Press Release

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Mheshimiwa, Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Marekani Dk. Willow Williamson, Mwakilishi kutoka Dawati la jinsia Mkoa wa Kinondoni Mathias Mulumba, Mwakilishi kutoka Muungano wa ‘Men engage Tanzania’ Marcela Lungu na Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali nchini, Habari za asubuhi.
UKATILI WA JINSIA: “MABADILIKO YANAANZA NA MIMI”
Wakati dunia ikiadhimisha Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) na CRC kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani Tanzania, (UsEmbassyTz) tunawasisitiza wanajamii kuibua na kufichua matukio yote ya ukatili wa kijinsia yanayoendelea kuanzia katika ngazi ya familia na katika taasisi kama vile mashuleni, vyuoni na sehemu kazi.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Dar es Salaam, Novemba 12, 2020. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, (TAMWA) kinalaani vikali, matukio ya ukatili wa kijinsia yanayoendelea hapa nchini katika kipindi cha miezi miwili.

Hivi karibuni, vyombo vya habari vimeripoti matukio kadhaa ya ukatili wa kijinsia hasa ubakaji wa watoto yanayoashiria kuwa bado vitendo hivi vinaendelea licha ya kuwepo sheria, matamko na sera zinazopinga vikali matukio hayo.

Miongoni mwa matukio hayo ni pamoja na lile la Novemba 11, mwaka huu, ambapo  Mwenyekiti wa Kijiji cha Ijinga, Wilaya ya Magu, Badri  Masengo (40) anayedaiwa kumpa ujauzito mwanafunzi wa darasa la sita,Shule ya Msingi Ijinga mwenye umri wa miaka 15 .

User Rating: 3 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar InactiveStar Inactive

Dar Es Salaam , Oktoba 2, 2020.

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) tunachukua fursa hii, kuutambulisha kwenu mradi wa “Rushwa ya ngono miongoni wanahabari wanawake katika vyombo vya habari” unaofadhiliwa na Mfuko wa Wanawake Tanzania - Women Fund Tanzania (WFT).

TAMWA ilianzishwa 1987, na wanahabari wanawake, kwa lengo la utetezi wa ustawi wa haki za wanawake na watoto kupitia taaluma yao na vyombo vya habari.

“Kwa kuwa TAMWA kiini chake ni wanahabari,  hivyo basi jukumu la utekelezaji wa mradi huu, unaowalenga wanahabari litakwenda kutekelezwa kwa kiasi kikubwa kwa kushirikiana na nyinyi wanahabari na vyombo vya habari,” Rose Reuben, Mkurugenzi Mtendaji, TAMWA.

TAMWA tunakwenda kuutekeleza mradi huu tukifahamu kabisa kuwa zipo tafiti mbalimbali zinazoonyesha kuwa bado kuna rushwa ya ngono ndani ya vyumba vya habari.

“Wakati huo huo, wanahabari wameonekana kuwa kimya kuhusu matukio hayo, aidha kwa kuogopa kupoteza ajira zao au pengine wakichelea kuaibika zaidi pindi watakapoweka wazi masahibu yao,” Reuben

Kimsingi, rushwa ya ngono haikubaliki na ni tabia isiyopendeza inayoshusha utu na kuwafanya waathirika kudhalilika, kupata msongo wa mawazo na kukosa kujiamini mahala pa kazi, lakini baya zaidi ni kuwa matukio mengi hayaripotiwi.

Baadhi ya watafiti, kama Barton A na Storm, (2014) walibaini kuwa asilimia 48 ya wanahabari wanawake waliohojiwa walikiri kuwa wamewahi kukumbana na  rushwa ya ngono ndani ya vyumba vya habari kwa namna moja au nyingine na asilimia 83 kati ya hao, walisema hawakuripoti matukio hayo.

