News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Florence Majani, TAMWA.

Ruangwa, Lindi. Ni Januari 17 mwaka 2018, saa sita mchana. Kundi la wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za Nambilanje, wameketi mbele ya walimu wao, wakijadiliana kuhusu mila na desturi zinazokwamisha maendeleo na kuchochea mimba za utotoni katika kata hiyo.

Walimu walikuwa kimya wakifuatilia kwa umakini majadiliano hayo.  Wanafunzi  nao hawakuwa na hofu bali walitoa ya moyoni na kueleza kinagaubaga kinachoendelea majumbani.

Majadiliano hayo yaliandaliwa na Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA)  ili kuangalia mila na desturi zinazochochea mimba za utotoni na ukatili kwa wanawake na watoto.

Wanafunzi hao waliweka bayana kuwa, baadhi ya  wazazi ndicho  chanzo cha wao kufeli kwani huwalazimisha kufeli na kuwataka kuandika ‘madudu’ ili wasiendelee na masomo ya sekondari.

Mwanafunzi wa kidato cha nne, shule ya Sekondari Nambilanje, Zahara Chigope anaweka bayana  kuwa wapo wanafunzi wenzake ambao wanashurutishwa na wazazi waandike ‘madudu’ kwenye mitihani ya taifa ili wasiendelee na masomo ya sekondari.

“Mzazi wake alimwambia aandike 11111 kila swali, ili afeli na asiendelee na sekondari,” alisema.

Alisema hata kwa wale wanaofaulu darasa la saba, wapo wazazi wanaokataa kwa makusudi kuwapeleka shule wakidai hawajalipwa fedha za korosho lakini kimsingi, ni ujanja tu ili wasiendelee na masomo.

Zahara alisema mwenzao mmoja aliyekuwa anafaulu vizuri kwenye masomo wakati wakiwa shule ya msingi, alifeli na alipomdodosa imekuwaje, ndipo alipomtobolea siri hiyo kuwa aliambiwa na mama yake aaandike ‘madudu.’

“Kweli alifeli kwa sababu aliniambia aliandika 11111 katika kila swali na sasa hivi yupo mitaani amezaa na wala hajaolewa,” alisema

Mwanafunzi mwingine wa kidato cha tatu wa shule hiyo, Zena Mitawa anasema mwenzao aliyetakiwa kuwa nao kidato cha tatu, alifeli  darasa la saba kutokana na ushauri wa mama yake.

“Alikuwa anatuambia hata kabla hatujafanya mtihani wa taifa kuwa, mama yake hataki aendelee na shule kwani tayari yupo mwanaume wa kumuoa. Kweli matokeo yalipotoka, hakufaulu na sasa ameolewa huko Lindi mjini,” anasema.

Mwanafunzi mwingine, Nasma Kumkana, alisema suala la wazazi kuwashawishi wanafunzi wafeli kwa makusudi ni kubwa na wanalisikia kutoka kwa wanafunzi wenzao.

“Sio hivyo tu, hata baadhi ya wazazi tunawasikia wanasema bora mtoto afeli kwa sababu hawana hela za kumhudumia atakapoingia sekondari, hata wakiambiwa elimu ni bure watasema hawana fedha za sare za shule,” anasema

Nasma anasema mila hizo zinaambatana na ile ya baadhi ya wazazi kumshauri mtoto atafute mboga kwa jasho lake.

“Hii ina maana kwamba, mama anamwambia mtoto leo zamu yako kutafuta mboga, kwa maana nyingine,  mtoto wa kike anapewa ruhusa ya kuwa na mwanaume ili apate fedha ya kusaidia familia,” anasema.

Akizungumzia suala hilo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nambilanje, Charles Chitawala anasema tatizo hilo ni kubwa kwa kata ya Nambilanje na maeneo mengine ya Ruangwa.

“Sisi kama viongozi suala hilo linatuudhi, inabidi tutoe elimu, ili tabia hizo waziache. Ilifikia mahali ikabidi tuitishe vikao vya wazazi na wazazi wajaze mikataba,” anasema.

Anasema mwaka 2018, wazazi walijaza mikataba na kukubaliana kuwa iwapo mzazi atabainika kuwa alimshauri au kumlazimisha mwanafunzi kufeli kwa namna yoyote ile, basi atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mwalimu Chitawala anasema mikataba hiyo ilitolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na kusainiwa na wazazi wa wanafunzi waliomaliza darasa la saba mwaka jana.

