- TAMWA
- Hits: 463
Planned results for 2009-2014 Strategic plan
Expected outputs
The expected outputs of the TAMWA interventions for the coming Six years include:
We humbly request for you support to enable us realize plan.
Dar es Salaam, Septemba 9, 2025. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinawapongeza wanawake wote waliojitokeza kuwania nafasi za uongozi kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na urais.
Mchakato wa uteuzi wa watia nia na uchukuaji fomu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, umefanyika hapa Tanzania, na TAMWA imeona ari kubwa kwa wanawake kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali.
Taasisi ya Ulingo Wanawake, imefanya majumuisho na kupata takwimu zinazoonyesha ongezeko la wanawake waliojitokeza kwenda majimboni.
Takwimu zinaonyesha kuwa, wanawake 231 walijitokeza kuchukua form za ubunge kupitia chama cha CCM na kati yao walioshinda na kupitishwa na chama ni wanawake 25. Kati ya hao 25, wanane ni wapya.
Pamoja na ubunge kadhalika, mwaka huu umeona mwamko wa vyama vya siasa kuwateua wanawake kama wagombea wenza,Eveline Wilbard Munis- NCCR, Husna Mohamed Abdallah-CUF, Aziza Haji Selemani-MAKINI, Amani Selemani Mzee-TLP, Chausiku Khatibu Mohamed-NLD, Sakia Mussa Debwa-SAU
Wengine ni Chuma Juma Abdallah na Devotha Minja- CHAUMA. Huku CCM ikiteua mgombea urais mwanamke, ambaye ni Samia Suluhu Hassan. Licha ya baadhi ya watia nia wanawake kuenguliwa na vyama vyao, TAMWA imeona dhamira na ujasiri wao wa kushiriki katika uchaguzi. Kwa wanawake waliopitishwa na vyama vyao kuwania uongozi, tunawapa pongezi kwa kuonyesha moyo wa uthubutu na nia ya kushiriki nafasi za juu za uongozi.
Kwa bahati mbaya, hatukuweza kupata takwimu sahihi za waliojitokeza kuwania ubunge katika vyama vingine.
Kwa muda mrefu, TAMWA imekuwa mstari wa mbele kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi kupitia warsha, makongamano, mijadala ya wazi pamoja na kutumia vyombo vya habari ili kufikisha ujumbe wa kuondoa vikwazo vinavyowanyima wanawake fursa ya kushiriki kikamilifu katika ngazi za maamuzi.
Kwa nafasi ya Urais, TAMWA inawapongeza wanawake wote waliojitokeza na kuteuliwa na vyama vyao kugombea nafasi ya juu kabisa ya uongozi, akiwamo Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa upande wa CCM, na Bi Saum Rashid wa UDP. Aidha, tumeona pia idadi kubwa ya wanawake waliojitokeza kuwania ubunge katika majimbo mbalimbali ya uchaguzi, jambo linaloashiria mwelekeo chanya wa ushiriki wa wanawake katika siasa.
Kwa TAMWA, hatua hizi ni mafanikio makubwa kwa sababu ajenda yetu kuu ni kuona wanawake wanashika nafasi za juu za uongozi na maamuzi, ili kuleta mabadiliko yenye kuzingatia usawa wa kijinsia.
Ripoti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) inaonyesha kuwa, hadi kufikia Februari 2024, wanawake walishikilia asilimia 37.4 ya viti vya Bunge nchini Tanzania, ikiwa ni jumla ya wabunge 148 kati ya 392 ambapo uwakilishi mkubwa unatokana na viti maalum.
Idadi ya wanawake katika nafasi za uwaziri inatofautiana, ambapo ripoti ya NBS Aprili 2024 na Julai 2024 zinaonyesha kuwa kulikuwa na mawaziri saba na kwamba asilimia 37.5 ya mawaziri ni wanawake, mtawalia.
Licha ya mafanikio haya makubwa lakini bado tunaamini wapo wanawake wanaozuiwa kushiriki nafasi za uongozi kutokana na mfumo dume, wapo wanawake wanaodhalilishwa mitandaoni kutokana na nafasi zao za uongozi.
