Gallery

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na taasisi nyingine nchini kulaani vikali matukio ya mauaji ya wanawake na watoto yaliyotokea hivi karibuni hapa nchini.

Kwa kadri siku zinavyoendelea mauaji ya wanawake na watoto yanayotokana na sababu mbalimbali yameripotiwa kutokea sehemu mbalimbali hasa katika maeneo ya Njombe, Rombo, Mto wa Mbu na Simiyu. 

Pamoja na matukio ya mauaji ya watoto Njombe na Simiyu, hivi karibuni  kumetokea mauaji ya wanawake Arusha na mikoa mingine.

TAMWA tunasikitishwa na mauaji hayo na tunaikumbusha jamii kuwa kila mtu anayo haki ya kuishi kulingana na sheria na taratibu za nchi yetu. 

Hivyo tukiwa wadau wanaosimamia haki za wanawake na watoto tunakemea haya na kuwataka wadau wengine kuanzia ngazi ya familia hadi serikalini kuwalinda watoto na kuhakikisha kuwa migogoro ya kifamilia inamalizwa kwa mazungumzo ya amani. 

Tumeona na tunapongeza juhudi kubwa zilizofanywa na vyombo vya usalama nchini lakini pamoja na juhudi hizo cha kujiuliza ni kuwa kwanini bado matukio haya ya mauaji yameendelea kuripotiwasiku baada ya siku? 

Tunachelea kwamba, matukio haya yasipoundiwa mifumo ya muda mrefu ili kuyakomesha kabisa, basi tutaendelea kupoteza kinamama na watoto ambao kimsingi ni nguvu kazi ya Taifa.

TAMWA tunapendekeza uwepo wa mfumo endelevu utakaohusisha wadau mbalimbali wakiwemo wananchi, vyombo vya usalama na kampuni za simu kuwezesha waathirika kutoa taarifa za dalili zozote za ukatili kabla haujatokea. 

TAMWA tunaungana na familia za waathirika wa matukio haya tukiwatakia faraja katika kipindi hiki kigumu. 

 

Rose Reuben

Mkurugenzi Mtendaji

TAMWA

 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Aprili 6, 2019. Wanachama wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, (TAMWA), kimemchagua Joyce Shebe kuwa Mwenyekiti mpya wa bodi ya chama hicho.

 

 Katika uchaguzi huo, pia wanachama waliwachagua wajumbe wa bodi ambao ni wanahabari Leah Mushi, Raziah Mwawanga na Halima Muselem kutoka Zanzibar.

 Kabla ya Shebe, Alakok Mayombo alikuwa Mwenyekiti wa bodi ya chama hicho aliyeongoza kuanzia 2016 mpaka mwaka huu.

 Uchaguzi huo umefanyika katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika leo Aprili 6, 2019.

“Mimi si mzungumzaji  sana, mimi ni msikilizaji zaidi. Lakini ninachoweza kusema kwa sasa ni kuwa TAMWA ni wanachama. Sisi wanachama ndiyo tutakaoijenga TAMWA,”Joyce Shebe.

Shebe aliwataka wanahabari wanawake kuongeza ushirikiano kwa kuwa kwa kutumia kalamu zao wanaweza kuibadili au kuibomoa jamii.

 

Rose Reuben

Mkurugenzi Mkuu

TAMWA

Email: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it..

Mobile: 0764438084

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Mtandao wa Wadau unaopambana na unywaji pombe kupita kiasi  – TAAnet, leo tarehe 3Machi, 2018 unaungana na watanzania wote kuadhimisha siku ya kutokunywa pombe duniani ambayo kwa mara ya kwanza yanafanyika kitaifa mkoani  Dodoma.

Maadhimisho hayo yatakayoongozwa na kauli mbiu ya mwaka huu ya “Maendeleo ya Viwanda yataletwa na Udhibiti wa Unywaji Pombe kupita kiasi”  yataanza kwa maandamano yatakayopokelewa na Mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa mkoa huo Dr. Bilinith Mahenge saa mbili asubuhi kwenye viwanja vya Chuo cha Biblia Dodoma

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Watu zaidi ya milioni 3 walifariki kutokana na matumizi mabaya ya pombe mwaka 2016. Zaidi ya robo tatu ya vifo hivi vilikuwa ni vya wanaume. Kwa ujumla, matumizi mabaya ya pombe husababisha zaidi ya asilimia 5 ya mzigo wa magonjwa duniani.

Matumizi ya pombe na athari zake ni tatizo linalozidi kukua nchini Tanzania, na linapaswa kudhibitiwa haraka iwezekanavyo. Ongezeko hili la unywaji pombe katika jamii ya watanzania TAAnet inazikumbusha  taasisi husika pamoja na Serikali kuangalia kwa hakara namna ya kudhibiti tabia hiyo ili kunusuru maisha ya vijana yanayoendelea kuharibika kila siku.

Kama wadau wa kupambana na madhara ya unywaji pombe , tungependa kuona watunga sera wanalitafutia tatizo hili ufumbuzi kwa  kuwa ufumbuzi wa ubunifu ambao utaokoa maisha, kama vile kutokomeza unywaji pombe kupindukia.

Tanzania ni miongoni mwa Nchi ambazo bado haina sera/muongozo  wa pombe ukilingalinisha na Nchi jirani kama Kenya, Malawi huku Uganda wakiwa njiani kumalizia mkakati wa sera yao ya pombe.

TAAnet inapendekeza kupitiwa kwa sheria na kuweka masharti kuhusiana na matangazo, uuzaji na udhamini wa pombe pamoja na kuonyeshwa kwa onyo la athari za pombe   kwenye matangazo ya vilevi ili kupunguza matumizi yake kwa jamii.

TAAnet inaamini kwamba, endapo kutakuwa na sera ya kudhibiti matumizi mabaya ya pombe, wanaume watawajibika zaidi na kuacha matumizi yaliyopitiza ya vileo, yanayochangia unyanyasaji wa kijinsia, na badala yake kuchangia ustawi wa familia na kukuza maendeleo kwenye jamii na katika Taifa kwa ujumla.

Kupunguza matumizi mabaya ya pombe kutasaidia kufikia malengo kadhaa yanayohusiana na afya ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG), ikiwa ni pamoja na  afya ya uzazi na watoto, magonjwa ya kuambukiza, magonjwa yasiyoambukizwa na magonjwa ya akili, majeraha na sumu. 

Edda sanga

Mkurugenzi Mtendaji

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), kimewakutanisha wafanyakazi wake wapatao 26 kutoka Zanzibar na Tanzania Bara kwa lengo la kujadili kwa pamoja mpango mkakati wa mwaka mpya wa 2018.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

On 16 July, 2018,the United Nations Population Fund (UNFPA),the Delegation of the European Union (EU) to Tanzania and the East African Community (EAC), the British High Commission, the Embassy of Ireland, the Embassy of the Kingdom of the Netherlands, and the High Commission of Canada will host an event to highlight the intensified efforts that are needed to end female genital mutilation (FGM) in the country. The event will include remarks by the Government of the United Republic of Tanzania represented by the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children and the Tanzania Police Force, as well as human rights activists, and the screening of the internationally acclaimed film “In the Name of Your Daughter”, followed by a Question and Answer (Q&A) Session with the audience.

Search