Mratibu wa Elimu kata ya Nambilanje, Lista Mziwanda anasema suala la wazazi kuwalazimisha wanafunzi kuandika  ‘utumbo’ kwenye mitihani ya taifa lipo kwa kiasi kikubwa eneo hilo ingawa hakuna takwimu rasmi.

“Tulizibaini kesi hizo baada ya kuwabana wanafunzi ambao tuliwategemea kufaulu lakini hawakufaulu. Ukikaa na mtoto vizuri anakuambia ukweli kuwa alilazimishwa na mama,” anasema

Anasema kesi hizo ni za wanafunzi ambao walifaulu vizuri kwenye mitihani ya ndani na ile ya kujipima ‘Mock’ lakini mitihani ya taifa walifeli.

“Kinachofanyika sasa ni kutoa elimu lakini na hizo sheria ndogondogo kama kuwasainisha wazazi mikataba kuwa wakibainika kuwalazimisha watoto wafeli, watachukuliwa hatua. Tumeanza suala la mikataba mwaka jana, tutaangalia mwaka huu,”anasema.

Mwalimu Mziwanda anasema kati ya wanafunzi 76 waliomaliza darasa la saba mwaka 2018, 66 walifaulu kwenda Sekondari na wanne wamekwenda Chuo cha ufundi Nkoye. Mwananchi ilibaini kuwa, mazingira ya kielimu wilayani humo ni magumu kwa baadhi ya wanafunzi ambao hulazimika kubaki  peke yao kwa muda mrefu baada ya  wazazi wao kuondoka nyumbani na kwenda kukaa shambani msimu wa kilimo.

 Mwanafunzi wa shule ya msingi Nambilanje Swaumu Ibadi anasema  mazingira ya kielimu kwake  ni magumu kwa sababu mama yake yupo shambani kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.

“Jana usiku sijala, mpaka mchana huu kwa sababu nakaa peke yangu, mama amehamia mashambani na dada yangu niliyeachwa naye, ameondoka,” anasema

Anasema akibahatika kula, basi ni milo miwili tu kwa siku na wakati huo akitembea umbali wa karibu kilometa10 kutoka nyumbani hadi shuleni.

Saumu ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba, anasema hana mahitaji muhimu ya shule kama sare, madaftari na chakula kwa sababu mama yake hajamnunulia.

Kwa mujibu wa Mtendaji wa Kijiji cha Nambilanje, Constatine Odilo, desturi za wazazi kuhamia shambani kipindi cha kilimo zinachangia  kushuka kwa kiwango cha elimu na hata mmomonyoko wa maadili.
“Tunapokea kesi nyingi hapa kijijini za watoto wadogo wa kike kuachwa peke yao nyumbani wakati wazazi wakiwa wamehamia shambani, hili linachangia watoto hawa kuwa huru na hata wasipoenda shule, nani atawajibika?” anasema.

Familia zachangia kushuka kwa elimu, kuvunjika kwa maadili

Pamoja na wazazi kuhujumu elimu ya watoto wao, mambo mengine yanayotajwa kusababisha mimba za utotoni  na kushuka kwa kiwango cha elimu eneo hilo ni wazazi kutengana.

Kwa mfano, Mtendaji wa Kata ya Nambilanje, Abdallah Tamba anasema  kesi nyingi za wazazi kutengana ni nyingi na hali hiyo husababisha watoto kubaki bila malezi.

“Kwa mila za huku, kuachana ni kitu rahisi tu, kama ilivyo kuoa. Kwa hiyo mara nyingi wazazi wanapotengana, watoto ndiyo hupata tabu, wanakosa malezi kabisa,” anasema

Anasema mara nyingi baba anapobaki na watoto, huoa mke mwingine na kama mama huyo hatajali suala la elimu, basi watoto huacha shule.

Lakini watoto wa eneo hilo wanasema wazi kuwa mfumo wa  matrilineal (mama kuwa kichwa cha familia) wa kabila za kusini, ndiyo huchangia changamoto hizo.

Kwa mfano, Nasra Juma, Mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari Nambilanje anasema baadhi ya kinamama ndiyo wanaowaambiwa watoto wao wa kike wasiende shule bali washiriki kuleta mboga nyumbani.

“Sasa mama anamwambia binti yake kuwa leo zamu yako kuleta mboga, hiyo ina maana kuwa anamruhusu kwenda kufanya chochote ili alete mboga nyumbani,” anasema

Mila nyingine zinazotajwa kuchangia kushuka kwa elimu ni unyago ambao hufanyika kipindi cha masomo.

