Gallery

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Mkurugenzi wa Chama Cha Wanahabari Wanawake (TAMWA) aliyemaliza muda wake, Edda Sanga, amepewa tuzo ya heshima ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake katika Asasi za kiraia. Tuzo hiyo imetolewa leo na Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP), wakati wa tamasha la 14 la Jinsia. 

“Nimefurahi kupokea tuzo hiyo nawashukuru sana na kuwapongeza pia wale ambao wameona nimestahili kupokea tuzo hiyo,” Amesema Edda Sanga. Pia amewataka wengine waliopata tuzo hiyo kuendeleza mapambano ya kumkomboa mtoto wa kike, kumlinda na kumpa haki yake.

TAMWA tunampongeza Edda Sanga kwa kutwaa tuzo hii adhimu na pia tunawapongeza TGNP Mtandao kwa kuona umuhimu wa kuandaa tuzo hizi.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

March 27,2015

Zaidi ya Wanachama 100 wa Chama cha Wanahabari Wanawake nchini- TAMWA Jumamosi tarehe 28th Machi, 2015 wanafanya Mkutano wake Mkuu wa mwaka 2014 ambapo pamoja na mambo mengine wanachama watapata fursa ya  kutathmini kazi zilizofanyika  mwaka 2014, na utekelezaji wa mpango mkakati wa 2015-2021. Mkutano huo utaanza saa 2:00 asubuhi katika ofisi za chama zilizoko Sinza Mori, Dar es Salaam.

Mkutano huo ulianza na mafunzo Ijumaa tarehe 27th Machi mwaka huu na kuwapa fursa wanachama kujadili mafanikio yaliyopatikana kwenye mpango mkakati wa miaka mitano iliyopita (2009 -2014) pamoja na changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji ambapo pia watamchagua Mwenyekiti mpya baada ya aliyekuwepo kumaliza muda wake.

Aidha baada ya mkutano huo wanachama watajumuika pamoja katika hafla ya kuchangia mfuko wa shughuli za TAMWA (Gala Dinner) ambazo ni pamoja na kupiga vita vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto itakayofanyika jioni katika hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam.

Mkutano mkuu wa TAMWA ndicho chombo cha juu chenye mamlaka ya kurekebisha katiba yake, kuingiza wanachama wapya, kuchagua viongozi, kupitisha ripoti za mwaka na kutoa maamuzi kuhusu mipango na mikakati ya chama kuhusu utetezi.

March 08,2015

Every year March 08, the whole world celebrates women’s day around the world. TAMWA as the largest shareholder of women and children rights has been the forefront duting celebration. TAMWA made various exhibitions as well as provided legal support and advice, in the event the special guest was the president of the Republic of Tanzania honorable Jakaya Mrisho Kikwete accompanied by the Minister of Social Welfare Gender and Children honorable Sophia Simba with his deputy, Hon Pindi Chana. TAMWA received two awards that are awareness of gender issues and fight-FGM as well as early marriage. The slogan was ''uwezeshaji wa wanawake tekeleza wakati ni sasa"

February 24,2015

High Commission of Canada honors advocate working to end child marriage

The High Commission of Canada presented an award today to honor a Tanzanian who has made a distinguished contribution to the effort to end child, early, and forced marriage (CEFM).

The High Commissioner of Canada, H.E. Alexandre Lévêque, presented the award to Ms. Valerie Msoka, at a ceremony this afternoon at the Serena Hotel in Dar es Salaam.

 The Permanent Secretary for Community Development, Gender, and Children (MCDGC), Ms. Anna Maembe, represented the Government of Tanzania at the ceremony.  Among those in attendance were many of the leaders in the fight against child marriage in Tanzania, along with development partners from UN agencies and foreign diplomatic missions.

Ms. Msoka will carry the title of Champion for CEFM for 2015.  As CEFM Champion, Ms. Msoka will take part in a range of outreach activities across Tanzania over the next year.  She will travel to Canada, to meet Canadian government officials and civil society representatives supporting the fight to end CEFM.

High Commissioner Lévêque applauded the tireless efforts of the scores of women and men working to end CEFM.  He said today’s award is designed to highlight the need for advocacy.

“The girls and women who have borne the burden of child, early, and forced marriage need to have their stories told,” said High Commissioner Lévêque.  “Here, and around the world, these girls and women need an advocate:  a champion who can tell their stories, and help bring people together to change things for the better.  Valerie Msoka will be that advocate.  I am proud to name her the High Commission of Canada’s CEFM Champion for Tanzania.”

