Press Release

Siku ya 16 ya Kupinga Ukatili Ambayo Pia ni Maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
 

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na mashirika mbalimbali dunianikuadhimisha Siku ya Haki za Binadamuyenye kauli mbiu Haki Zetu, Mustakabali WetuHatma Yetu, NSasa” (Our Rights, Our Future, Right Now) kwa kuzingatia maadili, kujali usawa na kulinda haki za wanawake na watoto kwa maendeleo endelevu.

Katika maadhimisho hayo leo ndio kilele cha kampeni ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia Duniani yenye Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inasema, “Kuelekea Miaka 30+ ya Beijing: Tuungane Kumaliza Ukatili wa Kijinsia kwa Wanawake na Watoto.”

Ni umuhimu jamii kushirikiana kuimarisha maadili ya watoto na kupinga ukatili wa kijinsia, ambao bado ni changamoto kubwa hasa mauaji ya wenzakuwekeza katika ustawi wa watoto kwa mustakabali ymaendeleo ya taifa.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali zinazohusu makuzi ya watoto, inaonyesha kuwa watoto wanapopewa msingi mzuri wa maadili, wanakua wenye utu, heshima, na kuwa nmchango mkubwa kwa jamii. Hata hivyo, kutokana na changamoto mbalimbali za kiuchumi, teknolojiakuporomoka kwa maadili, ukatili wa kijinsia, na unyanyasaji katika jamii au familia ukuaji wa watoto katika kujiamini, ubunifu vinaathiriwa. 

Katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatii wa jinsia, TAMWA tunaendelea kuwasisitiza wazazi, walezi, walimu, na jamii kwa ujumla juu ya umuhimu wa kuwajenga watoto katika misingi ya maadili, kuwafundisha kuheshimu haki za binadamu, kujua hatari za ukatili wa kijinsia na jinsi ya kuripoti matukio ya ukatili wanapokabiliana nayo.

Ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto ni kikwazo chamaendeleo ya kijamii, kiuchumi, na kisiasa kwa kuwa ndo waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia ambao unajumuisha ndoa za utotoni, ukeketaji, vipigo, ulawiti, na unyanyasaji wa kingono.

Huku tukihitimisha siku 16 za kupinga ukatili, na siku ya Haki za Binadamu, TAMWA tunasisitiza kuwa vita dhidi ya ukatili wa kijinsia kuendelea kukemewna wahusika wa vitendo vya kukatili kuchukuliwanahatuaza sheria ili kujenga jamii inayoheshimu haki za binadamu.

Kwa heshima ya siku hii muhimu, TAMWA inatoa wito kwa jamii nzima kushirikiana kwa dhati katika kuhakikisha kuwa watanzania wote na hasa wanawake na watoto wanalindwa dhidi ya ukatili na sauti za waathirika wa ukatili zinasikilizwa

Dkt. Rose Reuben

Mkurugenzi Mtendaji

Search