Gallery

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Godwin Assenga, TAMWA.

Septemba 22, 2020. Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), Rose Reuben amewataka wanafunzi kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na kuzingatia maadili.

Reuben, ameyasema hayo hivi karibuni wakati akiwakabidhi vyeti wahitimu wa darasa la saba na kidato cha nne wa Shule ya Filbert Bayi, jijini Dar es Salaam wakati wa mahafali ya 16 ya shule hiyo.

Akiwa mgeni rasmi katika mahafali hayo, Reuben aliwaasa wanafunzi hao kuwa makini na matumizi ya teknolojia ikiwamo mitandao ya kijamii kwa kuzingatia maadili waliyofunzwa na walimu, wazazi ili wafikie ndoto zao.

"Mimi ni Mwanahabari, natambua kwamba sasa hivi teknolojia imekua kiasi kwamba kuna mitandao. Mitandaoni kuna mambo mazuri sana, lakini pia yapo mabaya. Mitandaoni kunaweza kukupoteza, mitandaoni kunaweza kukujenga,” amesema.

Amewaasa wanafunzi hao kuwa, pindi watakapoitumia mitandao hiyo wakumbuke kuzingatia maadili waliyofunzwa na wazazi pamoja na walimu wao.

"Sina namna ya kuwazuia kutumia mitandao ya kijamii kwa sababu ndiyo dunia ya sasa, lakini itumieni mkijua kwamba mnaingia mitandaoni masikio yenu na macho yenu yakiwa wazi kwamba wewe ni mtu unaetegemewa na Taifa letu, unaetegemewa na wazazi wako" amesisitiza Reuben.

Kadhalika, amewasisitiza  wanafunzi kutumia vyema vipaji maalum walivyo navyo huku akiwakumbusha kwamba kila wanachokifanya, wakifanye katika ubora huku wakitumia vyema muda wao vizuri ili kuhakikisha wanafikia malengo na ndoto zao.

Amewapongeza wazazi kwa  kujitoa vyema kimalezi na kielimu licha ya kuwepo kwa janga la Corona, lililoathiri uchumi.

Wakati huo huo, uongozi wa shule ya Filbert Bayi, ulitoa punguzo la ada la Sh500, 000 kwa wanafunzi waliohitimu darasa la saba walioamua kuendelea na kidato cha kwanza katika shule hiyo.

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active
 
BACK GROUND:
 
Tanzania Media Womens Association (TAMWA) is a non-profit, non-partisan, non-governmental and human rights organization founded and registered on 17th  November, 1987 under the Societies Ordinance Cap 337 of 1954 with registration number (SO 6763) and the Association complied with the 2002, NGO Act of the United Republic of Tanzania in 2006. 
 
ABOUT THE CALL
TAMWA under African Women Development Fund (AWDF) is looking for an experienced RADIO AND TV producer who will be responsible to produce a radio spot and or Television Spot which will highlights Challenges, success and women political inclusion landscape in Tanzania 
 
The produced spots will be aired in Televisions and Community radio based in Arusha, Dodoma, Zanzibar and Dar es Salaam. 
The documentary will showcase challenges facing women politicians during the electoral process, successes achieved in women inclusion in all aspect of politics and the current political situation towards the coming election. 
 
Activity Duties 
Gathering content for radio and /TV spot
Looking for best scene for a spot
Editing the drafts
Producing a creative audio clip of a radio spot
Producing a creative visual spot for  TV
Submit first draft of a radio/TV draft spot 
Editing and designing
 
 
Activities Time Frame
Gathering Content for radio/Tv spot should be done from August 25
Editing drafts should be done  by early September
Sharing first draft of the audio/Tv spots should be done by 5th September
Final editing should be done by 10th  September
Submitting final draft by 15th September
 
The interested consultant/company should submit the budget offer, profoma invoice and attach a sample of the previous work and/or link electronically to This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. cc This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.;  by Monday 24th August 2020, before end of business.
 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinapenda kukanusha taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zikionyesha kuwa tumelishukuru Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uamuzi wa kumchukulia hatua Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima.

Pia taarifa hizo zimekwenda mbali zaidi zikionyesha TAMWA imemtaka Askofu Gwajima kumuomba radhi Rais Samia  Suluhu na Waziri wa Afya, Doroth Gwajima kwa niaba ya wanawake wote nchini.

Tunapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa taarifa hizo ambazo zimewekwa katika nembo za vyombo vya habari kama ITV, AYO TV na katika tamko linaloonyesha kusainiwa na Mkurugenzi wa TAMWA Dkt. Rose Reuben, si za kweli. 

TAMWA haijafanya mkutano wa kihabari, haijatoa tamko wala kuzungumza na chombo chochote cha habari kuhusu sakata la Askofu Gwajima na Bunge. 

TAMWA inafanya kazi kwa kufuata maadili na taratibu za kiuandishi  na ina taratibu  zake pindi inapotakiwa kuzungumzia masuala ya jinsia, habari na afya.

Search