Hivyo basi tunapoendelea kupata mafanikio haya, bado juhudi za dhati zinahitajika kuhakikisha wanawake wanasiasa wanafanya siasa kwa usalama kama wanaume katika mchakato wa uchaguzi ikiwa ni pamoja kupiga kura, kuchagua na wanaotaka kutia nia kwenye uongozi hawabaguliwi kutokana na jinsia zao.
Tunaamini kwa dhati kwamba uwepo wa wanawake katika ngazi za juu za uongozi ni muhimu kwa maendeleo ya taifa kwa sababu wanawake huleta mtazamo wa kipekee katika uongozi, husimamia kwa uwajibikaji zaidi, na mara nyingi hulinda maslahi ya makundi yote ya jamii, hususan watoto, vijana na wanawake wenzao.
“Kukosekana kwa wanawake katika ngazi za juu za uongozi kunadhoofisha utekelezaji wa sheria na sera zinazolenga kulinda haki za wanawake na watoto. Uwepo wao utahakikisha uimarishaji wa sheria za kuzuia ukatili wa kijinsia, ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, ukeketaji, ubakaji, ulawiti pamoja na udhalilishaji wa kijinsia unaoenea kupitia mitandao ya kijamii.”
Kwa msingi huo, TAMWA inaendelea kusisitiza kuwa ni wajibu wa jamii nzima, vyama vya siasa, serikali na wadau wa maendeleo kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi sawa ya kushiriki kwenye siasa na kushika nafasi za uongozi, ili kujenga taifa lenye usawa, amani na maendeleo endelevu.
Kadhalika wakati tayari kampeni zikiwa zimeanza, TAMWA tunahimiza siasa safi, jumuishi, zenye staha zinazolenga kujenga ustawi, utu wa jamii nzima badala ya kampeni zenye matusi, dhalili na kebehi.
Mkurugenzi Mtendaji
Dkt Rose Reuben
TAMWA
TERMS OF REFERENCE (ToR)
Consultancy to develop gender mainstreaming methodology guidelinesfor the Tanzanian Media Sector.
1. Background
Tanzania Media Women’s Association (TAMWA) has played a pivotal role in promoting gender equality and mainstreaming within the media landscape of Tanzania. From 2020 to 2023, TAMWA supported four media housesZanzibar Broadcasting Corporation (ZBC), Zanzibar Leo, Afya FM, and Dodoma Media Group (DMG)to strengthen gender-responsive practices, including the development and implementation of gender policies, documentation of sexual harassment cases, and establishment of functional gender desks.
In 2025, TAMWA conducted a follow-up with these media houses to evaluate the progress of the earlier interventions and assess the sustainability of gender mainstreaming efforts. Moreover, TAMWA engaged nine media houses out of the previous one for purpose of making comparison analysis of the state in terms of those supported and those have not been in the project to explore emerging and innovative best practices.
Building on the lessons learned, TAMWA now plans to refine and document its gender mainstreaming methodology,mapping best practices from various media houses and developingcomprehensive, context-specific guidelines to support media houses across Tanzania to adopt transformative and sustainable gender mainstreaming practices.These guidelineswill be shared and discussed with other media stakeholdersfor their validation and buy-in.
2. Purpose of the Assignment
The purpose of this consultancy is to review, refine, and document a gender mainstreaming methodology guideline document based on evidence gathered from past interventions, follow-up assessments, and comparison between TAMWA supported and othernon-supported media houses. The guideline should be practical, adaptable, and tailored to the Tanzanian media context.It is intended to address both internal operations and content creation within media houses, promoting equal representation and challenging harmful gender stereotypes.
3. Specific Objectives
4. Scope of Work
Under the overall guidance of TAMWA, the consultant will:
5.Key Deliverables and Duration – Summary
The consultancy will run over a period of four weeks and will produce the following key deliverables: an inception report outlining the methodology, tools, and workplan; a desk review summary and assessment tools with accompanying analysis; a dialogue session report; a draft gender mainstreaming methodology guideline; and a final, revised, and validated guideline.
