News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Wakati dunia ikiadhimisha wiki ya Umoja wa Mataifa ya Usalama Barabarani, viongozi wa ngazi mbalimbali nchini wametakiwa kuchukua hatua katika kudhibiti ajali za barabarani ili kuokoa maisha ya wananchi yanayopotea kila kukicha kwa kusababishwa na ajali za barabarani nchini.

Wiki ya Umoja Wa Mataifa ya Usalama Barabarani ilianzishwa kupitia Azimio la Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Oktoba 2005 ikiwa na lengo la kuboresha usalama wa barabarani duniani. Azimio hili liliitaka Tume ya Umoja wa Mataifa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kuandaa kwa pamoja wiki hiyo. Kwa mara ya kwanza wiki ya umoja wa mataifa ya usalama barabarani iliazimishwa mwaka 2007 , ya pili mwaka 2013, ya tatu 2015, na ya nne 2017. Mwaka huu ni maadhirimisho ya tano, ambayo yanaadhimishwa kuanzia tarehe 6 mpaka tarehe 12 mwezi huu wa tano 2019.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania,(TAMWA), tumepokea kwa masikitiko kifo cha mmiliki wa kampuni za IPP nchini, Dk Reginald Mengi ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa wamiliki wa vyombo vya habari MOAT.

 

Kifo hiki ni pigo kubwa kwa tasnia ya habari nchini, pia kwa jamii ya Watanzania hasa kwa watu wenye ulemavu.

 

Dk Mengi ameacha alama katika tasnia ya habari kwa kuanzisha vyombo vya habari na alibeba dhamana ya kuwa mlezi kwa wanahabari nchini, na alileta heshima katika tasnia hii nchini.

 

Atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika tuzo za umahiri wa habari za Ejat hasa katika maudhui kuhusu watu wenye ulemavu, ambako amekuwa akidhamini tuzo hizo.

Atakumbukwa kwa upendo wake  mkubwa kwa wenye ulemavu. Dk Mengi amekuwa muumini mzuri wa masuala ya usawa wa kijisia katika taasisi zake ambapo ametoa nafasi za ajira na za uongozi kwa wanawake na wanaume.

 

Pia Dk Mengi alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa Shirikisho la wenye Viwanda nchini.

Dk Mengi alikuwa na ndoto nyingi, mojawapo ni ya kushirikiana  na serikali kutokomeza  umaskini kama alivyoandika kwenye ukurasa wake wa twitter Machi 19, ''Ndoto yangu ni kushirikiana na serikali kutokomeza kabisa umaskini Tanzania''

 

Ulale salama Dk Mengi, tutaendelea kuyaishi maneno yako kwa mfano nukuu yake ya Januari 7 aliyotuma kupitia mtandao wake wa twitter akisema: ''Kwa unyenyekevu ninawashauri  watanzania wenzangu kuufanya mwaka 2019 kuwa mwaka wa upatanisho na msamaha, chuki ni mzigo mzito kuubeba mioyoni mwetu, kupendana ni njia peee ya kusonga mbele''.

 

Pumzika kwa amani Dk Mengi.

 

Rose Reuben

MKurugenzi TAMWA

 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Aprili 6, 2019. Wanachama wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, (TAMWA), kimemchagua Joyce Shebe kuwa Mwenyekiti mpya wa bodi ya chama hicho.

 

 Katika uchaguzi huo, pia wanachama waliwachagua wajumbe wa bodi ambao ni wanahabari Leah Mushi, Raziah Mwawanga na Halima Muselem kutoka Zanzibar.

 Kabla ya Shebe, Alakok Mayombo alikuwa Mwenyekiti wa bodi ya chama hicho aliyeongoza kuanzia 2016 mpaka mwaka huu.

 Uchaguzi huo umefanyika katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika leo Aprili 6, 2019.

“Mimi si mzungumzaji  sana, mimi ni msikilizaji zaidi. Lakini ninachoweza kusema kwa sasa ni kuwa TAMWA ni wanachama. Sisi wanachama ndiyo tutakaoijenga TAMWA,”Joyce Shebe.

Shebe aliwataka wanahabari wanawake kuongeza ushirikiano kwa kuwa kwa kutumia kalamu zao wanaweza kuibadili au kuibomoa jamii.

 

Rose Reuben

Mkurugenzi Mkuu

TAMWA

Email: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it..

