki maadhimisho hayo. 

 

 

Wanafunzi toka shule mbalimbali wilayani Kisarawe wakifanya  maandamano

 

Mmoja wa wanafunzi akizungumza jambo mbele ya mgeni rasmi na wageni waalikwa

 

Kikundi cha skauti kisarawe wakionyesha gwaride mbele ya mgeni rasmi

 

Kikundi cha maigizo kisarawe kikifanya igizo la madhara ya ukeketaji mbele ya mgeni rasmi

 

Latest News and Stories

Search