6. Consultant Profile and Qualifications
7. Application Process
Interested individual consultants should submit the following:
Applications should be submitted no later than 07 September2025 to This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.with the subject line: Consultancy – Gender Mainstreaming Methodology Guideline.
Dar es Salaam. Wajasiriamali wadogo wa mbogamboga, wamepewa elimu ya ujasiriamali na kukumbushwa kuepuka mikopo ‘hatarishi’ badala yake wakope kwa malengo.
Akizungumza na katika warsha ya wajasiriamali wanawake wa mbogamboga jijini Dar es Salaam, Meneja wa Elimu na Usimamizi, wa CRDB Foundation Joshua Mwakalobo amesema, wajasiriamali wengi wanakopa bila malengo na kuishi kwenye mikopo inayowasababishia madhara lukuki.
“Leo tunamzungumzia mama mboga mboga, ambaye akienda kukopa anakosa, sababu zinazochagiza kukosa mkopo ni kukosa dhamana. CRDB Foundation, iliamua kumsaidia mjasiriamali mdogo bila kujali vigezo vya msingi. Kwa hiyo wewe mjasiriamali, hauna TIN namba, hauna leseni unaweza kushikwa mkono na kupata mkopo” amesema Mwakalobo,
Mwakalobo ameyasema hayo wakati wa warsha ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, iliyoandaliwa na Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA) kwa kushirikiana na Benkiy a CRDB Foundation, ikilenga kumtambau mjasiriamali mwanamke wa mbogamboga.
Mwakalobo amesema, kabla ya kuchukua mkopo kuna mambo makubwa muhimu ya kujiuliza kabla ya kuchukua mkopo. Kwanza,Kwa nini ninakopa.
“Cha muhimu tunakopa kwa sababu ya kuongeza mtaji kwenye biashara na si kukopa kwa sababu mkopo una riba ndogo. Tunazungumzia uhitaji wa wewe kukopa,” amesema Mwakalobo
Kwa mujibu wa Mwakalobo kwa asilimia kubwa wanaume ndio wanaomiliki ardhi na hivyo asilimia kubwa ya wanawake wanakosa dhamana ya mikopo yao.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa TAMWA, Dr Rose Reuben alisemaTAMWA kwa kushirikiana CRDB Bank Foundation inatambua na kuthamini mchango wa mwanamke mjasiriamali mdogo wa mboga mboga ambaye amekuwa akifanya juhudi za kujikwamua kiuchumi kwa biashara hiyo.
TAMWA na CRDB tunatambua kuwa wajasiriamali wadogo wapo wa aina nyingi, lakini leo katika kuadhimisha mwezi huu wa wanawake, tunafuraha kuwatambua wajasiriamali wanawake wa mboga na matunda kwa kuonesha uthubutu katika kujikwamua kiuchumi.
TAMWA katika tamko imeeleza kuwa kumtambua mwanamke mjasiriamali wa mboga, kunalenga kuibua fursa, changamoto na kuleta suluhisho zitakazowezesha kuwainua wanawake kiuchumi, huku tukiendelea kupigania haki zao na kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.
March 27,2015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
MKUTANO MKUU WA TAMWA 2014 JUMAMOSI
Zaidi ya Wanachama 100 wa Chama cha Wanahabari Wanawake nchini- TAMWA Jumamosi tarehe 28th Machi, 2015 wanafanya Mkutano wake Mkuu wa mwaka 2014 ambapo pamoja na mambo mengine wanachama watapata fursa ya kutathmini kazi zilizofanyika mwaka 2014, na utekelezaji wa mpango mkakati wa 2015-2021. Mkutano huo utaanza saa 2:00 asubuhi katika ofisi za chama zilizoko Sinza Mori, Dar es Salaam.
Mkutano huo utakaoanza na mafunzo Ijumaa tarehe 27th Machi mwaka huu utawapa fursa wanachama kujadili mafanikio yaliyopatikana kwenye mpango mkakati wa miaka mitano iliyopita (2009 -2014) pamoja na changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji ambapo pia watamchagua Mwenyekiti mpya baada ya aliyekuwepo kumaliza muda wake.