The High Commissioner said Ms. Msoka’s work will support the efforts by Tanzania’s government, civil society, UN Women, the UNFPA, and development partners.

February 24,2015

Mafunzo kwa Waandishi wa Habari:
Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania-TAMWA kwa kushirikian na Shirika linalo hudumia Idadi ya Watu UNFPA Kinatoa mafunzo ya siku tatu kuhusiana na kuandika habari za uchunguzi wa unyanyasaji wa kijinsia.Mafunzo hayo yanaendelea kutolewa kwa waandishi wa habari mapema tarehe 23 hadi Tarehe 25 Februari mwaka huu katika kanda tatu nchini Tanzania.
Mafunzo katika kanda ya Kaskazini yatajumuisha mikoa ya Arusha, Manyara Tanga na Kilimanjaro na yatafanyika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro. Katika Kanda ya Kati, waandishi wa habari watatoka mikoa ya Dodoma, Morogoro, Singida na Tabora ambapo mafunzo yatafanyika mjini Singida. Mafunzo katika Nyanda za Juu Kusini yatajumuisha mikoa ya Iringa, Mbeya, Njombe na Ruvuma na yatafanyika mjini Iringa

February 10,2015

Commemoration Zero Tolerance of the FGM

The Minister of Community Development, Gender and Children (MCDGC) Hon. Sophia Simba on 10th February signed the Girl Summit Charter on behalf of the Government of Tanzania as part of the 2015 Zero Tolerance of the FGM day commemoration.

The event by the MCDGC follows the June 2014 Girl Summit held in London, as well Tanzania’s effort to end FGM and child marriage. Notably, the National FGM Forum held 6 and 7 February 2015 in Singida by MCDGC, TAMWA and UNFPA, as well as the launch of the national campaign against child marriage entitled Child Marriage-Free Zone in August 2014. All these events have highlighted that ending child marriage and FGM are national priorities.

 

During the signing Minister Sophia Simba emphasized that, "the government of the United Republic of Tanzania is fully committed to ensure that FGM comes to an end so that our girls can enjoy their happy life free from lifelong psychological and health stress which the cut girls endure. Also as a country, we will ensure that no girl will be married before eighteen especially after our new 2014 proposed constitution is approved and all discriminatory laws are repealed. I urge all ministries and agencies, CSOs and other stakeholders including politicians to make ending FGM and child marriage their priority agenda".

Speaking at the signing event, Dr. Natalia Kanem the UNFPA Representative noted that: “The momentum is building! We already have so much evidence of the fact that the public opinion in Tanzania is against child marriage, and FGM is against the law. The young women and men in Tanzania are counting on future leaders to bravely stand up for what is right. With strong leadership eradicating the practices can be achieved in just a short few years.”

The British High Commissioner to Tanzania, Ms. Dianna Melrose, welcomed the signing and noted that: “The Girl Summit has achieved unprecedented levels of public engagement and support to end child marriage and FGM, it is great to see Tanzania adding its voice to these efforts and reinforcing the message that FGM and child marriage are not acceptable in any part of this country.  Working together we can bring an end to these practices and ensure that all Tanzanian girls are able to fulfill their full potential free from violence.”

Tanzania has one of the highest child marriage prevalence rates in the world; almost two out of five Tanzanian girls will be married before their 18th birthday. While the FGM practice continues notably in Manyara, Arusha, Dodoma, Singida and Mara regions.

 

December 03,2014

Launch of Campaign Against Sextortion

A nationwide campaign to end sexual exploitation was launched in Dar es Salaam as part of the activities to mark the 16 Days of Activism against GBV.

Launching the campaign in Dar es Salaam, the Tanzania Vice President's wife, Mama Asha Bilal, called upon victims of ‘sextortion’ to come forward and report to responsible authorities reminding them that silence fuels the illegal practice.

Sextortion which is a combination of words sex and extortion is a form of GBV that employs non-physical forms of coercion to extort sexual favours from the victim.

Mama Bilal told the audience at the Leaders’s Club grounds that sextortion is a form of corruption where people in positions of authority such as government officials, teachers, doctors and law enforcement personnel seek sexual favours in exchange for a service that is within their authority to grant or withhold.

She said that the campaign aims at fighting against sexual abuse at the workplace and in schools and institutions of higher education.

