Gallery

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinatangaza nafasi kwa makampuni ya udalali na madalali binafsi kuuza magari yake mawili kama yanavyoonekana katika tangazo hapo chini.

 

Tafadhali tuma barua ya maombi kupitia barua pepe This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. kwa maelezo zaidi tembelea ofsi zetu au piga simu namba +255222772681 au  0719485006 au 0754462632

 

 

 

 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Florence Majani, TAMWA.

Ruangwa, Lindi. Kinamama katika kata ya Likunja, wilayani Ruangwa wamelaumiwa kuwa wao  ndicho chanzo cha kuvunjika kwa ndoa kila kukicha katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo, kasi ya wanandoa kuachana ni kubwa na hata ile ya kuoana nayo ni kubwa hasa msimu wa mavuno.

Hayo yameelezwa jana, wakati wa mafunzo ya wanakamati za ulinzi za kata hiyo, yaliyotolewa na Chama cha Wanahabari Wanawake(TAMWA) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mwalimu wa Shule ya Msingi Likunja, Maria Lilai, alisema ndoa zinavunjika kila siku kwa sababu ya mfumo wa  mwanamke kuwa na madaraka kwenye familia zaidi ya baba.

“Mfumo  wa ‘matrilinneal’ ambao unampa mama madaraka ya kuwa kichwa cha familia, ndiyo unaofanya ndoa nyingi zinavunjika. Kwa sababu wanaume wengi hawapendi kuwa chini ya mwanamke, hivyo  migogoro  mingi inaishia kwenye talaka,” alisema.

Alisema kesi zinazotolewa talaka ni za kila kukicha lakini zipo kesi ambazo wanandoa wanatengana lakini  mwanaume anakataa kutoa talaka.

“Akikataa kutoa talaka inabidi uinunue, wapo wanaume ambao hukataa kutoa talaka hadi uwape hela. Ukiwapa hela wanakupa talaka yako,” alisema.

 

Ofisa Maendeleo ya Jamii kata ya Likunja, Sarah Pongolela alisema kwa mila za Wamwera mwanaume anapooa ni lazima amjengee mke wake nyumba.

“Mara nyingi migogoro hii inaanzia kwenye mgawanyo wa mali, au pale ambapo kipato kinaongezeka,” alisema

 Alisema hakuna takwimu rasmi za matukio ya talaka kwa sababu mengi yanamalizika katika ngazi ya familia.

“Kesi nyingi zinamalizwa baada ya wanandoa kugawana mali, lakini kama kesi hiyo ina mgogoro zaidi, ndipo zinapofikishwa kwenye ofisi za kata au Bakwata au mahakamani,” alisema.

Akizungumzia kesi za talaka, Mwenyekiti wa Chama cha kinamama katika kata hiyo, Shelly Nachinuku,  alisema zipo kesi nyingi za ndoa kuvunjika lakini yeye alikuwa na maoni tofauti na Maria akidai kuwa chanzo ni wanaume.

“Kesi hizo zinaanzia kwa wanaume, mfano mwanaume akishaona amemzalisha mwanamke anamuacha, au akiona kuna watoto wengi ndani ya nyumba anamuacha na anaenda kwa mwanamke mwingine,” alisema

Alisema suala la talaka linachangiwa na wanaume kutokukaa nyumbani na kutotimiza majukumu yao  kwenye familia.

“Wanaume wanapoona msimu wa mavuno, wanazikimbia familia zao na kudai wanakwenda kuangalia mazao kumbe, wanayauza na kuanza kutumia fedha na wanawake wengine,” alisema

 Alisema hata huko shuleni imebainika kuwa wanafunzi wengi wanalelewa na mzazi mmoja au bibi  baada ya wazazi wao kuachana.

Katekisti wa Kanisa Katoliki, kigango cha Likunja, Erick Akwilambo alisema kesi hizo za wanandoa kuachana zipo nyingi katika kata hiyo na kueleza kuwa zinasababishwa na mfumo jike ambapo wanawake wanakuwa  na madaraka makubwa kwenye familia.

“Ndiyo maana hata hizi kesi za wanaume kupigwa ni nyingi, huku wanaume hawana la kusema, hata mtoto akizaliwa anakuwa ni wa ukoo wa kwa mama,” alisema

Ofisa Elimu wa Kata ya Likunja, Mwajuma Ibadi alisema sio talaka tu, bali hata ndoa nazo zinafungwa kwa wingi kama ilivyo talaka. Alisema tatizo kubwa ni kuwa wakazi wa eneo hilo wanafunga ndoa za mashindano.