Aidha Siku ya Jumamosi baada ya mkutano huo wanachama watajumuika pamoja katika hafla ya kuchangia mfuko wa shughuli za TAMWA (Gala Dinner) ambazo ni pamoja na kupiga vita vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto itakayofanyika jioni katika hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam.
Mkutano mkuu wa TAMWA ndicho chombo cha juu chenye mamlaka ya kurekebisha katiba yake, kuingiza wanachama wapya, kuchagua viongozi, kupitisha ripoti za mwaka na kutoa maamuzi kuhusu mipango na mikakati ya chama kuhusu utetezi.
Valerie N. Msoka
Mkurugenzi Mtendaji
PRESS RELEASE
TAMWA ANNUAL GENERAL MEETING 2014.
Over 100 TAMWA members will on Saturday, 28th March, 2015 sit for Annual General Meeting (AGM) and among other things get an opportunity to evaluate the 2014 performance and the implementation of the 2015-2021 strategic plan. The meeting will begin at 8.00am at its offices Sinza Mori, Dar es Salaam.
The AGM which will begin with a seminar on Friday, 27th March this year shall give members an opportunity to discuss the progress made in the last five years of strategic plan (2009-2014) and the challenges occurred during the implementation and chart the way forward for betterment of the association. They will also elect the new chairperson for the organisation as the current chairperson’s term has ended as per TAMWA’s constitution.
Furthermore on Saturday after their AGM, members shall converge together in the Fundraising for the TAMWA activities (Gala Dinner) that includes the fight against all acts of Violence Against Women and Children which will be held in the evening at Serena Hotel, Dar es Salaam.
The AGM is the supreme organ of TAMWA which among other things, amend its constitution, admits new members, appoint new leaders, approves the Annual and Financial Audited reports of the previous work and also make decisions about programs and strategies on advocacy.
Valerie N. Msoka
Executive Director
March 20,2015
TAMWA KUKUTANA NA WAHARIRI KUJADILI UKATILI UNAOSABABISHWA NA ULEVI WA POMBE KUPINDUKIA
Na Mwandishi wetu.
Chama cha Wanahabari Wanawake nchini- TAMWA leo tarehe 20 Machi, 2015 saa 3:00 asubuhi kinakutana na Wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali kujadili mikakati kwa kutumia vyombo vya habari ili kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyosababishwa na unywaji pombe kupindukia.
Mkutano huo wa TAMWA na Wahariri utajadili njia zitakazotumika kwa jamii ili kuweka uelewa wa madhara ya unywaji pombe kupindukia kwani unachangia ongezeko la vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto na kurudisha maendeleo nyuma.
Akizungumza; Mratibu wa Kituo cha Usuluhishi – CRC kilichoko ndani ya TAMWA Bi. Gladness Munuo amesema kwa mwaka mzima wa 2014, kilipokea kesi 107 za vitendo vya ukatili wa kijinsia vilivyosababishwa na ulevi wa pombe kupindukia ambapo kati ya hizo wanawake walikuwa 80, wanaume 22 na watoto walikuwa ni watano.
Aidha katika mkutano huo; Wahariri watajadili mbinu jinsi ya kukuza uelewa wa jamii juu ya madhara ya unywaji pombe kutokana na kuwa baadhi ya wanaume wamekuwa wakitelekeza familia zao na kuacha wanawake wakihangaika na watoto.
Akizungumza na mwandishi wetu, Bi. Munuo alisema vyombo vya Habari vikitumika katika kutoa elimu ya madhara ya unywaji pombe hasa kwa ukatili ambao umekuwa ukifanywa kimya kimya vinaweza kuleta mabadiliko makubwa ya kimaendeleo ndani ya jamii
Bi Munuo aliutaja ukatili unaofanywa kimya kimya kuwa ni wa kingono, ubakaji na vipigo ambao unafanyika ndani ya familia huku idadi ya wanawake na watoto kutelekezwa ikiendelea kuongezeka.
