News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania – TAMWA, kinampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr John Pombe Magufuli kwa kuguswa na matukio ya ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikiathiri hali ya kijamii na kiuchumi nchini.

Takwimi za shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha Tanzania inapoteza 3.4 ya hali ya uzalishaji (GDP) katika kugharamia masuala yoyote yanayotokana na ajali za barabarani yakiwemo matibabu na madhara mengine kama kupoteza maisha, majeraha makubwa, ulemavu wa kudumu, mali kuharibika pamoja na vifo vya wananchi. 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake –TAMWA, kinaungana na mashirika mengine yanayopinga ukatili wa kijinsia na kutetea haki za binadamu kote nchini kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika ambayo huadhimishwa tarehe 16 Juni kila mwaka.

Maadhimisho hayo ambayo yatafanyika wilayani Ilala Kata ya kivule leo tarehe 14 Juni, 2018 kuanzia saa tatu Asubuhi hadi saa tano katika viwanja vya stendi ya Mbondole, Mgeni rasmi ni Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Sophia Mjema ambapo kauli mbiu mwaka huu ni “Kuelekea Uchumi wa Viwanda, Tusimwache Mtoto Nyuma’’ inamlenga kila mzazi, mlezi, ndugu, jamaa, jirani na rafiki kumpenda mtoto kwa namna yoyote ile, kuhakikisha anatunzwa vizuri na haki zake zinalindwa ipasavyo ili atimize ndoto zake. 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

This is to officially congratulate three TAMWA members who emerged among winners of the Excellence in Journalism Awards (EJAT) for the year 2017! The celebrations which were held at GOLDEN TULIP, Dar- Es- Salaam on 12th May 2018 was coordinated by Media Council of Tanzania (MCT).

JANE SHIRIMA  - AZAM TV - HEALTH CATEGORY.

SALOME KITOMARI - NIPASHE - TOURISM AND CONSERVATION CATEGORY.

TUMAINI MSOWOYA - MWANANCHI - EDUCATION CATEGORY.

Hongera sana!!!

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania - TAMWA, Jumamosi 14/04/2018 kimefanya Mkutano Mkuu wa mwaka 2017 ambapo pamoja na mambo mengine,  wanachama walipata fursa ya kutathmini kazi zilizofanyika mwaka 2017, na utekelezaji wa mpango mkakati wa 2018 - 2019. Mkutano huo ni wa 30 tangu kuanzishwa chma hicho na ndicho chombo cha juu chenye mamlaka ya kurekebisha katiba yake, kuingiza wanachama wapya, kuchagua viongozi, kupitisha ripoti za mwaka na kutoa maamuzi kuhusu mipango na mikakati ya chama kuhusu utetezi.

 

Mwenyekiti wa TAMWA Bi Alakok Mayombo, akizungumza jambo wakati wa mkutano

 

Mwanzilishi wa TAMWA Bi Fatma Alloo, akizungumza na wanachama wakati wa mkutano mkuu

 

Baadhi ya Wanachama wa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mkutano

Latest News and Stories

Search