“Ombwe hili ni kubwa na huenda likawaathiri hata wanahabari wachanga walio vyuoni, ambao huenda wakakataa tamaa ya kuingia katika tasnia hii na hivyo kuizorotesha tasnia lakini baya zaidi, kukosa wanahabari wanawake katika nafasi za juu za uongozi na wenye mafanikio katika tasnia hiyo,”Reuben

Kadhalika, imebainika kuwa vyombo vyingi vya habari nchini havina sera madhubuti zilizowekwa kuwaongoza wanahabari katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinapowakumba ikiwamo masuala ya rushwa ya ngono katika mazingira ya kazi   na  hivyo kuchangia kuongezeka kwa visa vya rushwa ya ngono.

“Hivyo basi, kukiwa na ombwe kama hilo, TAMWA katika utekelezaji wa mradi huu, itafanya tathmini kwa kupitia maswali, ili kujua yanayowasibu wanahabari” Reuben

Kadhalika, TAMWA itawajengea uwezo wanahabari, wakiwamo wahariri na wanawake wanahabari walio katika vyombo vya habari.

Kisha, TAMWA itashirikiana na vyombo vya habari kufanya uchechemuzi, kufanya mazungumzo  na wamiliki wa vyombo vya habari ili kuwashirikisha matokeo ya tathmini na kuelimisha jamii kuhusu rushwa ya ngono ndani ya vyumba vya Habari na kwa kutumia mitandao ya kijamii.

Katika mradi huo TAMWA itashirikisha wadau mbalimbali  wa habari wakiwamo, MISA, TEF, MCT, TCRA na OSHA.

Mradi huo utatekelezwa jijini Dar es salaam ambapo ni kitovu cha vyombo vyingi vya habari nchini zikiwamo Redio, Runinga, magazeti na mitandao ya kijamii.

TAMWA inaamini kuwa kwa kufanya tathimini ya rushwa ya ngono katika vyombo vya habari na kuwajengea kuwajengea uwezo wanahabari, itawawezesha pia kufichua na kuandika vyema habari zinazohusu rushwa hii ambayo kwa mujibu wa mila na desturi za watanzania walio wengi imekuwa ikizungumzwa kwa kwa kificho au kutokuzungumzwa kabisa.

TAMWA inatambua kuwa uwepowa Sheria ya Rushwa ya ngono ambayo inasimamiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU)

Lakini zaidi hasa, tunataka wanahabari wapaze sauti zao, tuvunje ukimya, wayazungumze yanayowasibu, na kuondoa kabisa ukatili wa kijinsia wa aina hii ambao unachangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya tasnia ya habari ikiwa ni pamoja na kuua vipaji.

Pasipo kuvunja ukimya uliotanda dhidi ya suala la rushwa ya ngono, waathirika kujengewa uwezo wa kukusanya vidhibiti visivyokuwa na mashaka yoyote taasisi yenye mamlaka ya kushughulikia makosa haya haziwezi kufanya kazi yake kwa ufasaha na kuleta mabadiliko katika jamii yetu.

Kadhalika serikali, taasisi za habari na za jinsia, zinatakiwa kushirikiana kumaliza tatizo hili ambalo halijazungumzwa kwa kina ili tuvunje ukimya huu.

Mkurugenzi Mtendaji

Rose Reuben

TAMWA

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania kwa kushirikiana na Mtandao wa wadau kutoka asasi za kiraia unaotetea marekebisho ya sheria na sera ihusuyo usalama barabarani Tanzania na kuratibiwana Chama cha Wanawake Wanasheria Tanzania (TAWLA) kwa pamoja tunaungana na watanzania wote na Dunia kwa ujumla kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kuwakumbuka Wahanga wa ajali za Barabarani.

Siku hii huadhimishwa kimataifa, kila ifikapo Jumapili ya wiki ya tatu (3) ya mwezi Novemba kila mwaka Kwa ajili ya kuwakumbuka waathirika wa ajali za barabarani na kuwaenzi mamilioni ya watu waliopoteza maisha na wengine wengi walioathirika kwa njia moja au nyingine kutoka na ajali hizo.