Meneja Ufuatiliaji na Tathmini wa TAMWA, John Ambrose anasema zipo mila na desturi zenye manufaa kwa jamii lakini endapo mila hizo zinachochea mimba, kushuka kwa elimu, zinamzuia mtoto kupata haki yake basi hazina budi kupingwa.

“Ndiyo maana tumeandaa midahalo hii, kwa kushirikiana na Taasisi ya Foundation for Civila Society, ili wanafunzi waeleze wazi yanayowasibu nyumbani, shuleni na katika mazingira yao mengine, tumeshuhudia mengi yanayofanyika kwa watoto na yanachangia ukatili kwao,” anasema Ambrose

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Florence Majani, TAMWA.

Ruangwa. Licha ya serikali kujenga shule za kata kwa wingi ili kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari, wazazi wilayani Ruangwa, wamelalamikiwa kuwajengea watoto wao mazingira ya kufeli mitihani ya darasa la saba ili wasiendelee na shule na waolewe.

Hayo yalibainika wakati wa mdahalo kwa wanafunzi kuhusu mila na desturi zinazochochea mimba za utotoni ulioandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania(TAMWA) wilayani Ruangwa.

Kwa nyakati tofauti wanafunzi hao walisema baadhi ya  wazazi huwalazimisha watoto wao kukataa shule au kuwashauri wajifelishe mitihani ya darasa la saba ili waolewe.

“Kuna mwenzetu mmoja, alikuwa na akili sana lakini matokeo yalipotoka hakufaulu kujiunga na sekondari, tulipomuuliza kulikoni alisema mama yake alimwambia aandike 0000 ili afeli na aolewe,” alisema Zahara Chigope, Mwanafunzi wa Kidato cha nne, Sekondari ya Nambilanje.

Mwanafunzi mwingine, Nasma Kumkana, alisema suala la wazazi kuwashawishi wanafunzi wafeli kwa makusudi ni kubwa na wanalisikia kutoka kwa wanafunzi wenzao.

“Sio hivyo tu, hata baadhi ya wazazi tunawasikia wanasema bora mtoto afeli kwa sababu hawana hela za kumhudumia atakapoingia sekondari, hata wakiambiwa elimu ni bure watasema hawana fedha za sare za shule,” alisema

Nasma alisema mila hizo zinaambatana na ile ya baadhi ya wazazi kumshauri mtoto atafute mboga kwa jasho lake.

“Hii ina maana kwamba, mama anamwambia mtoto leo zamu yako kutafuta mboga, kwa maana nyingine,  mtoto wa kike anapewa ruhusa ya kuwa na mwanaume ili apate fedha ya kusaidia familia,” alisema.

Akizungumzia suala hilo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nambilanje, Charles Chitawala alisema tatizo hilo ni kubwa kwa kata ya Nambilanje na maeneo mengine ya Ruangwa.

“Sisi kama viongozi suala hilo linatuudhi, inabidi tutoe elimu, ili tabia hizo waziache. Ilifikia mahali ikabidi tuitishe vikao vya wazazi na wazazi wajaze mikataba,” alisema.

Alisema mwaka 2018, wazazi walijaza mikataba na kukubaliana kuwa iwapo mzazi atabainika kuwa alimshauri au kumlazimisha mwanafunzi kufeli kwa namna yoyote ile, basi atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mwalimu Chitawala alisema mikataba hiyo ilitolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na kusainiwa na wazazi wa wanafunzi waliomaliza darasa la saba mwaka jana.

Mratibu wa Elimu kata ya Nambilanje, Lista Mziwanda alisema suala la wazazi kuwalazimisha wanafunzi kuandika  ‘utumbo’ kwenye mitihani ya taifa lipo kwa kiasi kikubwa eneo hilo ingawa hakuna takwimu rasmi.

“Tulizibaini kesi hizo baada ya kuwabana wanafunzi ambao tuliwategemea kufaulu lakini hawakufaulu. Ukikaa na mtoto vizuri anakuambia ukweli kuwa alilazimishwa na mama,” alisema

Alisema kesi hizo ni za wanafunzi ambao walifaulu vizuri kwenye mitihani ya ndani na ile ya kujipima ‘Mock’ lakini mitihani ya taifa walifeli.

