News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Mwandishi Wetu, Tamwa.
Kisarawe. Wadau wa maendeleo na ustawi wa jamii Wilaya ya Kisarawe wametaja  moja ya sababu zinazochangia ubakaji na ndoa za utotoni wilaya ya Kisarawe kuwa ni madereva bodaboda.
Wakizungumza leo Septemba 18 katika warsha ya wadau wa kutokomeza ukatili wa kijinsia dhidi ya Wanawake na watoto iliyofanyika wilayani humo wadau hao wamesema umbali wa shule unasababisha wanafunzi walaghaiwe na madereva bodaboda na kuishia kupata mimba au kubakwa.
Akizungumza katika warsha hiyo iliyoandaliwa na Chama Cha Wanahabari Wanawake(Tamwa) Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo amesema ushirikiano wa wadau ni muhimu katika kumaliza ukatili huo.
"Ndiyo maana tumefurahi kwa Tamwa kuja hapa kwa sababu wanalifahamu tatizo hili kwa upana. Lakini pia tumeiwata wazee maarufu na viongozi wa dini na maofisa ustawi wa jamii pamoja na wanasheria. Nia yetu tupate suluhisho la tatizo hilo,"amesema. 
Amesema kesi nyingi hazifiki mwisho kwa sababu ya kukosekana kwa ushirikiano wa wanafamilia pindi kesi zinapofika mahakamani. 
Mkurugenzi was Tamwa, Eda Sanga amesema unyanyasaji wa  watoto unaleta simanzi na ndiyo maana chama hicho kinapaza sauti na kusema imetosha Sasa.
"Kwa kauli moja tunasema huu unyanyasaji,ukatili, utovu wa nidhamu , visasi, uonevu , dhuluma na ukiukwaji wa  haki za mtoto kiujumla utokomezwe na utokomee,"amesema. 
Tamwa inatekeleza mradi unaowezesha Wanawake na kujenga usawa wa kijinsia katika Wilaya saba Tanzania bara.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake - TAMWA kimefurahishwa na kinazidi kuupongeza Umoja wa Wabunge Wanawake nchini kwa juhudi ambazo unaendelea kuonyesha kutafuta kiasi cha Sh.3.2bilioni za kujenga vyoo vya mfano kwa wanafunzi wasichana na wenye mahitaji maalumu katika majimbo 264 ya uchaguzi nchini.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake nchini – TAMWA kimesikitishwa na kulaani vitendo na matukio ya ukatili uliopindukia unaofanywa na baadhi ya walimu kuwapiga wanafunzi bila kufuata sheria zinavyoelekeza na kupelekea baadhi yao kuathirika kisaikolojia na hata kupoteza maisha kutokana na vipigo hivyo.

Miongoni mwa matukio ya kusikitisha ni lile la tarehe 27 Agost ambapo MWANAFUNZI wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kibeta, Bukoba mkoani Kagera, Sperius Eradius (13) alifariki dunia baada ya kupigwa na mwalimu wake kwa kutuhumiwa kuiba pochi ya mwalimu.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Tarehe 16 Julai, 2018,Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani   (UNFPA),lina Ujumbe Kutoka Jumuia ya Umoja Ulaya (EU) kwa Tanzania Jumuiya ya Afrika mashariki (EAC), Ubalozi wa Uingereza, Ubalozi wa  Ireland, Ubalozi wa Uholanzi, pamoja na ubalozi wa Kanada kwa pamoja watakuwa wenyeji wa shughuli ya kuonesha juhudi zinazohitajika katika kukomesha suala la ukeketaji hapa nchini.  Katika tukio hilo Kutakuwa na hotuba kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, wazee na Watoto. Pia kutakuwa  na Hotuba ya mwakilishi wa Jeshi la polisi Tanzania na wanaharakati wa haki za binaadamu pia kutakuwa na uzinduzi wa filamu mpya   yenye hadi ya kimataifa inayoitwa “In the Name of Your Daughter”,. Baadsa ya filamu hiyo kutakuwa na wasaa wa maswali na majibu kutoka kwa washiriki wa tukio hilo.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

On 16 July, 2018,the United Nations Population Fund (UNFPA),the Delegation of the European Union (EU) to Tanzania and the East African Community (EAC), the British High Commission, the Embassy of Ireland, the Embassy of the Kingdom of the Netherlands, and the High Commission of Canada will host an event to highlight the intensified efforts that are needed to end female genital mutilation (FGM) in the country. The event will include remarks by the Government of the United Republic of Tanzania represented by the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children and the Tanzania Police Force, as well as human rights activists, and the screening of the internationally acclaimed film “In the Name of Your Daughter”, followed by a Question and Answer (Q&A) Session with the audience.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania – TAMWA, kinampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr John Pombe Magufuli kwa kuguswa na matukio ya ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikiathiri hali ya kijamii na kiuchumi nchini.

Takwimi za shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha Tanzania inapoteza 3.4 ya hali ya uzalishaji (GDP) katika kugharamia masuala yoyote yanayotokana na ajali za barabarani yakiwemo matibabu na madhara mengine kama kupoteza maisha, majeraha makubwa, ulemavu wa kudumu, mali kuharibika pamoja na vifo vya wananchi. 

Latest News and Stories

Search