News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) leo Aprili 5, kwa kushirikiana na Hospitali ya Narayani India wametoa  elimu ya afya pamoja na ushauri wa kitaalamu kwa wanahabari wanawake kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kwa lengo la kuwajengea uwezo juu ya afya ya uzazi na magonjwa na magonjwa ya saratani.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika  jijini Dar es salaam, mwenyekiti wa TAMWA, Bi. Alakok Mayombo alisema washiriki wa mafunzo hayo watajengewa uwezo kuhusu afya ya uzazi pamoja na matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii.

“Katika kipindi cha siku mbili za mkutano mkuu wa chama chetu,  Tulizungumza na marafiki wa TAMWA Narayana hospital ambao walikubali kutoa elimu ya afya uzazi kwa wakina mama kupitia kipengele chao cha awareness kuhusu hasa magonjwa ya kansa" Alisema Bi. Mayombo. 

Alisema kupitia elimu ambayo itatolewa kwa washiriki hao itawawezesha kuwasaidia kujilinda na kupambana  kansa kwa akina mama. 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA Rose Reuben, alisema, mbali na mafunzo hayo ya afya ya uzazi pia watatoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya ya mitandao ya kijamii.

“Ni lazima jamii itambue sheria ya maudhui ya mtandao pamoja na sheria za vyombo vya habari katika mitandao ya kijamii.  Lengo letu ni kujiongezea ujuzi katika maeneo haya, hivyo  watu wa TCRA watakuja kutusaidia kutoa mafunzo kuhusu  matumizi ya mtandao ni”. Alisema Rose.

Nae daktari kutoka Hospitali ya Narayana, Bwana Limbanga Freddie alisema, tafiti zinaonyesha kumekuwepo na ongezeko kubwa la wagonjwa wa kansa kutokana na mabadiliko ya mfumo wa maisha pamoja na kutofanya mazoezi, kutokufanya kazi ngumu na kutumia vyakula ambavyo ni hatari kwa afya.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Wakati dunia ikisherehekea Siku ya Wanawake Duniani, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA)kinakuletea wanahabari wakongwe waanzilishi wa TAMWA. Hiki ndicho wanachokisema katika maadhimisho haya ya Siku ya Wanawake Duniani.

Halima Shariff, yeye ni mtafiti, kiongozi na mwalimu . Ni miongoni mwa waasisi wa TAMWA aliyezaliwa kutoka katika familia ya kawaida kabisa, mkoani Tanga.
 
Akiwa ni mtaalamu na nguli wa habari nchini, Halima amewahi kuandika katika gazeti la Daily News miaka ya 80 na mtangazaji wa  Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani(Deustche Welle).
 
Pamoja na fani ya habari, Halima amewahi  kushika nafasi kubwa katika taasisi za kimataifa  na kwa sasa ni Mkurugenzi wa Mradi wa Uzazi wa Mpango wa Advanced Family Planning Project(AFP).
 
Ni miongoni mwa wanawake waliosimamia kidete maendeleo ya wanawake na watoto katika masuala ya elimu, afya ya uzazi na Virusi vya Ukimwi. 
 
Amewahi kuongoza miradi mikubwa ya afya  ikiwamo ya Shirika la Misaada la watu wa Marekani USAID. Ameshiriki katika kutetea hadi  kufanikisha kupitishwa kwa muswada wa  masuala ya Ukimwi, kuanzishwa kwa sera ya HIV/AIDS katika maeneo ya kazi. Amewahi pia kuwa Kamishna wa Tume ya Ukimwi Tanzania (TACAIDS). 
 
Anachokisema katika kuadhimisha Sharif katika kuadhimisha Siku ya Wanawake duniani: 
 
“Kuimarisha nafasi ya mwanamke katika nyanja zote katika jamii ni harakati endelevu zinazohitaji jitihada za pamoja zenye kasi inayoongezeka kizazi hadi kizazi. Kwa mantiki hiyo Tanzania tumefanikiwa kujenga uelewe wa jamii kuhusu nafasi muhimu ya mwanamke katika kujenga familia na katika maendeleo kwa ujumla” 
 
“Lakini bado hatujawekeza vya kutosha katika kuhakikisha afya ya mwanamke inapewa kipaumbele ukizingatia kwamba bado wastani wa kuzaa wa taifa ni watoto sita kwa mwanamke wa rika la uzazi (15-49). 
 
