Press Release

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Dar Es Salaam, Machi, 19, 2021. Bodi ya wanachama, wanachama na Sekretariati ya Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinampongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Rais Samia Suluhu Hassan aliyekuwa Makamu wa Rais, ameapishwa leo, Machi 19, 2021 baada ya kifo cha Hayati Rais John Magufuli ikiwa ni utekelezaji wa hatua za kikatiba na kisheria inayoeleza kuwa, Makamu wa Rais ataapishwa kuwa Rais, endapo Rais aliyeko madarakani atafariki dunia. 
 
TAMWA tunampongeza Rais huyu wa awamu ya sita, tukiamini kuwa ni kiongozi amestahili, makini na  anayekwenda kusimamia maadili, kusimamia katiba na kuzisimamia haki za wanawake na watoto. 
 
Tunaamini Rais wetu mpya ni muumini wa usawa wa kijinsia na hivyo atakwenda kuwa mstari wa mbele kusimamia sheria na haki zinazolinda watu wote, ikiwa ni pamoja na mwanamke hakika hatuna shaka na utendaji wake, TAMWA inaamini   ‘Wanawake Wanaweza  na sio kwa kuwezeshwa pekee bali waliaminika tangu enzi kwa kupewa madaraka ya kuwa  wasimamizi wakuu wa familia, kuanzia ngazi ya malezi,  jambo ambalo linawafanya kuwa imara, wanyenyekevu, wavumilivu na makini  zaidi hata katika nafasi za kisiasa na uongozi katika maeneo mengine.
 
Tangu akiwa Makamu wa Rais, amekuwa chachu kwa watoto wa kike na wanawake wa Tanzania katika kuwaza makubwa kwenye kuleta mabadiliko katika jamii ya kijinsia.
 
Hatuna  shaka na  utendaji kazi wa Rais wetu mpya na  historia yake ya kufanya kazi katika taasisi zisizo za kiserikali, kwa zaidi ya miaka kumi ambapo alijikita zaidi katika harakati za usawa kijinsia. 
Hivyo basi tunaamini kuwa atakwenda kusimamia ajenda hizo akiwa anaelewa kwa kina umuhimu wa usawa wa kijinsia na umuhimu wa kumaliza ukatili wa kijinsia,
 
Rais Samia Suluhu Hassan ameweka historia Afrika Mashariki  kwa kuwa mwanamke wa kwanza kuwa Rais, jambo ambalo  litaacha alama kwa vizazi vijavyo na kisha kuulinda  na kuuheshimisha mfumo wa ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi. 
Wakati tukiendelea kuomboleza msiba wa Hayati Rais John Magufuli, TAMWA ina imani kuwa, Rais Mama Samia Suluhu ataendelea kusimamia kauli yake  ile ya kuitaka jamii  kupinga na kupambana na vitendo vya ukatili katika maeneno yao.
 
Hongera Rais Samia Suluhu Hassan! Hongera Tanzania!
 
Rose Reuben,
Mkurugenzi Mtendaji,
TAMWA.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Mheshimiwa, Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Marekani Dk. Willow Williamson, Mwakilishi kutoka Dawati la jinsia Mkoa wa Kinondoni Mathias Mulumba, Mwakilishi kutoka Muungano wa ‘Men engage Tanzania’ Marcela Lungu na Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali nchini, Habari za asubuhi.
UKATILI WA JINSIA: “MABADILIKO YANAANZA NA MIMI”
Wakati dunia ikiadhimisha Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) na CRC kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani Tanzania, (UsEmbassyTz) tunawasisitiza wanajamii kuibua na kufichua matukio yote ya ukatili wa kijinsia yanayoendelea kuanzia katika ngazi ya familia na katika taasisi kama vile mashuleni, vyuoni na sehemu kazi.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Dar es Salaam, Novemba 12, 2020. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, (TAMWA) kinalaani vikali, matukio ya ukatili wa kijinsia yanayoendelea hapa nchini katika kipindi cha miezi miwili.

Hivi karibuni, vyombo vya habari vimeripoti matukio kadhaa ya ukatili wa kijinsia hasa ubakaji wa watoto yanayoashiria kuwa bado vitendo hivi vinaendelea licha ya kuwepo sheria, matamko na sera zinazopinga vikali matukio hayo.

Miongoni mwa matukio hayo ni pamoja na lile la Novemba 11, mwaka huu, ambapo  Mwenyekiti wa Kijiji cha Ijinga, Wilaya ya Magu, Badri  Masengo (40) anayedaiwa kumpa ujauzito mwanafunzi wa darasa la sita,Shule ya Msingi Ijinga mwenye umri wa miaka 15 .