Kauli mbiu ya kimataifa kwa mwaka huu inasema; ‘Kumbuka, Saidia,Chukua Hatua’.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Oktoba 11, 2020, Dar Es Salaam. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), kinaungana na watanzania, pamoja na watu wote ulimwenguni kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike. 
Kauli mbiu kitaifa kwa mwaka huu, inasema; Tumuwezeshe mtoto wa kike, kujenga taifa lenye usawa na kimataifa, kauli mbiu inasema: Sauti yangu, ni mustakabali wetu wa usawa.’ 
 
Kila mwaka ifikapo Oktoba 11, dunia huadhimisha siku hii ili kukumbushana madhila wanayopitia watoto wa kike na kuikumbusha jamii nguvu iliyomo kwa watoto hao.
Kwa mfano ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto(UNICEF) inaeleza kuwa watoto wa kike milioni 12 huolewa kabla ya kufikisha umri wa miaka 18 kila mwaka?
 
Watoto wa kike takribani milioni 6 hadi 17 duniani kote hawajapata nafasi ya kwenda shule na inaelezwa kuwa watoto wa kike milioni 15 duniani, wenye umri wa kuanzia miaka 15 hadi 19 wameathirika kisaikolojia kutokana na manyanyaso ya ukatili wa kijinsia, ikiwamo kubakwa, vipigo na udhalilishaji wa kingono.  
Takwimu zinazojitokeza zinaonyesha kuwa tangu kuzuka kwa COVID-19, unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana (VAWG), na hasa unyanyasaji wa nyumbani, umeongezeka kwa kasi.
 
TAMWA ni shirika lisilo la kiserikali, lilioanzishwa mwaka 1987  kwa lengo la kutetea haki na ustawi wa wanawake na watoto, kupitia vyombo vya habari hivyo basi, wakati tunaadhimisha siku hii, tunaiasa jamii kuacha mifumo yote inayomkandamiza mtoto wa kike na badala yake tunahimiza taifa lenye amani,  linalozingatia ulinzi kwa watoto wa jinsia zote. 
 
Kupitia miradi mbalimbali tuliyofanya, TAMWA imebaini kuwepo kwa mifumo kandamizi kwa watoto wa kike, mifumo hiyo imepelekea baadhi ya jamii kukumbatia vitendo vya   ubakaji, ulawiti, ndoa za utotoni, manyanyaso kutoka ndani ya familia, kunyimwa haki ya kupata elimu na kugubikwa na mzigo wa majukumu ya kazi za nyumbani. 
 
Changamoto hizi na nyingine nyingi, zimechangia mtoto wa kike kukosa fursa ya elimu, kuathirika na maradhi, kuathirika kisaikolojia na kukosa nafasi yake ya kufurahia utoto wao kutokana na mimba za utotoni na ndoa za utotoni. 
 
Taifa lenye amani ni lile linalothamini haki za watoto, ikiwamo haki ya kuishi kwa furaha, kupata huduma za msingi ikiwemo huduma ya afya, elimu na amani. 
 
Kwa mujibu wa takwimu za madawati ya jinsia ya hapa nchini imebainika kuwa mimba za utotoni ziliongezeka kwa kasi wakati wa likizo ya miezi mitatu  mwaka huu iliyosababishwa na mlipuko wa virusi vya corona. 
Hivyo basi, TAMWA inaiomba serikali kuandaa utaratibu wa ulinzi, utoaji taarifa na ufuatiliaji kwa watoto hasa wakati wa dharura za milipuko ya magonjwa au majanga kama Covid-19 ili kuepusha madhara yanayoweza kuzuilika.
 
Wakati huo huo takwimu za uhalifu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) zinaonyesha kuwa, katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2016 jumla ya kesi 10,551 za uhalifu dhidi ya watoto ziliripotiwa katika vituo vya polisi, ukilinganisha na kesi 9,541 kuanzia Januari hadi Desemba 2015. Uhalifu huo ni pamoja na ubakaji, utelekezaji wa watoto, wizi wa watoto, ukeketaji na mashambulio ya kudhuru mwili.
 