“Kinachofanyika sasa ni kutoa elimu lakini na hizo sheria ndogondogo kama kuwasainisha wazazi mikataba kuwa wakibainika kuwalazimisha watoto wafeli, watachukuliwa hatua. Tumeanza suala la mikataba mwaka jana, tutaangalia mwaka huu,”alisema.

Mwalimu Mziwanda alisema kati ya wanafunzi 76 waliomaliza darasa la saba mwaka 2018, 66 walifaulu kwenda Sekondari na wanne wamekwenda Chuo cha ufundi Nkoye.

Mmoja wa wazazi, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama ya kata, Esha Chigope, alisema kesi hizo zipo nyingi.

Esha alisema kuna mkazi mwenzao aliyefahamika kama Tendele, alikiri kumshauri mtoto wake aandike 1111, ili afeli mtihani wa darasa la saba.

“Tendele mwenyewe anasema wazi, alitaka mtoto wake afeli kwa sababu hakuna umuhimu kwa mtoto wa kike kusoma, kwa hiyo kweli mtoto akafeli,” alisema Esha.

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Hashim Mgandilu alisema watawachukulia hatua wazazi wanaorubuni wanafunzi wafeli na kusema kuwa hiyo  jamii ya wazazi inayohujumu watoto.

“Ndiyo maana tuliingia mikataba kati ya serikali na mzazi, kwamba hata mtoto akifeli, mzazi awajibike kwa kutoa maelezo kwa nini kijana amefeli,” alisema.

Alisema hali ya mwamko wa elimu kwa ukanda wa kusini hasa vijiji vya Nambilanje, Namichiga, Nachienjele na Nanjaro bado ni ndogo  na inahitajika elimu ya kutosha.

Alisema hata katika ziara zake alizofanya katika vijiji 81 vya Wilaya ya Ruangwa, alibaini suala la unyago ndilo linachochea kufifia kwa elimu wilayani humo.

“Watoto wanatolewa kupelekwa unyago kipindi cha masomo. Nilikamata wazazi waliokaidi agizo langu pamoja na watoto 22 waliokuwa wanachezwa huo unyago,”alisema Mgandilu.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Florence Majani, TAMWA.

Ruangwa, Lindi. Kinamama katika kata ya Likunja, wilayani Ruangwa wamelaumiwa kuwa wao  ndicho chanzo cha kuvunjika kwa ndoa kila kukicha katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo, kasi ya wanandoa kuachana ni kubwa na hata ile ya kuoana nayo ni kubwa hasa msimu wa mavuno.

Hayo yameelezwa jana, wakati wa mafunzo ya wanakamati za ulinzi za kata hiyo, yaliyotolewa na Chama cha Wanahabari Wanawake(TAMWA) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mwalimu wa Shule ya Msingi Likunja, Maria Lilai, alisema ndoa zinavunjika kila siku kwa sababu ya mfumo wa  mwanamke kuwa na madaraka kwenye familia zaidi ya baba.

“Mfumo  wa ‘matrilinneal’ ambao unampa mama madaraka ya kuwa kichwa cha familia, ndiyo unaofanya ndoa nyingi zinavunjika. Kwa sababu wanaume wengi hawapendi kuwa chini ya mwanamke, hivyo  migogoro  mingi inaishia kwenye talaka,” alisema.

Alisema kesi zinazotolewa talaka ni za kila kukicha lakini zipo kesi ambazo wanandoa wanatengana lakini  mwanaume anakataa kutoa talaka.

“Akikataa kutoa talaka inabidi uinunue, wapo wanaume ambao hukataa kutoa talaka hadi uwape hela. Ukiwapa hela wanakupa talaka yako,” alisema.

 

Ofisa Maendeleo ya Jamii kata ya Likunja, Sarah Pongolela alisema kwa mila za Wamwera mwanaume anapooa ni lazima amjengee mke wake nyumba.

“Mara nyingi migogoro hii inaanzia kwenye mgawanyo wa mali, au pale ambapo kipato kinaongezeka,” alisema

 Alisema hakuna takwimu rasmi za matukio ya talaka kwa sababu mengi yanamalizika katika ngazi ya familia.

“Kesi nyingi zinamalizwa baada ya wanandoa kugawana mali, lakini kama kesi hiyo ina mgogoro zaidi, ndipo zinapofikishwa kwenye ofisi za kata au Bakwata au mahakamani,” alisema.

Akizungumzia kesi za talaka, Mwenyekiti wa Chama cha kinamama katika kata hiyo, Shelly Nachinuku,  alisema zipo kesi nyingi za ndoa kuvunjika lakini yeye alikuwa na maoni tofauti na Maria akidai kuwa chanzo ni wanaume.