Aidha baadhi ya wanandoa wamekuwa wakitumia kilevi kupindukia na kusababisha wengine kushindwa kuwahudumia watoto wao ki - afya, kukosa chakula na mahitaji mengine kama ada za shule hali ambayo husababisha taifa kupoteza nguvu kazi. Mkutano huo ni mwendelezo wa mikakati ya kupinga vitendo vya ukatili unaosababishwa na nywaji pombe kupindukia katika kukuza uelewa wa jamii ili kuwezesha kutoa taarifa za matukio hayo pamoja na madhara ya kiafya na maendeleo kupitia Habari, vipindi vya redio na televisheni.
February 24,2015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UBALOZI WA KANADA KUMTUNUKU MKURUGENZI MTENDAJI WA TAMWA KUWA BALOZI WA KUPINGA NDOA ZA UTOTONI
Ubalozi wa Canada nchini Tanzania kwa mara ya kwanza utamkabidhi Muurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA), Valerie Msoka kuwa balozi wa kampeni ya kupinga ndoa za utotoni (CEFM).
Kwa mujibu wa Ubalozi huo, tukio hilo litafanyika leo, Februari 24, 2015 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam kuanzia saa 8 mchana. Hafla hiyo itahudhuriwa, miongoni mwa watu wengine, na Katibu Mkuu Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Anna Maembe, Balozi wa Canada nchini Tanzania, Alexandre Lévêque, Msaidizi wa Balozi wa Canada anayehusika na masuala ya kisiasa, Eric Bertram, na wawakilishi wa Umoja wa Mataifa na vyombo vya habari.
CEFM inatambua mchango uliotolewa na mtu ambaye ametumia jitihada na muda wake mwingi katika kutetea haki za watoto na ambaye amekuwa akiunga mkono harakati za kuhakikisha taifa letu linakua mahali salama kwa watoto hasa watoto wa kike katika kizazi cha sasa na kijacho.
Kutokana na uzoefu wake wa kupigania haki za biandamu hasa haki za wanawake na watoto, Valerie, ameifanya TAMWA kuwa jina la kukumbukwa katika kuleta usawa na haki za wanawake na watoto. Majukumu yake ya hivi karibuni ni pamoja na:
Mbunge katika Bunge Maalum la Katiba: Alifikisha masuala ya ndoa za utotoni nchini Tanzania katika bunge hilo na haja ya kuingiza umri wa motto unaotambulika kisheria katika katiba. Hii ilisababisha kamati za Bunge hilo kupendekeza umri wa motto kikatiba kuanzia 0 hadi miaka 18.
Mjumbe wa Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalum la Katiba: Aliweza kutetea masuala ya usawa ndani ya kamati ikiwa ni pamoja na haki ya kumlinda mtoto wa kike na wanawake dhidi yya mila potofu ikiwa ni pamoja na ndoa za utotoni, ukeketaji, haki ya kumiliki ardhi na uongozi.
Mjumbe wa Mtandao wa Kupinga Ndoa za Utotoni Tanzania (TECMN): Aliwezesha kuundwa kwa ukanda huru wa kukomesha ndoa za utotoni nchini Tanzania (Agosti 2014) kwa kuwa mwezeshaji wa tukio hilo jijini Dar es salaam mbele ya rais wa zamani wa Tanzania Benjamin Mkapa, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, mgeni rasmi Graca Machel, wakuu wa Balozi mbalimbali nchini na mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Kutambuliwa kwake kuwa Balozi wa Kampeni ya Kupinga Ndoa za Utotoni, kutaleta hamasa zaidi na kumfanya kuongeza jitihada, nguvu na kutoa muda wake zaidi katika kutetea haki za watoto nchini Tanzania.
Valerie N. Msoka
Mkurugenzi Mtendaji
February 22,2015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI
Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania-TAMWA kwa kushirikian na Shirika linalo hudumia Idadi ya Watu UNFPA Kinatoa mafunzo ya siku tatu kuhusiana na kuandika habari za uchunguzi wa unyanyasaji wa kijinsia.Mafunzo hayo yatatolewa kwa waandishi wa habari mapema tarehe 23 hadi Tarehe 25 Februari mwaka huu katika kanda tatu nchini Tanzania.