“TAMWA tunaomba wazazi, walezi na watoto wa kike,wanaofanyiwa ukatili, wavunje ukimya, kwani zipo asasi, taasisi na vyombo vya serikali ambavyo wanaweza kuvitumia kuripoti matukio ya ukatili wa kijinsia 
Ndiyo  maana kauli mbiu ya kimataifa ya mwaka huu inasema, sauti yako, ni mustakabali wetu wenye usawa. 
Tunasisitiza serikali ijenge mifumo imara ya utoaji taarifa ili tujue kwa kina sababu na kiwango cha ukatili huu. Kwa kufanya hivi tutapata mifumo bora ya kukabiliana na ukatili dhidi ya watoto nchini .
 
Tukumbuke kuwa, watoto hawa, wakiwamo wa kike ni taifa la kesho, hivyo basi wanapoharibiwa misingi bora ya maisha, tunakwenda kuharibu mustakabali wa taifa, Joyce Shebe, Mwenyekiti wa TAMWA.
 
Hatutaweza kupata wafanyabishara, wakulima, mawaziri, wabunge, wakurugenzi na viongozi bora wanawake, iwapo watoto wa kike wa sasa  watabakwa, watapata mimba, wataozwa katika umri mdogo, watashambuliwa na kunyanyaswa. 
 
Tuna taarifa kuwa ukatili kwa watoto unafanywa na watu wa karibu sana, wapo wazazi, walezi wanaochochea au kuchangia kwa namna moja ama nyingine ukatili kwa watoto wa kike, ikiwamo kuwaozesha, kuwabaka, kuwaumiza miili yao na kuwazuia kupata elimu, tunakemea haya na tunataka serikali iendelee kuwachukulia  hatua kali wazazi/walezi wa aina hii, Shebe.
 
TAMWA Bado tunakumbusha umuhimu wa mabadiliko ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971 tukiamini kuwa, mtoto wa kike mwenye umri chini ya miaka 18, bado hajapevuka vya kutosha kumudu majukumu ya ndoa na kubeba ujauzito. 
 Tunahimiza zaidi elimu kwa mtoto wa kike, fursa ya kusikilizwa, haki ya kupata huduma za afya na zaidi hasa mtoto wa kike na nafasi sawa na mtoto wa kiume, Shebe.
 
 Tunaipongeza serikali, chini ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kwa jitihada za ulinzi na afya kwa watoto wa kike Tanzania. 
TAMWA bado tunaishikilia kauli yetu isemayo: Mtoto wa mwenzio, ni wako, mlinde na nirudie kauli mbiu ya mwaka huu ambayo inasema Sauti yangu, ni mustakabali wetu wa usawa.
 
Watoto pazeni sauti zenu mara tu mnapoona dalili za kufanyiwa ukatili.
 