Mobile: 0764438084

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) leo Aprili 5, kwa kushirikiana na Hospitali ya Narayani India wametoa  elimu ya afya pamoja na ushauri wa kitaalamu kwa wanahabari wanawake kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kwa lengo la kuwajengea uwezo juu ya afya ya uzazi na magonjwa na magonjwa ya saratani.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika  jijini Dar es salaam, mwenyekiti wa TAMWA, Bi. Alakok Mayombo alisema washiriki wa mafunzo hayo watajengewa uwezo kuhusu afya ya uzazi pamoja na matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii.

“Katika kipindi cha siku mbili za mkutano mkuu wa chama chetu,  Tulizungumza na marafiki wa TAMWA Narayana hospital ambao walikubali kutoa elimu ya afya uzazi kwa wakina mama kupitia kipengele chao cha awareness kuhusu hasa magonjwa ya kansa" Alisema Bi. Mayombo. 

Alisema kupitia elimu ambayo itatolewa kwa washiriki hao itawawezesha kuwasaidia kujilinda na kupambana  kansa kwa akina mama. 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA Rose Reuben, alisema, mbali na mafunzo hayo ya afya ya uzazi pia watatoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya ya mitandao ya kijamii.

“Ni lazima jamii itambue sheria ya maudhui ya mtandao pamoja na sheria za vyombo vya habari katika mitandao ya kijamii.  Lengo letu ni kujiongezea ujuzi katika maeneo haya, hivyo  watu wa TCRA watakuja kutusaidia kutoa mafunzo kuhusu  matumizi ya mtandao ni”. Alisema Rose.

Nae daktari kutoka Hospitali ya Narayana, Bwana Limbanga Freddie alisema, tafiti zinaonyesha kumekuwepo na ongezeko kubwa la wagonjwa wa kansa kutokana na mabadiliko ya mfumo wa maisha pamoja na kutofanya mazoezi, kutokufanya kazi ngumu na kutumia vyakula ambavyo ni hatari kwa afya.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Wakati dunia ikisherehekea Siku ya Wanawake Duniani, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA)kinakuletea wanahabari wakongwe waanzilishi wa TAMWA. Hiki ndicho wanachokisema katika maadhimisho haya ya Siku ya Wanawake Duniani.

Halima Shariff, yeye ni mtafiti, kiongozi na mwalimu . Ni miongoni mwa waasisi wa TAMWA aliyezaliwa kutoka katika familia ya kawaida kabisa, mkoani Tanga.
 
Akiwa ni mtaalamu na nguli wa habari nchini, Halima amewahi kuandika katika gazeti la Daily News miaka ya 80 na mtangazaji wa  Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani(Deustche Welle).
 
Pamoja na fani ya habari, Halima amewahi  kushika nafasi kubwa katika taasisi za kimataifa  na kwa sasa ni Mkurugenzi wa Mradi wa Uzazi wa Mpango wa Advanced Family Planning Project(AFP).
 
Ni miongoni mwa wanawake waliosimamia kidete maendeleo ya wanawake na watoto katika masuala ya elimu, afya ya uzazi na Virusi vya Ukimwi. 
 
Amewahi kuongoza miradi mikubwa ya afya  ikiwamo ya Shirika la Misaada la watu wa Marekani USAID. Ameshiriki katika kutetea hadi  kufanikisha kupitishwa kwa muswada wa  masuala ya Ukimwi, kuanzishwa kwa sera ya HIV/AIDS katika maeneo ya kazi. Amewahi pia kuwa Kamishna wa Tume ya Ukimwi Tanzania (TACAIDS). 
 
Anachokisema katika kuadhimisha Sharif katika kuadhimisha Siku ya Wanawake duniani: 
 
“Kuimarisha nafasi ya mwanamke katika nyanja zote katika jamii ni harakati endelevu zinazohitaji jitihada za pamoja zenye kasi inayoongezeka kizazi hadi kizazi. Kwa mantiki hiyo Tanzania tumefanikiwa kujenga uelewe wa jamii kuhusu nafasi muhimu ya mwanamke katika kujenga familia na katika maendeleo kwa ujumla” 
 
“Lakini bado hatujawekeza vya kutosha katika kuhakikisha afya ya mwanamke inapewa kipaumbele ukizingatia kwamba bado wastani wa kuzaa wa taifa ni watoto sita kwa mwanamke wa rika la uzazi (15-49). 
 
“Inatia moyo kwamba serikali imekuwa ikielekeza nguvu huko lakini ni eneo linalohitaji kutazamwa zaidi kwani mara nyingi wanawake hukosa fursa za kujiendeleza kutokana na changamoto za uzazi,”

Latest News and Stories

Search