- TAMWA
- Hits: 1378
An Evening with Champions Active to #EndFGM
On 16 July, 2018,the United Nations Population Fund (UNFPA),the Delegation of the European Union (EU) to Tanzania and the East African Community (EAC), the British High Commission, the Embassy of Ireland, the Embassy of the Kingdom of the Netherlands, and the High Commission of Canada will host an event to highlight the intensified efforts that are needed to end female genital mutilation (FGM) in the country. The event will include remarks by the Government of the United Republic of Tanzania represented by the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children and the Tanzania Police Force, as well as human rights activists, and the screening of the internationally acclaimed film “In the Name of Your Daughter”, followed by a Question and Answer (Q&A) Session with the audience.
- TAMWA
- Hits: 1322
TAMWA YAKEMEA MAUAJI YA WANAWAKE NA WATOTO NCHINI
Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na taasisi nyingine nchini kulaani vikali matukio ya mauaji ya wanawake na watoto yaliyotokea hivi karibuni hapa nchini.
Kwa kadri siku zinavyoendelea mauaji ya wanawake na watoto yanayotokana na sababu mbalimbali yameripotiwa kutokea sehemu mbalimbali hasa katika maeneo ya Njombe, Rombo, Mto wa Mbu na Simiyu.
Pamoja na matukio ya mauaji ya watoto Njombe na Simiyu, hivi karibuni kumetokea mauaji ya wanawake Arusha na mikoa mingine.
TAMWA tunasikitishwa na mauaji hayo na tunaikumbusha jamii kuwa kila mtu anayo haki ya kuishi kulingana na sheria na taratibu za nchi yetu.
Hivyo tukiwa wadau wanaosimamia haki za wanawake na watoto tunakemea haya na kuwataka wadau wengine kuanzia ngazi ya familia hadi serikalini kuwalinda watoto na kuhakikisha kuwa migogoro ya kifamilia inamalizwa kwa mazungumzo ya amani.
Tumeona na tunapongeza juhudi kubwa zilizofanywa na vyombo vya usalama nchini lakini pamoja na juhudi hizo cha kujiuliza ni kuwa kwanini bado matukio haya ya mauaji yameendelea kuripotiwasiku baada ya siku?
Tunachelea kwamba, matukio haya yasipoundiwa mifumo ya muda mrefu ili kuyakomesha kabisa, basi tutaendelea kupoteza kinamama na watoto ambao kimsingi ni nguvu kazi ya Taifa.
TAMWA tunapendekeza uwepo wa mfumo endelevu utakaohusisha wadau mbalimbali wakiwemo wananchi, vyombo vya usalama na kampuni za simu kuwezesha waathirika kutoa taarifa za dalili zozote za ukatili kabla haujatokea.
TAMWA tunaungana na familia za waathirika wa matukio haya tukiwatakia faraja katika kipindi hiki kigumu.
Rose Reuben
Mkurugenzi Mtendaji
TAMWA
- TAMWA
- Hits: 1369
CALL FOR CONSULTANCY SERVICES TO CONDUCT SRHR REPORTING SURVEY IN THE MEDIA OF TANZANIA
TAMWA is a non-partisan, non-profit sharing professional media membership association registered in 1987 under the society’s ordinance cap 337 of 1954 with registration number so 6763. The association also in 2004 complied with the new non-governmental organizations’ (NGO) law of 2002 with 0NGO1886 registration number. For operational purposes, TAMWA is also registered in Zanzibar under society act no 6 of 1995 with registration number 493. TAMWA has offices in Zanzibar and Dar es Salaam. TAMWA started with 12 media women, but the membership has grown to more than 160 women journalists. TAMWA has 34 years’ experience in partnership with other organizations, advocating for women and children’s rights through the use of media. TAMWA’S mission - to advocate for women and children’s rights by conducting awareness raising activities for cultural, policy and legal transformations in the society through the use of media. TAMWA visions, to havea peaceful Tanzania environment which respects human rights from a gender perspective.
The baseline survey Advancing Media advocacy to Rural and Urban Women and Girls’ SRHR in Tanzania aim at enhancing the project towards enriching media practitioners’ skills in promoting sexual and reproductive health rights outcomes in Tanzania. The project focuses on the increasing competencies of media practitioners on reporting SRHR OUTCOMES, targeting the Mainstream Media (TV, Newspapers and Radio) Community radio Online Media in order to increase the proportion of media sensitization on SRHR contents.