Mafunzo katika kanda ya Kaskazini yatajumuisha mikoa ya Arusha, Manyara Tanga na Kilimanjaro na yatafanyika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro. Katika Kanda ya Kati, waandishi wa habari watatoka mikoa ya Dodoma, Morogoro, Singida na Tabora ambapo mafunzo yatafanyika mjini Singida. Mafunzo katika Nyanda za Juu Kusini yatajumuisha mikoa ya Iringa, Mbeya, Njombe na Ruvuma na yatafanyika mjini Iringa.
Miongoni mwa vitendo vya ukatili wa kijinsia ni pamoja na ubakaji,wanawake kurithiwa, watoto wa kike kulazimishwa kuolewa na ukeketaji kwa wawanamke na watoto.
Aidha TAMWA kupitia mradi yake imeweza Kujenga na Kuimarisha Usawa na Kutokomeza Ukatili wa Kijinsia kwa kutumia vyombo vya habari nchini. Imekuwa ikielimisha jamii namna ya kutambua ukatili wa kijinsia na madhara yake na kuitaka serikali na vyombo vya sheria kuweka mikakati itakayowezesha kuutokomeza.
TAMWA imesisitiza kuwa kama jamii na serikali hawatashirikiana kikamilifu kushughulikia vitendo vya ukatili wa kijinsia, itakuwa ni vigumu kutokomeza vitendo hivyo.
TAMWA inaamini kuwa endapo jamii itatoa taarifa mapema dhidi ya vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto pale vinapotokea, ingesaidia kuhakikisha vinashughulikiwa ipasavyo na hivyo kupungua kwa haraka na hatimaye kutokomezwa kabisa.
Valerie N. Msoka
Mkurugenzi Mtendaji
February 06,2015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAMWA KUAZIMISHA SIKU YA UKEKETAJI MKOANI SINGIDA LEO
Chama cha Wanahabari Wanawake nchini – TAMWA kinaungana na mashirika mengine yanayopinga vitendo vya ukatili wa kijinsia na kutetea haki za binadamu leo tarehe 6 mwezi wa pili, 2015 saa 2:00 asubuhi kuadhimisha siku ya Kitaifa ya kupinga ukeketaji duniani ambayo mwaka huu kilele kitafanyika mkoani Singida.
Maadhimisho hayo yatakayofanyika katika ukumbi wa Katala Beach Hotel (KBH) mjini Singida yanahusisha mikoa yote iliyoathirika na ukeketaji ili kuunganisha nguvu za wabunge, wakuu wa mikoa, polisi, mahakimu, viongozi wa dini, mashirika yasiyo ya kiserikali, mashirika ya Umoja wa Mataifa, mashirkia ya kimaendeleo, wahanga wa vitendo hivyo, wanafunzi, walimu, wazee wa mila pamoja na ng’ariba ili kuweka mikakati ya kuondoa ukatili huo kutoka asilimia 15 hadi sifuri.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ni Mh. Sophia Simba huku kauli mbiu ikiwa ni “Piga vita ukeketaji” maadhimisho yanafanyika katika kipindi ambacho wanawake na wasichana zaidi ya 1,500 nchini hukeketwa kila msimu, hivyo yatajenga nguvu ya pamoja ili kuhakikisha vitendo hivyo vinapungua kama siyo kuisha kabisa.
TAMWA inaamini kuwa ukeketaji unaweza kuisha endapo jamii itapatiwa elimu ya kuondokana na mila kandamizi kwani zinakiuka haki za binadamu na kudhoofisha afya za wasichana na wanawake, kutokwa damu nyingi kwa wanaokeketwa na hadi kusababisha kifo, madhara ambayo hurudisha nyuma juhudi za kimaendeleo ya familia na taifa kwa ujumla.
Aidha TAMWA kwa ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), shirika ambalo limekuwa mstari wa mbele katika kutetea haki za watoto wa kike, imekuwa ikipinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto ukiwemo ukeketaji kwa kuelimisha jamii ili iondokane na mila hizo hasa katika mikoa ya Mara, Manyara, Dodoma, Singida, Arusha, Morogoro, Kilimanjaro na Tanga.