“Inatia moyo kwamba serikali imekuwa ikielekeza nguvu huko lakini ni eneo linalohitaji kutazamwa zaidi kwani mara nyingi wanawake hukosa fursa za kujiendeleza kutokana na changamoto za uzazi,”

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Wakati dunia ikisherehekea Siku ya Wanawake Duniani, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA) kinakuletea wanahabari wakongwe waanzilishi wa TAMWA. Hiki ndicho wanachokisema katika maadhimisho haya ya Siku ya Wanawake Duniani.

Ummy Mahfoudh.  Ni mwanahabari mkongwe, Mwanachama wa Chama cha Wanahabari  Wanawake tangu 1988. Amewahi kufanya kazi katika taasisi zisizo za kiserikali za kitaifa na kimataifa katika nchi za Uingereza, Denmark, Tunisia na Afrika Kusini.
Ni miongoni mwa walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika mkutano wa kidunia wa haki za mwanamke, maarufu mkutano wa Beijing mwaka 1995. Amewahi kushiriki utafiti wa chanzo cha mauaji ya wanawake wazee kutokana na imani za kishirikina na mauaji ya albino Tanzania. 
 Kwa sasa ni mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya magazeti Zanzibar
Ni mshairi, ana mume na watoto wanne. 
Anachokisema katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Tanzania;
“Katika kuadhimisha Siku ya Mwanamke  Duniani, tukumbushane kushughulika na kizazi cha sasa. Tupo kisasa kiasi cha kusahau sisi tulilelewa vipi. Watoto wa kike wafundishwe masuala chanya ya kimila badala ya kufikiri kila kitu cha kimila ni kibaya,”
“Mimi watoto wangu wote nawalea sawa bila kujali wa kike au wa kiume. Wale wa kiume wote wakifikisha miaka 14 wanajua kukuna nazi, kupika nk” (Ummie Mahfoudh)
 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na taasisi nyingine nchini kulaani vikali matukio ya mauaji ya wanawake na watoto yaliyotokea hivi karibuni hapa nchini.

Kwa kadri siku zinavyoendelea mauaji ya wanawake na watoto yanayotokana na sababu mbalimbali yameripotiwa kutokea sehemu mbalimbali hasa katika maeneo ya Njombe, Rombo, Mto wa Mbu na Simiyu. 

Pamoja na matukio ya mauaji ya watoto Njombe na Simiyu, hivi karibuni  kumetokea mauaji ya wanawake Arusha na mikoa mingine.

TAMWA tunasikitishwa na mauaji hayo na tunaikumbusha jamii kuwa kila mtu anayo haki ya kuishi kulingana na sheria na taratibu za nchi yetu. 

Hivyo tukiwa wadau wanaosimamia haki za wanawake na watoto tunakemea haya na kuwataka wadau wengine kuanzia ngazi ya familia hadi serikalini kuwalinda watoto na kuhakikisha kuwa migogoro ya kifamilia inamalizwa kwa mazungumzo ya amani. 

Tumeona na tunapongeza juhudi kubwa zilizofanywa na vyombo vya usalama nchini lakini pamoja na juhudi hizo cha kujiuliza ni kuwa kwanini bado matukio haya ya mauaji yameendelea kuripotiwasiku baada ya siku? 

Tunachelea kwamba, matukio haya yasipoundiwa mifumo ya muda mrefu ili kuyakomesha kabisa, basi tutaendelea kupoteza kinamama na watoto ambao kimsingi ni nguvu kazi ya Taifa.

TAMWA tunapendekeza uwepo wa mfumo endelevu utakaohusisha wadau mbalimbali wakiwemo wananchi, vyombo vya usalama na kampuni za simu kuwezesha waathirika kutoa taarifa za dalili zozote za ukatili kabla haujatokea. 

TAMWA tunaungana na familia za waathirika wa matukio haya tukiwatakia faraja katika kipindi hiki kigumu. 