The Coalition against Sextortion (CAS), formed in May 2014, is chaired by the Tanzania Women Judges Association(TAWJA) and co-chaired by the Women Fund Tanzania(WFT) and brings together a number of Human and Women and Children Rights organizations such as TAMWA,TGNP, TAWLA, WLAC and TUCTA with the objective of breaking the silence on sextortion through awareness raising and evidence based advocacy

The co-chairperson of CAS Ruth Meena said the campaign will bring to light the suffering brought on by sexual harassment both in terms of emotional abuse and in the lack of concern by judiciary.

The Tanzania Media Women Association (Tamwa) reports that an estimated 75 to 89 per cent of women in Tanzania have experienced some form of sexual harassment.

 

November 25,2014

16 Days of Gender Activism

 The 16 Days of Activism Against Gender Violence is an international campaign that starts on 25 November, International Day for the Elimination of Violence against Women and ends on 10 December, Human Rights Day. The campaign hopes to raise awareness about gender-based violence as a human rights issue at the local, national, regional and international level. This year’s theme is ”Let’s challenge militarism and end violence against women”

TAMWA has seen the need of training 30 Photojournalists with Interest of vanishing gender based violence. This Training of 30 photo journalists from different regions in Tanzania is going along with the 16 Days of Gender Activism and also exhibiting photos that have a theme of gender violence. The photo exhibition is taking place in the National Museum with duration of two days 25th and 26th of Nov 2014.

The main objective of TAMWA is to convey information by the use of picture. It is widely known that a well taken photo speaks thousand words so every picture will transmit different messages.

November 20,2014

9TH AFRICA REGIONAL CONFERENCE ON THE 20 YEAR REVIEW OF THE BEIJING DECLARATION AND PLATFORM FOR ACTION

 

Press Release: Governments Must Re-Dedicate to Women’s & Girls’ Rights Commitments.

August 26,2014

The National Ending Child Marriage Campaign launched in Dar es Salaam

Graça Machel speaking at the launch of the National Ending Child Marriage campaign in Dar es Salaam

The Ministry of Community Development, Gender and Children in collaboration with the United Nations Population Fund (UNFPA), Tanzania Media Women’s Association (TAMWA), Graça Machel Trust (GMT), Children’s Dignity Forum (CDF) and the Tanzania Ending Child Marriage Network (TECMN) launched a National Ending Child Marriage campaign branded “Child Marriage Free Zone”.

The campaign is aimed at strengthening national dynamics for ending child marriage and ensuring that girls in the country get their rights.

Graca Machel, founder of the Graca Machel Trust, launched the campaign and said the fact that Tanzania was in the frontline in the African liberation against colonialists, it should also take the lead in the fight against gender violence.

She said the on-going constitutional making in Tanzania is an opportunity to review and redress oppressive laws on women and children.

She called for better strategies in devising the type of messages and activities that are used in the fight against child marriage saying communities are not homogenous and that what might work in Mwanza will not necessarily work in Iringa.

Ms Machel added that for a long time the focus has been on the community as a whole while ignoring the fact that it is the mother and father who play an important role in child marriage process.

Retired, Third phase President, Benjamin Mkapa   who was also in attendance said girls have constitutional rights that ought to be protected and that leaders must respect and observe girls’ rights.

The Minister of Community Development, Gender and Children Minister, Sophia Simba welcomed participants to the launch and said that child marriage is a cross cutting issue and  the government in its efforts to fight child marriage the has been implementing the Maputo Protocol which recognizes a child as a person who is below 18 years.

MS Simba added that the government has put in place numerous initiatives to save girls and women including the 2015 vision that incorporated gender equality as a national priority issue. Others are the child the policy of 2009 and Sexual Offences Special Provision Act (SOSPA) of 1998.

The campaign will initially focus on Tarime district, Mara region and the experience gained will be used in the fight against child marriage in Tanzania.

Tanzania is among 20 leading countries in child marriage cases with statistics showing that for every five girls, two are married under the age of 18.

Ending Child Marriage is among  TAMWA’s strategies against Gender Based Violence.

 

March 28, 2014

TAMWA ANNUAL GENERAL MEETING HELD AT TAMWA RESOURCE CENTRE

 Members of the Tanzania Media Women’s Association- TAMWA today 28th March, 2014 begun its Annual General Meeting- (AGM), which among other things they had  an opportunity to discuss the implementation of its Strategic Plan for the next five years from 2015 to 2021.