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, Abeda Rashid Abdallah.....
Ndugu wadau wa masuala ya jinsia.
Viongozi wa serikali,
Wanahabari, 
Itifaki imezingatiwa!
 
Zanzibar, February 4, 2021. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kina furaha kubwa kupata fursa hii adhimu,  leo Februari 4th, 2021, ya kukutana tena na wadau wake muhimu walioshiriki katika utekelezaji wa mradi wa Wanawake Sasa’ uliofadhiliwa na taasisi ya kimataifa ya African Women, Development Fund (AWDF).
 
Mradi wa ‘Wanawake Sasa’ umehitimishwa kwa mafanikio makubwa na kamwe mafanikio hayo yasingepatikana bila nyinyi wadau muhimu ambao mlishiriki katika kuhimiza Amani, ushirikiano  katika chaguzi na ushiriki wa wanawake katika siasa, uongozi na maamuzi.
 
Kutokana na ushirikiano wenu, tumeona namna ambavyo Rais, John Maguuli ameendelea kuteua viongozi wanawake, na hilo limethibitishwa katika kauli yake aliyoitoa Novemba, 2020 mara baada ya uchaguzi kuwa; ataendelea kuwaamini wanawake. 
Kwa msingi huo napenda nitumie fursa hii kuahidi kuwa, serikali ninayoiongoza itaendelea kuwaamini wanawake katika kushika nafasi mbalimbali za uongozi, alisema Rais JPM.
 
Ndugu Mgeni Rasmi,
Si hayo tu, tumeona kivitendo, ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi na tumeshuhudia idadi ya wanawake zaidi ya 230 katika bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwamo mawaziri wanawake.
Kwa upande wa Zanzibar, tuliona uthubutu wa kinamama wawili, waliojitokeza na kuchukua fomu za kuwania urais. 
 
Ndugu mgeni rasmi,
TAMWA inaishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na ile ya bara kwa kushiriki katika matukio ya utekelezaji wa mradi huu katika maeneo manne, ikiwamo Zanzibar, Arusha, Dar es Salaam na Dodoma. 
 
Viongozi wa Serikali wameshiriki kwa kiasi kikubwa katika kufungua, kutoa nasaha na kutoa ushauri kwa TAMWA katika ajenda hii ya ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi, Amani na mshikamano. Tunawashukuru!
 
Ndugu Mgeni Rasmi
Kupitia midahalo ya wanawake wanasiasa iliyofanywa katika maeneo yetu manne ya mradi, wanawake wanasiasa zaidi ya 150 kutoka vyama mbalimbali vya siasa nchini,  walipata fursa ya kujifunza umuhimu wa kutumia vyombo vya habari kueneza ajenda zao za kisiasa.
 
Pia kupitia midahalo hiyo, waliweza kujifuza changamoto za kila mmoja hasa katika mrengo wa ukatili wa kijinsia, ikiwamo rushwa ya ngono na kujua namna ya kukabiliana na changamoto za aina hiyo.
Wanawake wanasiasa waliopata mafunzo waliteuliwa kuanzia ngazi ya kanda hadi kitaifa. 
 
Ndugu Mgeni Rasmi,
TAMWA iliwaleta pamoja viongozi wa dini 50 kutoka maeneo hayo manne ambao walishiriki kikamilifu kueneza Amani wakati wa uchaguzi na kusisitiza ushiriki wa wanawake katika siasa, uongozi na maamuzi. Haya kwetu ni mafanikio kwani, nafasi ya viongozi wa dini katika kuhubiri Amani na kuwaleta watu pamoja, vilisaidia katika kufanyika kwa uchaguzi wa Amani, huru na wa haki. 
 
Ndugu mgeni rasmi, 
Kama ujuavyo TAMWA inatumia silaha yake kuu, ambayo ni vyombo vya habari katika kufikisha ajenda kwa jamii, na hivyo iliwapa mafunzo wanahabari zaidi ya 70 kutoka katika maeneo hayo manne. Wanahabari hao walifundishwa na kupata ujuzi kuhusu umuhimu wa ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi.
 
Wanahabari hao baada ya mafunzo walifanikisha kuchapishwa kwa Makala za magazeti 40, vipindi vya redio  na televisheni, talk show na kuongeza wigo wa  idadi ya wanahabari tuliofanya nao kazi awali na kuwafikia wa wanahabri zaidi kutoka Zanzibar, Arusha hadi  Dodoma ambao waliandaa Makala za kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi. 
 