“Kwa mfano, wanandoa wakiachana, basi kila mmoja atataka aoe au aoelewe tena ili kumkomoa mwenza waliyeachana,”alisema

Ibadi alisema asilimia 70 ya wanafunzi kwenye shule za msingi, wanalelewa na bibi au babu baada ya wazazi kutengana.

Alisema ndiyo maana kuna mmomonyoko wa maadili ikiwamo mimba za utotoni na elimu duni kwa kuwa watoto wengi wanakosa malezi ya wazazi wote wawili.

Mtendaji Kata ya Likunja, Hassan Kalembo alisema kesi hizo za ndoa kuvunjika zipo kwa wingi lakini hana takwimu rasmi.

“Tunapokea malalamiko hayo kila siku, lakini chanzo cha haya yote ni tamaa. Wanawake wa kabila hili(wamwera) wakiona mume amechuma mali kadhaa wanataka kuachana ili wagawane mali,” alisema.

Ofisa Maendeleo wilaya ya Ruangwa, Rashid Namkulala alisema matukio ya wazazi kutengana au kuachana ndiyo yanayosababisha malezi duni kwa watoto.

“Sisi viongozi tutaendelea kutoa elimu ya kina kwa wakazi wa eneo hili ili kesi za talaka zipungue. Tumeshuhudia kuwa watoto wanakosa malezi bora pindi tu wazazi wanapotengana,” alisema

Hata hivyo, Ofisi ya Ustawi wa Jamii ya wilaya ya Ruangwa, walisema hawana takwimu za talaka.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Call For the Consultancy Services to Conduct Survey on Current Prevalence and Mechanisms to Prevent or Deal with Sexual Harassment, Sexual Corruption and Efforts of Gender Mainstreaming in the Media of Tanzania

 

1.0 BRIEF DESCRIPTION OF TAMWA

Tanzania Media Women’s association (TAMWA) is a non-partisan, non-profit sharing professional media membership association registered in 1987 under the society’s ordinance cap 337 of 1954 with registration number so 6763. The association also in 2004 complied with the new non-governmental organizations’ (NGO) law of 2002 with 0NGO1886 registration number. Our mission is to advocate for women and children’s rights by conducting awareness raising activities for cultural, policy and legal transformations in the society through the use of media. We envision having peaceful Tanzania environment which respects human rights from a gender perspective.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Wakati dunia ikiadhimisha wiki ya Umoja wa Mataifa ya Usalama Barabarani, viongozi wa ngazi mbalimbali nchini wametakiwa kuchukua hatua katika kudhibiti ajali za barabarani ili kuokoa maisha ya wananchi yanayopotea kila kukicha kwa kusababishwa na ajali za barabarani nchini.

Wiki ya Umoja Wa Mataifa ya Usalama Barabarani ilianzishwa kupitia Azimio la Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Oktoba 2005 ikiwa na lengo la kuboresha usalama wa barabarani duniani. Azimio hili liliitaka Tume ya Umoja wa Mataifa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kuandaa kwa pamoja wiki hiyo. Kwa mara ya kwanza wiki ya umoja wa mataifa ya usalama barabarani iliazimishwa mwaka 2007 , ya pili mwaka 2013, ya tatu 2015, na ya nne 2017. Mwaka huu ni maadhirimisho ya tano, ambayo yanaadhimishwa kuanzia tarehe 6 mpaka tarehe 12 mwezi huu wa tano 2019.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Florence Majani, TAMWA.

Ruangwa. Licha ya serikali kujenga shule za kata kwa wingi ili kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari, wazazi wilayani Ruangwa, wamelalamikiwa kuwajengea watoto wao mazingira ya kufeli mitihani ya darasa la saba ili wasiendelee na shule na waolewe.

Hayo yalibainika wakati wa mdahalo kwa wanafunzi kuhusu mila na desturi zinazochochea mimba za utotoni ulioandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania(TAMWA) wilayani Ruangwa.

Kwa nyakati tofauti wanafunzi hao walisema baadhi ya  wazazi huwalazimisha watoto wao kukataa shule au kuwashauri wajifelishe mitihani ya darasa la saba ili waolewe.

“Kuna mwenzetu mmoja, alikuwa na akili sana lakini matokeo yalipotoka hakufaulu kujiunga na sekondari, tulipomuuliza kulikoni alisema mama yake alimwambia aandike 0000 ili afeli na aolewe,” alisema Zahara Chigope, Mwanafunzi wa Kidato cha nne, Sekondari ya Nambilanje.