 The meeting which took place at its office in Sinza Mori Dar es Salaam, reviewed the progress made in the past five years from 2009-2014 as well as the challenges faced in the implementation of the Strategic Plan ending in 2014.

Every TAMWA member was provided with 2009-2014 Strategic plan Evaluation form to fill their views on the performance, success and challenges encountered during 2009-2014 Strategic plan implementation over past six years.

Also they had an opportunity to go through new TAMWA strategic plan development processes to prepare themselves for the actual TAMWA Strategic plan for 2015-2021 development scheduled to commence in June 2014.

TAMWA Annual General Meeting is the highest organ body which makes the final decisions of the organisation which includes operational planning and approval of its Annual Report.

March 08,2014

TAMWA AND INTERNATIONAL WOMEN’S DAY 2014

As the world marks international women’s day, The Tanzania Media Women’s Association (TAMWA) also reflects on its journey in bringing the issues of Women onto the national agenda.

The International Women's Day is traditionally a day when women of the world unite to celebrate achievements and protest injustices against women. The day celebrates the social, political and economic achievements of women while focusing world attention on areas requiring further action to achieve equality for women.

For TAMWA, each year marks a step against inequality which started in 1987 when twelve women journalists who strongly opposed the way media portrayed women and the way women were treated in the media houses, joined hands to remedy the situation.

Through the years, the realization grew that it was not only media women who were discriminated, undermined, under-represented and sexually harassed, it was in every sphere of society. So, TAMWA joined the national and international fight for against injustices and for gender equality.

Today the organization has grown to more than 100 members and TAMWA continues to educate, raise awareness and facilitate both women and men on their rights, especially those of women and the girl child.

TAMWA does this through its media advocacy because it believes that the media plays a crucial role in changing people’s attitudes. By working closely with media houses, editors and journalists through meetings and trainings, TAMWA has contributed variously to the transformation of the Tanzania society.

Over the last 20 years, through the use of media, TAMWA has succeeded in creating and intensifying awareness and mobilising for action on issues related to gender-based violence such as wife battery, killing of elderly women due to witchcraft beliefs, rape, FGM, child marriage, early pregnancies, women visibility in decision making as well as alleviating poverty amongst women. The struggle for women special seats went hand in hand with the enactment of the popular law on sexual harassment namely the Sexual Offences Special provision Act (SOSPA) of 1998 for which TAMWA was instrumental.

Each year, TAMWA uses the International Women’s Day to highlight issues that need action and celebrate what has been achieved. And this year’s theme "Inspiring change" amply reflects what TAMWA has done through the years - the growing awareness of the need for women's equal participation at all levels and every sphere of the society as well as a united voice against gender based violence.

For years, TAMWA has been celebrating the International Women’s Day by participating in number of TV and radio programmes, exhibition, presentations and articles in the print media all aimed at creating awareness to the Tanzanian society including policy makers on the need to change the policies that undermine women in the country.

In 2014, TAMWA celebrates the 200 journalists trained in the past year on reporting GBV and gender sensitive reporting, the 400 girls who ran away from undergoing FGM, of the men who take up action against women and children being abused, the families it has reconciled and cases it has assisted through its Crisis Resolving Centre.

Most importantly, TAMWA celebrates the fact that through its media advocacy women have participated in the historic constitutional making process and that the Constitutional Assembly includes 100 women and 101 men from Civil Society Organisations, learning institutions and religious bodies. It is a gain against inequality worth celebrating.

 TAMWA in collaboration with Gender Equality and Women Empowerment GEWE II: GBV Component partners have met with Tanzania Mainland Editors today, 31st August 2013 at TAMWA Resource Centre, Sinza Mori to launch Journalist Guide to GBV reporting.

TAMWA has also urged editors to support TAMWA campaign against gender based violence cases in Tanzania that has largely affected Women and Children.

The manual will guide journalists in the investigation GBV cases and best ways to report GBV issues/cases affecting women and children.

 Click here to Download your English and Swahili copies

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Florence Majani, TAMWA.

Ruangwa. Licha ya serikali kujenga shule za kata kwa wingi ili kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari, wazazi wilayani Ruangwa, wamelalamikiwa kuwajengea watoto wao mazingira ya kufeli mitihani ya darasa la saba ili wasiendelee na shule na waolewe.