Valerie Msoka
Murugenzi Mtendaji
December 10, 2014
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UTAFITI WA UNYANYASAJI KWA MAENDELEO YA MWANAMKE NA TAIFA
Chama cha Wanahabari Wanawake nchini-TAMWA kikishirikiana na mashirika mengine manne ya kutetetea haki za wanawake na watoto , leo kinazindua ripoti ya utafiti kuhusu uelewa wa jamii juu ya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto katika ofisi zake za Sinza Mori, Dar es Salaam saa 3 asubuhi.
Ripoti ya Utafiti huo uliofanyika katika wilaya 10 zikiwemo 3 za visiwani ambazo ni (Pemba Kaskazini), Magharibi (Unguja Mjini Magharibi), Unguja Kusini na 7 za Tanzania Bara ambazo ni pamoja na Kisarawe (Pwani), Newala (Mtwara ), Mvomero (Morogoro), Lindi vijijini, Ruangwa (Mtwara), Kinondoni na Ilala, Dar es Salaam itatoa matokeo baada ya kumalizika kwa mradi huo unaojulikana kama (GEWE II)
Aidha kutokana na Utafiti mkubwa wa Hali ya Afya Tanzania (Demographic Health Survey) uliofanyika mwaka 2010 umeonyesha kuwa, vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake wenye umri kati ya miaka 15-49 umeongezeka kutoka asilimia 33% miaka ya nyuma hadi kufikia asilimia asilimia 44% mwaka 2010.
TAMWA inaamini kuwa utafiti huu uliofadhiliwa na Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania utasaidia kuendelea kufichua hali halisi ya vitendo vya unyanyasaji kwa wanawake na watoto vikiwemo, ukeketaji, ubakaji, vipigo kwa wanawake, mimba katika umri mdogo na vingine kama hivyo ambavyo vimekuwa vikimkwamisha mwanamke katika kuboresha maendeleo yake ya kijamii na kiuchumi.
TAMWA, katika utafiti huu imeshirikiana mashirika ya Mtandao wa Kijinsia Tanzania-TGNP, Chama cha Wanasheria Wanawake-TAWLA, Jumuiya ya WanawakeWanasheria Zanzibar (ZAFELA), na Kituo Cha Usuhishi-CRC ambayo pia yalishirikiana katika kutekeleza mradi huo.
Valerie N. Msoka
Mkurugenzi Mtendaji
PRESS RELEASE
GENDER BASED VIOLENCE SURVEY ON WOMEN AND NATIONAL DEVELOPMENT.
Tanzania Media Women Association (TAMWA) in collaboration with other four organizations that advocate for the rights of women and children, will today 10th December, 2014 launch a survey report on the community’s awareness of Gender Based Violence as perpetrated against children and women. The launch will take place at TAMWA’s office, Sinza Mori, Dar es Salaam.
The report was conducted in 10 districts among which include 3 in Zanzibar (Pemba North, Unguja West and Unguja South) and 7 from Mainland Tanzania namely Kisarawe (Cost), Newala (Mtwara ), Mvomero (Morogoro), Lindi Urban, Ruangwa (Mtwara), Kinondoni and Ilala (Dar es Salaam ). The findings of the study come following the completion of GEWE II Project.
In addition, according to the 2010 Demographic Health Survey, incidents of Gender Based Violence increased from 33% previously to 44% in 2010 among women of the age between 15 and 49. As a follow up on the existed situation and interventions made through GEWE II project which was therefore relevant and appropriate.
TAMWA believes that the Survey will contribute to the establishment of the context of Gender Based Violence against women and children in the country. The incidents of GBV in the society include Female Genital Mutilation (FGM), rape, beating, early pregnancy among others which hinder women social and economic development.
The survey was conducted by TAMWA in collaboration with other organizations including TGNP Mtandao, Tanzania Women Lawyers Association (TAWLA), Zanzibar Female Lawyers Association (ZAFELA), Crisis Resolving Center (CRC) which have all been implementing GEWE II project which is supported by Danish Embassy in Tanzania.