“Kesi hizo zinaanzia kwa wanaume, mfano mwanaume akishaona amemzalisha mwanamke anamuacha, au akiona kuna watoto wengi ndani ya nyumba anamuacha na anaenda kwa mwanamke mwingine,” alisema

Alisema suala la talaka linachangiwa na wanaume kutokukaa nyumbani na kutotimiza majukumu yao  kwenye familia.

“Wanaume wanapoona msimu wa mavuno, wanazikimbia familia zao na kudai wanakwenda kuangalia mazao kumbe, wanayauza na kuanza kutumia fedha na wanawake wengine,” alisema

 Alisema hata huko shuleni imebainika kuwa wanafunzi wengi wanalelewa na mzazi mmoja au bibi  baada ya wazazi wao kuachana.

Katekisti wa Kanisa Katoliki, kigango cha Likunja, Erick Akwilambo alisema kesi hizo za wanandoa kuachana zipo nyingi katika kata hiyo na kueleza kuwa zinasababishwa na mfumo jike ambapo wanawake wanakuwa  na madaraka makubwa kwenye familia.

“Ndiyo maana hata hizi kesi za wanaume kupigwa ni nyingi, huku wanaume hawana la kusema, hata mtoto akizaliwa anakuwa ni wa ukoo wa kwa mama,” alisema

Ofisa Elimu wa Kata ya Likunja, Mwajuma Ibadi alisema sio talaka tu, bali hata ndoa nazo zinafungwa kwa wingi kama ilivyo talaka. Alisema tatizo kubwa ni kuwa wakazi wa eneo hilo wanafunga ndoa za mashindano.

“Kwa mfano, wanandoa wakiachana, basi kila mmoja atataka aoe au aoelewe tena ili kumkomoa mwenza waliyeachana,”alisema

Ibadi alisema asilimia 70 ya wanafunzi kwenye shule za msingi, wanalelewa na bibi au babu baada ya wazazi kutengana.

Alisema ndiyo maana kuna mmomonyoko wa maadili ikiwamo mimba za utotoni na elimu duni kwa kuwa watoto wengi wanakosa malezi ya wazazi wote wawili.

Mtendaji Kata ya Likunja, Hassan Kalembo alisema kesi hizo za ndoa kuvunjika zipo kwa wingi lakini hana takwimu rasmi.

“Tunapokea malalamiko hayo kila siku, lakini chanzo cha haya yote ni tamaa. Wanawake wa kabila hili(wamwera) wakiona mume amechuma mali kadhaa wanataka kuachana ili wagawane mali,” alisema.

Ofisa Maendeleo wilaya ya Ruangwa, Rashid Namkulala alisema matukio ya wazazi kutengana au kuachana ndiyo yanayosababisha malezi duni kwa watoto.

“Sisi viongozi tutaendelea kutoa elimu ya kina kwa wakazi wa eneo hili ili kesi za talaka zipungue. Tumeshuhudia kuwa watoto wanakosa malezi bora pindi tu wazazi wanapotengana,” alisema

Hata hivyo, Ofisi ya Ustawi wa Jamii ya wilaya ya Ruangwa, walisema hawana takwimu za talaka.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Ofisa Maendeleo Wilaya ya Ruangwa, Rashid Namkulala amekemea vikali Mila na desturi zinazochochea ukatili wa wanawake na watoto wilayani humo. Ameyasema hayo juzi wakati wa mdahalo kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Nambilanje na ya Msingi Nambilanje. Chama Cha Wanahabari Wanawake (TAMWA) kimesimamia mafunzo kwa kamati ya ulinzi na usalama ya Kijiji cha Nambilanje na midahalo na majadiliano kwa shule za Msingi na Sekondari kuhusu Mila na desturi zinazochochea mimba za utotoni wilayani humo.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Godwin Assenga, TAMWA.

In Summary

The Tazania Media Women's Association (TAMWA) has appointed Ms Rose Reuben as the new Executive Director effectively from January 7, 2019. 

The new Director is replacing Ms Edda Sanga, whose term in office has expired after saving the Association for over three years.

The new appointed TAMWA Executive Director, Ms Rose Reuben (Right), receiving office documents from the representative of the Association’s Board Chairperson, 

Ms Judica Losai during the handing over ceremony that took place at TAMWA Office in Dar es Salaam on Friday, January 11, 2019.

Latest News and Stories

Search