News/Stories

UJUMBE WA UMMY MAHFOUDH: SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
 

Wakati dunia ikisherehekea Siku ya Wanawake Duniani, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA) kinakuletea wanahabari wakongwe waanzilishi wa TAMWA. Hiki ndicho wanachokisema katika maadhimisho haya ya Siku ya Wanawake Duniani.

Ummy Mahfoudh.  Ni mwanahabari mkongwe, Mwanachama wa Chama cha Wanahabari  Wanawake tangu 1988. Amewahi kufanya kazi katika taasisi zisizo za kiserikali za kitaifa na kimataifa katika nchi za Uingereza, Denmark, Tunisia na Afrika Kusini.
Ni miongoni mwa walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika mkutano wa kidunia wa haki za mwanamke, maarufu mkutano wa Beijing mwaka 1995. Amewahi kushiriki utafiti wa chanzo cha mauaji ya wanawake wazee kutokana na imani za kishirikina na mauaji ya albino Tanzania. 
 Kwa sasa ni mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya magazeti Zanzibar
Ni mshairi, ana mume na watoto wanne. 
Anachokisema katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Tanzania;
“Katika kuadhimisha Siku ya Mwanamke  Duniani, tukumbushane kushughulika na kizazi cha sasa. Tupo kisasa kiasi cha kusahau sisi tulilelewa vipi. Watoto wa kike wafundishwe masuala chanya ya kimila badala ya kufikiri kila kitu cha kimila ni kibaya,”
“Mimi watoto wangu wote nawalea sawa bila kujali wa kike au wa kiume. Wale wa kiume wote wakifikisha miaka 14 wanajua kukuna nazi, kupika nk” (Ummie Mahfoudh)
 

Latest News and Stories

Search