Joyce Shebe
Mwenyekiti, TAMWA

User Rating: 4 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Inactive
Dar es Salaam, Oktoba 1, 2020. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kina furaha kubwa kuutambulisha umma wa Watanzania, kuanza kwa utekelezaji wa mradi wa ‘Wanawake Wanaweza’, unaofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wanawake (UN-Women).
Hii ni fursa adhimu kwa TAMWA ambayo baadhi ya malengo yake makuu ni utetezi wa haki za wanawake na watoto, kuongeza ushiriki wa wanawake katika uongozi, kuondoa mifumo kandamizi inayochochoea ukatili kwa makundi hayo maalum, kwa kutumia vyombo vya habari. 
Hivyo basi jukumu  la TAMWA  katika mradi huu ni kuongeza uelewa kwa umma kuhusu umuhimu wa ushiriki wa Wanawake katika siasa na katika uongozi na madhara ya magonjwa ya mlipuko kama Covid-19 kwa wanawake na wasichana.
“Katika kufanikisha lengo kuu la mradi huu, TAMWA itawajengea uwezo wanahabari  katika kuripoti habari za jinsia na ufuatiliaji wa ushiriki wa wanawake katika uongozi na siasa,Rose  Reuben, Mkurugenzi Mtendaji, TAMWA. 
Kadhalika ili kufanikisha hayo, TAMWA itaendesha midahalo ya kihabari kwa ajili ya kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu umuhimu wa ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi. 
Mikoa 16 ambayo ni Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, Mwanza, Mara, Mbeya, Ruvuma, Lindi na Mtwara, Wilaya 112 za mikoa hiyo na kata 458, ndiyo maeneo  yatakayotumika kama sampuli ya utekelezaji wa malengo ya mradi huu.
Kama ilivyoelezwa hapo juu, kuwa malengo ya mradi huu yatatimizwa kwa kutumia vyombo vya habari, hivyo basi TAMWA itashirikiana na wadau wake wakuu ambao ni vyombo vya habari, zikiwamo runinga 10, redio za kijamii 50, radio za masafa marefu 10 , magazeti 20 na mitandao ya kijamii, ili kuifikia jamii. 
TAMWA inatambua kuwa ushiriki wa wanawake katika nafasi za maamuzi (hasa ya kisiasa) bado ni mdogo, hali ambayo inakinzana na azma ya kujenga jamii isiyokuwa na ubaguzi kama ilivyobainishwa kwenye dira ya Taifa 2025, Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, pamoja na sheria mbalimbali za nchi. 
Kwa mfano, ripoti ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, (NEC: 2016) inaonyesha kuwa, asilimia 17 ya mawaziri ni wanawake, makatibu wakuu wanawake ni asilimia 11, wakuu wa mikoa ni asilimia 23, wakuu wa wilaya ni asilimia 28 na hii inaonyesha kuwa bado nafasi ya mwanamke katika ngazi za uongozi ni mdogo. 
“Hata hivyo, bado tunaupongeza  uongozi wa awamu ya tano, kwa mara ya kwanza alichaguliwa Makamu wa Rais mwanamke nchini, Mama Samia  Suluhu Hassan Reuben
Hivyo basi katika kipindi cha mwaka mmoja wa utekelezaji wa mradi huu, TAMWA, inatarajia kutumia nyenzo zake muhimu kuongeza uelewa kwa jamii na kuhakikisha wanawake wanaonekana kuwa viongozi halali na madhubuti katika jamii yetu Reuben 
Kama tulivyoainisha awali, kuwa wadau ni muhimu katika utekelezaji wa mradi huu, hivyo wadau wengine tutakaowashirikisha ni Chuo Kikuu cha Dar es Salam, kitivo cha Sayansi ya Jamii, Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Shirika la  Wanasheria Wanawake na Maendeleo Afrika, (WILDAF), Viongozi wa dini na Mtandao wa radio za kijamii nchini (TADIO), Wizara ya Habari na Wizara ya Afya.
Wengine ni Mtandao wa Wanawake Viongozi Afrika (AWLN) na machampioni wa GEWE, Viongozi wa kimila, Kituo cha Demokrasia nchini(TCD).
 Hawa wote ni wadau ambao TAMWA itafanya nao kazi wakati wa utekelezaji wa mradi huu, na kwa nafasi yao watakuwa na mengi ya kuishirikisha TAMWA na umoja huu ndicho chanzo cha mafanikio ya utekelezaji wa mradi huu, Rose Reuben
TAMWA ambayo kiini chake ni wanahabari, inatarajia kushirikiana na vyombo vya habari ili kufikisha hii ajenda ya ushiriki wa wanawake katika siasa na katika uongozi kwa jamii, tukiamini kwamba, wanawake ni nguzo muhimu katika maendeleo ya jamii. 
Viongozi wa dini, taasisi za habari, taasisi za jinsia, ambazo TAMWA inakwenda kushirikiana nazo, ni nguzo muhimu katika kufanikisha adhma kuu ya mradi huu,Reuben.
Bila kuwasahau viongozi wa kimila na viongozi wa mikoa, wilaya na kata mbalimbali ambazo tutazifikia, TAMWA inatarajia ushirikiano mkubwa kutoka kwao. 
Mkurugenzi Mtendaji 
Rose Reuben
TAMWA.
 

Search