 

Rose Reuben

Mkurugenzi Mtendaji

TAMWA

 

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na taasisi nyingine nchini kulaani vikali matukio ya mauaji ya wanawake na watoto yaliyotokea hivi karibuni hapa nchini.

Kwa kadri siku zinavyoendelea mauaji ya wanawake na watoto yanayotokana na sababu mbalimbali yameripotiwa kutokea sehemu mbalimbali hasa katika maeneo ya Njombe, Rombo, Mto wa Mbu na Simiyu. 

Pamoja na matukio ya mauaji ya watoto Njombe na Simiyu, hivi karibuni  kumetokea mauaji ya wanawake Arusha na mikoa mingine.

TAMWA tunasikitishwa na mauaji hayo na tunaikumbusha jamii kuwa kila mtu anayo haki ya kuishi kulingana na sheria na taratibu za nchi yetu. 

Hivyo tukiwa wadau wanaosimamia haki za wanawake na watoto tunakemea haya na kuwataka wadau wengine kuanzia ngazi ya familia hadi serikalini kuwalinda watoto na kuhakikisha kuwa migogoro ya kifamilia inamalizwa kwa mazungumzo ya amani. 

Tumeona na tunapongeza juhudi kubwa zilizofanywa na vyombo vya usalama nchini lakini pamoja na juhudi hizo cha kujiuliza ni kuwa kwanini bado matukio haya ya mauaji yameendelea kuripotiwasiku baada ya siku? 

Tunachelea kwamba, matukio haya yasipoundiwa mifumo ya muda mrefu ili kuyakomesha kabisa, basi tutaendelea kupoteza kinamama na watoto ambao kimsingi ni nguvu kazi ya Taifa.

TAMWA tunapendekeza uwepo wa mfumo endelevu utakaohusisha wadau mbalimbali wakiwemo wananchi, vyombo vya usalama na kampuni za simu kuwezesha waathirika kutoa taarifa za dalili zozote za ukatili kabla haujatokea. 

TAMWA tunaungana na familia za waathirika wa matukio haya tukiwatakia faraja katika kipindi hiki kigumu. 

 

Rose Reuben

Mkurugenzi Mtendaji

TAMWA

 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Mwandishi wetu, Dar es salaam.

Mpiga picha wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Aika Kimaro, ameibuka mshindi wa pili katika shindano la kupiga picha za habari.

Mshindi wa kwanza katika shindano hilo alikuwa mpiga picha wa kujitegemea, Imani Isamula ambaye aliibuka kidedea kwa kura 57 dhidi ya kura 43 alizopata Aika.

Washindi hao walitangazwa juzi jijini Dar es Salaam katika mdahalo katika mdahalo ulioandaliwa na Ubalozi wa Netherland katika mwendelezo wa maonyesho ya picha (World Press Photo 2018) ambayo yanaendelea.

Imani aliibuka kidedea kutokana na picha zake za walemavu wa miguu ambapo mlameavu mmoja ni mwanamke ambaye amekimbiwa na mume wake na kuachiwa watoto ambao anawalea peke yake.

Katika picha nyingine mlemavu wa kiume ambaye licha ya ulemavu wake anaonekana kujishughulisha na shughuli za uvuvi wa samaki.

Kwa upande wa Aika moja kati ya picha zakie mbili zilizoshinda, inamuonyesha mwanamke aliyebeba mzigo wa magunia mawili yaliyofungwa kwa kamba yakiwa na chupa tupu za plastiki huku amebeba mtoto mgongoni anavuka barabara.

Akifafanua kuhusu picha hizo, Aika alisema mama huyo licha ya kuwa na shuguli nyingi nyumbani ambazo hazimuingizii kipato ameamua kumbeba mtoto wake mgongoni na kuamua kuingia mtaani kujitafutia chochote kwa ajili ya watoto wake.

“Katika picha ya pili, hawa ni watoto wanaonekana wakiwa na magunia wanaokota makopo na chupa za maji ili wakauze, picha hii inazungumza mengi, kwanza hawa ni watoto ambao wamekosa haki zao za msingi kama haki ya kusoma na haki ya kucheza,” alisema Aika.

Latest News and Stories

Search