Press Release

TAMWA SEKRETARIATI MPYA MTANDAO WA USHIRIKI WA WANAUME NA WAVULANA KATIKA MASUALA YA JINSIA (MEN ENGAGE TANZANIA - MET)

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
 

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kimethibitishwa na kutangazwa kuwa Sekretarieti mpya ya Mtandao wa Ushiriki wa  Wanaume na Wavulana katika masuala ya Jinsia (Men Engage Tanzania MET).

TAMWA imepewa jukumu hilo baada ya kufanyiwa tathmini na Shirika la Wanaume na Wavulana katika masuala ya Jinsia (Men Engage Afrika MEA) mapema mwaka huu baada ya Mtandao huo nchini kuratibiwa na shirika la Child Diginity Forum (CDF) kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita. 

Katika jukumu hilo TAMWA itaendeleza historia yake ya utetezi wa haki za binadamu kwa mrengo wa kijinsia kwa kuwahusisha wanaume na wavulana kupinga ukatili na kuhamasisha mawasiliano kuanzia ngazi ya familia, jamii, kitaifa hadi kimataifa. 

Pamoja na hilo, TAMWA imepewa jukumu la kufanya kazi pamoja na mashirika wanachama katika kujengeana uwezokuhamasisha haki, usawa,na kupambana na ukatili kijinsia.

Mtandao wa MEA una mashirika wanachama takribani 31nchini huku ukiwa na jumla ya mashirika wanachama zaidi ya 400 kutoka  Afrika, Amerika ya Kusini,Amerika ya Kaskazini, Asia na Bara la Ulaya.

Mkurugenzi Mtendaji

TAMWA

Search