News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake nchini – TAMWA kimesikitishwa na kulaani vitendo na matukio ya ukatili uliopindukia unaofanywa na baadhi ya walimu kuwapiga wanafunzi bila kufuata sheria zinavyoelekeza na kupelekea baadhi yao kuathirika kisaikolojia na hata kupoteza maisha kutokana na vipigo hivyo.

Miongoni mwa matukio ya kusikitisha ni lile la tarehe 27 Agost ambapo MWANAFUNZI wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kibeta, Bukoba mkoani Kagera, Sperius Eradius (13) alifariki dunia baada ya kupigwa na mwalimu wake kwa kutuhumiwa kuiba pochi ya mwalimu.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Tarehe 16 Julai, 2018,Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani   (UNFPA),lina Ujumbe Kutoka Jumuia ya Umoja Ulaya (EU) kwa Tanzania Jumuiya ya Afrika mashariki (EAC), Ubalozi wa Uingereza, Ubalozi wa  Ireland, Ubalozi wa Uholanzi, pamoja na ubalozi wa Kanada kwa pamoja watakuwa wenyeji wa shughuli ya kuonesha juhudi zinazohitajika katika kukomesha suala la ukeketaji hapa nchini.  Katika tukio hilo Kutakuwa na hotuba kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, wazee na Watoto. Pia kutakuwa  na Hotuba ya mwakilishi wa Jeshi la polisi Tanzania na wanaharakati wa haki za binaadamu pia kutakuwa na uzinduzi wa filamu mpya   yenye hadi ya kimataifa inayoitwa “In the Name of Your Daughter”,. Baadsa ya filamu hiyo kutakuwa na wasaa wa maswali na majibu kutoka kwa washiriki wa tukio hilo.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

On 16 July, 2018,the United Nations Population Fund (UNFPA),the Delegation of the European Union (EU) to Tanzania and the East African Community (EAC), the British High Commission, the Embassy of Ireland, the Embassy of the Kingdom of the Netherlands, and the High Commission of Canada will host an event to highlight the intensified efforts that are needed to end female genital mutilation (FGM) in the country. The event will include remarks by the Government of the United Republic of Tanzania represented by the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children and the Tanzania Police Force, as well as human rights activists, and the screening of the internationally acclaimed film “In the Name of Your Daughter”, followed by a Question and Answer (Q&A) Session with the audience.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania – TAMWA, kinampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr John Pombe Magufuli kwa kuguswa na matukio ya ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikiathiri hali ya kijamii na kiuchumi nchini.

Takwimi za shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha Tanzania inapoteza 3.4 ya hali ya uzalishaji (GDP) katika kugharamia masuala yoyote yanayotokana na ajali za barabarani yakiwemo matibabu na madhara mengine kama kupoteza maisha, majeraha makubwa, ulemavu wa kudumu, mali kuharibika pamoja na vifo vya wananchi. 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake –TAMWA, kinaungana na mashirika mengine yanayopinga ukatili wa kijinsia na kutetea haki za binadamu kote nchini kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika ambayo huadhimishwa tarehe 16 Juni kila mwaka.

Maadhimisho hayo ambayo yatafanyika wilayani Ilala Kata ya kivule leo tarehe 14 Juni, 2018 kuanzia saa tatu Asubuhi hadi saa tano katika viwanja vya stendi ya Mbondole, Mgeni rasmi ni Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Sophia Mjema ambapo kauli mbiu mwaka huu ni “Kuelekea Uchumi wa Viwanda, Tusimwache Mtoto Nyuma’’ inamlenga kila mzazi, mlezi, ndugu, jamaa, jirani na rafiki kumpenda mtoto kwa namna yoyote ile, kuhakikisha anatunzwa vizuri na haki zake zinalindwa ipasavyo ili atimize ndoto zake. 

Latest News and Stories

Search