Ndugu mgeni rasmi, 
TAMWA na wanahabari kupitia kazi zao, walishirikiana na kuwafikia wanawake ambao awali waliogopa kushiriki katika siasa na uongozi. Hii iliongeza idadi ya wanawake waliojitokeza kuwania nafasi za uongozi kuanzia ngazi za chini hadi nafasi za ubunge. 
 
Taarifa fupi ya mradi Wanawake Sasa
Wanawake Sasa ni mradi uliotekelezwa kwa ushirikiano wa asasi tatu, TAMWA, WiLDAF na GPF Tanzania, chini ya ufadhili wa Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake wa Afrika (AWDF).
Mradi huu ulikuwa na malengo makuu matatu, kuongeza idadi ya wanawake katika nafasi za uongozi na maamuzi, kwa kuwahamasisha na kuwawezesha wanawake, wanawake wenye ulemavu na vijana kuwa viongozi.
 
Lengo la pili, ni kuwahamasisha na kuwawezesha wanawake katika vyama vya siasa kuwania nafasi za uongozi katika vyama vyao. 
Lengo la tatu ni, kukuza wanawake kisiasa, kuhamasisha Amani katika chaguzi kupitia vyombo vya habari kwa kuishirikisha jamii. Mradi huu wa mwaka mmoja, ulianza kutekelezwa Januari Novemba 2020 na utekelezaji wake ulivihusisha vyama vitano vya siasa (CCM,ACT WAZALENDO,CUF,CHADEMA NA NCCR-MAGEUZI) katika kanda nne Arusha, Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar.
 
Mkurugenzi Mtendaji,
 
Rose Reuben.
 
TAMWA.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania kwa kushirikiana na Mtandao wa wadau kutoka asasi za kiraia unaotetea marekebisho ya sheria na sera ihusuyo usalama barabarani Tanzania na kuratibiwana Chama cha Wanawake Wanasheria Tanzania (TAWLA) kwa pamoja tunaungana na watanzania wote na Dunia kwa ujumla kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kuwakumbuka Wahanga wa ajali za Barabarani.

Siku hii huadhimishwa kimataifa, kila ifikapo Jumapili ya wiki ya tatu (3) ya mwezi Novemba kila mwaka Kwa ajili ya kuwakumbuka waathirika wa ajali za barabarani na kuwaenzi mamilioni ya watu waliopoteza maisha na wengine wengi walioathirika kwa njia moja au nyingine kutoka na ajali hizo.

Kauli mbiu ya kimataifa kwa mwaka huu inasema; ‘Kumbuka, Saidia,Chukua Hatua’.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Oktoba 11, 2020, Dar Es Salaam. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), kinaungana na watanzania, pamoja na watu wote ulimwenguni kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike. 
Kauli mbiu kitaifa kwa mwaka huu, inasema; Tumuwezeshe mtoto wa kike, kujenga taifa lenye usawa na kimataifa, kauli mbiu inasema: Sauti yangu, ni mustakabali wetu wa usawa.’ 
 
Kila mwaka ifikapo Oktoba 11, dunia huadhimisha siku hii ili kukumbushana madhila wanayopitia watoto wa kike na kuikumbusha jamii nguvu iliyomo kwa watoto hao.
Kwa mfano ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto(UNICEF) inaeleza kuwa watoto wa kike milioni 12 huolewa kabla ya kufikisha umri wa miaka 18 kila mwaka?
 
Watoto wa kike takribani milioni 6 hadi 17 duniani kote hawajapata nafasi ya kwenda shule na inaelezwa kuwa watoto wa kike milioni 15 duniani, wenye umri wa kuanzia miaka 15 hadi 19 wameathirika kisaikolojia kutokana na manyanyaso ya ukatili wa kijinsia, ikiwamo kubakwa, vipigo na udhalilishaji wa kingono.  
Takwimu zinazojitokeza zinaonyesha kuwa tangu kuzuka kwa COVID-19, unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana (VAWG), na hasa unyanyasaji wa nyumbani, umeongezeka kwa kasi.
 
TAMWA ni shirika lisilo la kiserikali, lilioanzishwa mwaka 1987  kwa lengo la kutetea haki na ustawi wa wanawake na watoto, kupitia vyombo vya habari hivyo basi, wakati tunaadhimisha siku hii, tunaiasa jamii kuacha mifumo yote inayomkandamiza mtoto wa kike na badala yake tunahimiza taifa lenye amani,  linalozingatia ulinzi kwa watoto wa jinsia zote. 
 
Kupitia miradi mbalimbali tuliyofanya, TAMWA imebaini kuwepo kwa mifumo kandamizi kwa watoto wa kike, mifumo hiyo imepelekea baadhi ya jamii kukumbatia vitendo vya   ubakaji, ulawiti, ndoa za utotoni, manyanyaso kutoka ndani ya familia, kunyimwa haki ya kupata elimu na kugubikwa na mzigo wa majukumu ya kazi za nyumbani. 
 