Valerie N. Msoka
Executive Director
December 01,2014
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
SIKU YA UKIMWI DUNIANI IADHIMISHWE KWA KUPINGA UKATILI KIJINSIA
Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania-TAMWA kinaungana na watanzania wote kuadhimisha siku ya Ukimwi Duniani ambayo hufanyika tarehe 1 Desemba kila mwaka, kikiitaka jamii kuvichukulia hatua vitendo vya unyanyasaji kijinsia ambavyo huchangia ongezeka la maambukizi ya Virusi Vinavyosababisha UKIMWI (VVU).
Miongoni mwa ukatili unaochangia ongezeko la VVU ni pamoja na ubakaji, wanawake kurithiwa, watoto wa kike kulazimishwa kuolewa na ukeketaji vitendo ambavyo hufanyika kwa wawanamke na watoto kwa kulazimishwa bila kujali hiari ya mtu husika.
Tafiti zinasema kuwa 5.1% ya Watanzania wenye umri kati ya miaka 15-49 wanaishi na VVU. Maambukizi ya VVU ni makubwa na kati ya hao wanawake ni 6.2% na wanaume ni 3.8% katika Tanzania Bara, kiwango cha maambukizi ya VVU ni miongoni mwa wanawake na wanaume wenye umri kati ya miaka 15-49 ambapo yamepungua kutoka 7.0% mwaka 2003-04 na 5.3% katika mwaka 2011-12.
TAMWA imesisitiza kuwa kama jamii na serikali havitashirikiana kikamilifu kushughulikia vitendo vya ukatili kijinsia kisheria, kauli mbiu ya mwaka huu ya “Tanzania Bila Maambukizi Mpya ya VVU, Vifo Vitokanavyo na UKIMWI na Ubaguzi na Unyanyapaa Inawezekana” haitaweza kufanikiwa.
Aidha TAMWA kupitia mradi wake wa Kujenga na Kuimarisha Usawa na Kutokomeza Ukatili wa Kijinsia (GEWE II) kwa kutumia vyombo vya habari nchini kimekuwa kikielimisha jamii namna ya kutambua ukatili wa kijinsia na madhara yake na kuitaka serikali na vyombo vya sheria kuweka mikakati itakayowezesha kuutokomeza.
TAMWA inaamini kuwa endapo jamii itavitolea taarifa mapema vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto pale vinapotokea na kuhakikisha vikavishughulikiwa ipasavyo, maambukizi ya UKIMWI yanaweza kupungua kwa haraka.
Valerie N. Msoka
Mkurugenzi Mtendaji
PRESS RELEASE
LETS COMMEMORATE WOLRD AIDS DAY WHILE FIGHTING GENDER BASED VIOLENCE
Tanzania Media Women Organization (TAMWA) joins Tanzanians to commemorate World AIDS Day which is annually commemorated on 1st December where as it calls on members of the community to take collective initiative against gender based violence acts which contribute to spread of HIV/AIDS.
Among the acts which contribute to spread of HIV include rape, inheriting women, forced marriage, Female Genital Mutilation among others. Most of people subjected to such acts are women, girls and children.
According to the third Tanzania HIV and Malaria Indicator Survey 2011 – 2012 (THMIS III), overall, 5.1% of Tanzanians age 15-49 are HIV-positive. HIV prevalence is higher among women (6.2%) than among men (3.8%). In Mainland Tanzania, HIV prevalence among women and men age 15-49 has decreased from 7.0% in the 2003-04 to 5.3% in the 2011-12.
TAMWA believes that if the government and people in the society are not cooperative to each other in the fight against GBV this year’s theme “Tanzania without new HIV infections, Deaths caused by HIV/AIDS, Discrimination and Stigma is possible” cannot be realized.
However, TAMWA’s Anti Gender Based Violence (GBV) programme of Building and Strengthening Gender Equality and Eradication of Violence against Women and Children (GEWE II) through the media has been providing education on the awareness of gender based violence acts and their effects calling on the government and legal organs to put in place strategies that would alleviate such acts.
TAMWA believes that if incidents of Gender Base Violence on women and children are timely reported and legal action taken against perpetrators spread of HIV will be equally reduced.
Valerie N. Msoka
Executive Director