To come up with scientific ground of the project goals, ensure effectiveness and efficiencies of the project, TAMWA is conducting a baseline survey to inform the current SRHR media contents and the media practitioners understanding of the SRHR but also understanding best media channels for SRHR issues. The findings will enable the project team to come up with the relevant training manual or tool that will help TAMWA to build capacity, support and motivate media practitioners to cover SRHR issues including training.
- TAMWA
- Hits: 1187
TAANnet - KUADHUAMISHA SIKU YA KUTOKUNYWA POMBE DUNIANI
Mtandao wa Wadau unaopambana na unywaji pombe kupita kiasi – TAAnet, leo tarehe 3Machi, 2018 unaungana na watanzania wote kuadhimisha siku ya kutokunywa pombe duniani ambayo kwa mara ya kwanza yanafanyika kitaifa mkoani Dodoma.
Maadhimisho hayo yatakayoongozwa na kauli mbiu ya mwaka huu ya “Maendeleo ya Viwanda yataletwa na Udhibiti wa Unywaji Pombe kupita kiasi” yataanza kwa maandamano yatakayopokelewa na Mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa mkoa huo Dr. Bilinith Mahenge saa mbili asubuhi kwenye viwanja vya Chuo cha Biblia Dodoma
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Watu zaidi ya milioni 3 walifariki kutokana na matumizi mabaya ya pombe mwaka 2016. Zaidi ya robo tatu ya vifo hivi vilikuwa ni vya wanaume. Kwa ujumla, matumizi mabaya ya pombe husababisha zaidi ya asilimia 5 ya mzigo wa magonjwa duniani.
Matumizi ya pombe na athari zake ni tatizo linalozidi kukua nchini Tanzania, na linapaswa kudhibitiwa haraka iwezekanavyo. Ongezeko hili la unywaji pombe katika jamii ya watanzania TAAnet inazikumbusha taasisi husika pamoja na Serikali kuangalia kwa hakara namna ya kudhibiti tabia hiyo ili kunusuru maisha ya vijana yanayoendelea kuharibika kila siku.
Kama wadau wa kupambana na madhara ya unywaji pombe , tungependa kuona watunga sera wanalitafutia tatizo hili ufumbuzi kwa kuwa ufumbuzi wa ubunifu ambao utaokoa maisha, kama vile kutokomeza unywaji pombe kupindukia.
Tanzania ni miongoni mwa Nchi ambazo bado haina sera/muongozo wa pombe ukilingalinisha na Nchi jirani kama Kenya, Malawi huku Uganda wakiwa njiani kumalizia mkakati wa sera yao ya pombe.
TAAnet inapendekeza kupitiwa kwa sheria na kuweka masharti kuhusiana na matangazo, uuzaji na udhamini wa pombe pamoja na kuonyeshwa kwa onyo la athari za pombe kwenye matangazo ya vilevi ili kupunguza matumizi yake kwa jamii.
TAAnet inaamini kwamba, endapo kutakuwa na sera ya kudhibiti matumizi mabaya ya pombe, wanaume watawajibika zaidi na kuacha matumizi yaliyopitiza ya vileo, yanayochangia unyanyasaji wa kijinsia, na badala yake kuchangia ustawi wa familia na kukuza maendeleo kwenye jamii na katika Taifa kwa ujumla.
Kupunguza matumizi mabaya ya pombe kutasaidia kufikia malengo kadhaa yanayohusiana na afya ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG), ikiwa ni pamoja na afya ya uzazi na watoto, magonjwa ya kuambukiza, magonjwa yasiyoambukizwa na magonjwa ya akili, majeraha na sumu.
Edda sanga
Mkurugenzi Mtendaji
- TAMWA
- Hits: 1159
TAMWA YAKUTANISHA WAFANYAKAZI WAKE
Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), kimewakutanisha wafanyakazi wake wapatao 26 kutoka Zanzibar na Tanzania Bara kwa lengo la kujadili kwa pamoja mpango mkakati wa mwaka mpya wa 2018.