Changamoto hizi na nyingine nyingi, zimechangia mtoto wa kike kukosa fursa ya elimu, kuathirika na maradhi, kuathirika kisaikolojia na kukosa nafasi yake ya kufurahia utoto wao kutokana na mimba za utotoni na ndoa za utotoni. 
 
Taifa lenye amani ni lile linalothamini haki za watoto, ikiwamo haki ya kuishi kwa furaha, kupata huduma za msingi ikiwemo huduma ya afya, elimu na amani. 
 
Kwa mujibu wa takwimu za madawati ya jinsia ya hapa nchini imebainika kuwa mimba za utotoni ziliongezeka kwa kasi wakati wa likizo ya miezi mitatu  mwaka huu iliyosababishwa na mlipuko wa virusi vya corona. 
Hivyo basi, TAMWA inaiomba serikali kuandaa utaratibu wa ulinzi, utoaji taarifa na ufuatiliaji kwa watoto hasa wakati wa dharura za milipuko ya magonjwa au majanga kama Covid-19 ili kuepusha madhara yanayoweza kuzuilika.
 
Wakati huo huo takwimu za uhalifu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) zinaonyesha kuwa, katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2016 jumla ya kesi 10,551 za uhalifu dhidi ya watoto ziliripotiwa katika vituo vya polisi, ukilinganisha na kesi 9,541 kuanzia Januari hadi Desemba 2015. Uhalifu huo ni pamoja na ubakaji, utelekezaji wa watoto, wizi wa watoto, ukeketaji na mashambulio ya kudhuru mwili.
 
“TAMWA tunaomba wazazi, walezi na watoto wa kike,wanaofanyiwa ukatili, wavunje ukimya, kwani zipo asasi, taasisi na vyombo vya serikali ambavyo wanaweza kuvitumia kuripoti matukio ya ukatili wa kijinsia 
Ndiyo  maana kauli mbiu ya kimataifa ya mwaka huu inasema, sauti yako, ni mustakabali wetu wenye usawa. 
Tunasisitiza serikali ijenge mifumo imara ya utoaji taarifa ili tujue kwa kina sababu na kiwango cha ukatili huu. Kwa kufanya hivi tutapata mifumo bora ya kukabiliana na ukatili dhidi ya watoto nchini .
 
Tukumbuke kuwa, watoto hawa, wakiwamo wa kike ni taifa la kesho, hivyo basi wanapoharibiwa misingi bora ya maisha, tunakwenda kuharibu mustakabali wa taifa, Joyce Shebe, Mwenyekiti wa TAMWA.
 
Hatutaweza kupata wafanyabishara, wakulima, mawaziri, wabunge, wakurugenzi na viongozi bora wanawake, iwapo watoto wa kike wa sasa  watabakwa, watapata mimba, wataozwa katika umri mdogo, watashambuliwa na kunyanyaswa. 
 
Tuna taarifa kuwa ukatili kwa watoto unafanywa na watu wa karibu sana, wapo wazazi, walezi wanaochochea au kuchangia kwa namna moja ama nyingine ukatili kwa watoto wa kike, ikiwamo kuwaozesha, kuwabaka, kuwaumiza miili yao na kuwazuia kupata elimu, tunakemea haya na tunataka serikali iendelee kuwachukulia  hatua kali wazazi/walezi wa aina hii, Shebe.
 
TAMWA Bado tunakumbusha umuhimu wa mabadiliko ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971 tukiamini kuwa, mtoto wa kike mwenye umri chini ya miaka 18, bado hajapevuka vya kutosha kumudu majukumu ya ndoa na kubeba ujauzito. 
 Tunahimiza zaidi elimu kwa mtoto wa kike, fursa ya kusikilizwa, haki ya kupata huduma za afya na zaidi hasa mtoto wa kike na nafasi sawa na mtoto wa kiume, Shebe.
 
 Tunaipongeza serikali, chini ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kwa jitihada za ulinzi na afya kwa watoto wa kike Tanzania. 
TAMWA bado tunaishikilia kauli yetu isemayo: Mtoto wa mwenzio, ni wako, mlinde na nirudie kauli mbiu ya mwaka huu ambayo inasema Sauti yangu, ni mustakabali wetu wa usawa.
 
Watoto pazeni sauti zenu mara tu mnapoona dalili za kufanyiwa ukatili.
 
Joyce Shebe
Mwenyekiti, TAMWA

Search