Mwanafunzi mwingine, Nasma Kumkana, alisema suala la wazazi kuwashawishi wanafunzi wafeli kwa makusudi ni kubwa na wanalisikia kutoka kwa wanafunzi wenzao.

“Sio hivyo tu, hata baadhi ya wazazi tunawasikia wanasema bora mtoto afeli kwa sababu hawana hela za kumhudumia atakapoingia sekondari, hata wakiambiwa elimu ni bure watasema hawana fedha za sare za shule,” alisema

Nasma alisema mila hizo zinaambatana na ile ya baadhi ya wazazi kumshauri mtoto atafute mboga kwa jasho lake.

“Hii ina maana kwamba, mama anamwambia mtoto leo zamu yako kutafuta mboga, kwa maana nyingine,  mtoto wa kike anapewa ruhusa ya kuwa na mwanaume ili apate fedha ya kusaidia familia,” alisema.

Akizungumzia suala hilo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nambilanje, Charles Chitawala alisema tatizo hilo ni kubwa kwa kata ya Nambilanje na maeneo mengine ya Ruangwa.

“Sisi kama viongozi suala hilo linatuudhi, inabidi tutoe elimu, ili tabia hizo waziache. Ilifikia mahali ikabidi tuitishe vikao vya wazazi na wazazi wajaze mikataba,” alisema.

Alisema mwaka 2018, wazazi walijaza mikataba na kukubaliana kuwa iwapo mzazi atabainika kuwa alimshauri au kumlazimisha mwanafunzi kufeli kwa namna yoyote ile, basi atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mwalimu Chitawala alisema mikataba hiyo ilitolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na kusainiwa na wazazi wa wanafunzi waliomaliza darasa la saba mwaka jana.

Mratibu wa Elimu kata ya Nambilanje, Lista Mziwanda alisema suala la wazazi kuwalazimisha wanafunzi kuandika  ‘utumbo’ kwenye mitihani ya taifa lipo kwa kiasi kikubwa eneo hilo ingawa hakuna takwimu rasmi.

“Tulizibaini kesi hizo baada ya kuwabana wanafunzi ambao tuliwategemea kufaulu lakini hawakufaulu. Ukikaa na mtoto vizuri anakuambia ukweli kuwa alilazimishwa na mama,” alisema

Alisema kesi hizo ni za wanafunzi ambao walifaulu vizuri kwenye mitihani ya ndani na ile ya kujipima ‘Mock’ lakini mitihani ya taifa walifeli.

“Kinachofanyika sasa ni kutoa elimu lakini na hizo sheria ndogondogo kama kuwasainisha wazazi mikataba kuwa wakibainika kuwalazimisha watoto wafeli, watachukuliwa hatua. Tumeanza suala la mikataba mwaka jana, tutaangalia mwaka huu,”alisema.

Mwalimu Mziwanda alisema kati ya wanafunzi 76 waliomaliza darasa la saba mwaka 2018, 66 walifaulu kwenda Sekondari na wanne wamekwenda Chuo cha ufundi Nkoye.

Mmoja wa wazazi, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama ya kata, Esha Chigope, alisema kesi hizo zipo nyingi.

Esha alisema kuna mkazi mwenzao aliyefahamika kama Tendele, alikiri kumshauri mtoto wake aandike 1111, ili afeli mtihani wa darasa la saba.

“Tendele mwenyewe anasema wazi, alitaka mtoto wake afeli kwa sababu hakuna umuhimu kwa mtoto wa kike kusoma, kwa hiyo kweli mtoto akafeli,” alisema Esha.

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Hashim Mgandilu alisema watawachukulia hatua wazazi wanaorubuni wanafunzi wafeli na kusema kuwa hiyo  jamii ya wazazi inayohujumu watoto.

“Ndiyo maana tuliingia mikataba kati ya serikali na mzazi, kwamba hata mtoto akifeli, mzazi awajibike kwa kutoa maelezo kwa nini kijana amefeli,” alisema.

Alisema hali ya mwamko wa elimu kwa ukanda wa kusini hasa vijiji vya Nambilanje, Namichiga, Nachienjele na Nanjaro bado ni ndogo  na inahitajika elimu ya kutosha.

Alisema hata katika ziara zake alizofanya katika vijiji 81 vya Wilaya ya Ruangwa, alibaini suala la unyago ndilo linachochea kufifia kwa elimu wilayani humo.

“Watoto wanatolewa kupelekwa unyago kipindi cha masomo. Nilikamata wazazi waliokaidi agizo langu pamoja na watoto 22 waliokuwa wanachezwa huo unyago,”alisema Mgandilu.

Search