Gallery

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na taasisi nyingine nchini kulaani vikali matukio ya mauaji ya wanawake na watoto yaliyotokea hivi karibuni hapa nchini.

Kwa kadri siku zinavyoendelea mauaji ya wanawake na watoto yanayotokana na sababu mbalimbali yameripotiwa kutokea sehemu mbalimbali hasa katika maeneo ya Njombe, Rombo, Mto wa Mbu na Simiyu. 

Pamoja na matukio ya mauaji ya watoto Njombe na Simiyu, hivi karibuni  kumetokea mauaji ya wanawake Arusha na mikoa mingine.

TAMWA tunasikitishwa na mauaji hayo na tunaikumbusha jamii kuwa kila mtu anayo haki ya kuishi kulingana na sheria na taratibu za nchi yetu. 

Hivyo tukiwa wadau wanaosimamia haki za wanawake na watoto tunakemea haya na kuwataka wadau wengine kuanzia ngazi ya familia hadi serikalini kuwalinda watoto na kuhakikisha kuwa migogoro ya kifamilia inamalizwa kwa mazungumzo ya amani. 

Tumeona na tunapongeza juhudi kubwa zilizofanywa na vyombo vya usalama nchini lakini pamoja na juhudi hizo cha kujiuliza ni kuwa kwanini bado matukio haya ya mauaji yameendelea kuripotiwasiku baada ya siku? 

Tunachelea kwamba, matukio haya yasipoundiwa mifumo ya muda mrefu ili kuyakomesha kabisa, basi tutaendelea kupoteza kinamama na watoto ambao kimsingi ni nguvu kazi ya Taifa.

TAMWA tunapendekeza uwepo wa mfumo endelevu utakaohusisha wadau mbalimbali wakiwemo wananchi, vyombo vya usalama na kampuni za simu kuwezesha waathirika kutoa taarifa za dalili zozote za ukatili kabla haujatokea. 

TAMWA tunaungana na familia za waathirika wa matukio haya tukiwatakia faraja katika kipindi hiki kigumu. 

 

Rose Reuben

Mkurugenzi Mtendaji

TAMWA

 

User Rating: 2 / 5

Star ActiveStar ActiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake nchini – TAMWA leo, kinaungana na mashirika yote nchini yanayotetea haki za binadamu hasa wanawake na watoto ulimwenguni kusherekea siku ya wanawake duniani ambayo huadhimishwa tarehe 8 mwezi Machi kila mwaka.

 Maadhimisho haya yanabeba kauli mbiu ya kitaifa inayosema  “Wakati ni sasa: Wanaharakati Mijini na Vijijini kubadilisha maisha ya wanawake”, ambayo inatutaka wote tushirikiane kikamilifu kubadilisha maisha ya wanawake kwa kuondokana na ukatili wa kijinsia ili kupanua wigo wa fursa za usawa kiuchumi kwa wanawake.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

CHAMA CHA WANAHABARI WANAWAKE TANZANIA TAMWA  kinawatangazia  wanachama  wake  kuwa  kutakuwa  na  Mkutano  Mkuu  wa  Wanachama (AGM)   utakaofanyika  Juni 13-14, 2025.

LENGO LA MKUTANO MKUU WA AGM NI:

• Uchaguzi wa wanachama  wapya  kwamujibu   wa Katiba ya Chama.
• Tathmini ya  mwenendowa chama – mafanikio, changamoto, namwelekeompya.
• Uwasilishajiwa  taarifa  ya  mapato  namatumizi  ya chama.
• Uwasilishaji  wa  taarifa za   utekelezaji  wamiradi  namustakabali  wa TAMWA.
• Fursaya   wanachamakutoa  maoni  namapendekezo  ya  kuimarisha  mchangowa TAMWA katikajamii.

Mkutano huu utafanyika tarehe 13-14 Juni, 2025

• Eneo: Ukumbi wa TAMWA, Sinza, Mori, Dar es Salaam
• Moduli: Kwa kufika ofisi za TAMWA na kwa njia ya Zoom 
• Muda: Saa 4 asubuhi

Wanachama  wote  mnahimizwa  kuhudhuria

Kwa maelezo  zaidi, tafadhaliwasiliananaTAMWA kupitia;

Barua pepeThis email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. Simu:0716622200

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Tarehe 16 Julai, 2018,Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani   (UNFPA),lina Ujumbe Kutoka Jumuia ya Umoja Ulaya (EU) kwa Tanzania Jumuiya ya Afrika mashariki (EAC), Ubalozi wa Uingereza, Ubalozi wa  Ireland, Ubalozi wa Uholanzi, pamoja na ubalozi wa Kanada kwa pamoja watakuwa wenyeji wa shughuli ya kuonesha juhudi zinazohitajika katika kukomesha suala la ukeketaji hapa nchini.  Katika tukio hilo Kutakuwa na hotuba kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, wazee na Watoto. Pia kutakuwa  na Hotuba ya mwakilishi wa Jeshi la polisi Tanzania na wanaharakati wa haki za binaadamu pia kutakuwa na uzinduzi wa filamu mpya   yenye hadi ya kimataifa inayoitwa “In the Name of Your Daughter”,. Baadsa ya filamu hiyo kutakuwa na wasaa wa maswali na majibu kutoka kwa washiriki wa tukio hilo.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

July 08,2014

Mariam Hamdani and Valerie Msoka are two veteran TAMWANITES who have this year made their mark in Tanzania’s media literary scene.

In a book titled ‘A history of Zanzibar Media – Traditions and Transitions’ Mariam Hamdani and co-authors Ali Rashid and Fatma S. Amour, chronicle the history of media and mass communication development in Zanzibar from time immemorial to-date.

For more information download it.

Search