Hayo yalibainika wakati wa mdahalo kwa wanafunzi kuhusu mila na desturi zinazochochea mimba za utotoni ulioandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania(TAMWA) wilayani Ruangwa.

Kwa nyakati tofauti wanafunzi hao walisema baadhi ya  wazazi huwalazimisha watoto wao kukataa shule au kuwashauri wajifelishe mitihani ya darasa la saba ili waolewe.

“Kuna mwenzetu mmoja, alikuwa na akili sana lakini matokeo yalipotoka hakufaulu kujiunga na sekondari, tulipomuuliza kulikoni alisema mama yake alimwambia aandike 0000 ili afeli na aolewe,” alisema Zahara Chigope, Mwanafunzi wa Kidato cha nne, Sekondari ya Nambilanje.

Mwanafunzi mwingine, Nasma Kumkana, alisema suala la wazazi kuwashawishi wanafunzi wafeli kwa makusudi ni kubwa na wanalisikia kutoka kwa wanafunzi wenzao.

“Sio hivyo tu, hata baadhi ya wazazi tunawasikia wanasema bora mtoto afeli kwa sababu hawana hela za kumhudumia atakapoingia sekondari, hata wakiambiwa elimu ni bure watasema hawana fedha za sare za shule,” alisema

Nasma alisema mila hizo zinaambatana na ile ya baadhi ya wazazi kumshauri mtoto atafute mboga kwa jasho lake.

“Hii ina maana kwamba, mama anamwambia mtoto leo zamu yako kutafuta mboga, kwa maana nyingine,  mtoto wa kike anapewa ruhusa ya kuwa na mwanaume ili apate fedha ya kusaidia familia,” alisema.

Akizungumzia suala hilo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nambilanje, Charles Chitawala alisema tatizo hilo ni kubwa kwa kata ya Nambilanje na maeneo mengine ya Ruangwa.

“Sisi kama viongozi suala hilo linatuudhi, inabidi tutoe elimu, ili tabia hizo waziache. Ilifikia mahali ikabidi tuitishe vikao vya wazazi na wazazi wajaze mikataba,” alisema.

Alisema mwaka 2018, wazazi walijaza mikataba na kukubaliana kuwa iwapo mzazi atabainika kuwa alimshauri au kumlazimisha mwanafunzi kufeli kwa namna yoyote ile, basi atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mwalimu Chitawala alisema mikataba hiyo ilitolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na kusainiwa na wazazi wa wanafunzi waliomaliza darasa la saba mwaka jana.

Mratibu wa Elimu kata ya Nambilanje, Lista Mziwanda alisema suala la wazazi kuwalazimisha wanafunzi kuandika  ‘utumbo’ kwenye mitihani ya taifa lipo kwa kiasi kikubwa eneo hilo ingawa hakuna takwimu rasmi.

“Tulizibaini kesi hizo baada ya kuwabana wanafunzi ambao tuliwategemea kufaulu lakini hawakufaulu. Ukikaa na mtoto vizuri anakuambia ukweli kuwa alilazimishwa na mama,” alisema

Alisema kesi hizo ni za wanafunzi ambao walifaulu vizuri kwenye mitihani ya ndani na ile ya kujipima ‘Mock’ lakini mitihani ya taifa walifeli.

“Kinachofanyika sasa ni kutoa elimu lakini na hizo sheria ndogondogo kama kuwasainisha wazazi mikataba kuwa wakibainika kuwalazimisha watoto wafeli, watachukuliwa hatua. Tumeanza suala la mikataba mwaka jana, tutaangalia mwaka huu,”alisema.

Mwalimu Mziwanda alisema kati ya wanafunzi 76 waliomaliza darasa la saba mwaka 2018, 66 walifaulu kwenda Sekondari na wanne wamekwenda Chuo cha ufundi Nkoye.

Mmoja wa wazazi, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama ya kata, Esha Chigope, alisema kesi hizo zipo nyingi.

Esha alisema kuna mkazi mwenzao aliyefahamika kama Tendele, alikiri kumshauri mtoto wake aandike 1111, ili afeli mtihani wa darasa la saba.

“Tendele mwenyewe anasema wazi, alitaka mtoto wake afeli kwa sababu hakuna umuhimu kwa mtoto wa kike kusoma, kwa hiyo kweli mtoto akafeli,” alisema Esha.

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Hashim Mgandilu alisema watawachukulia hatua wazazi wanaorubuni wanafunzi wafeli na kusema kuwa hiyo  jamii ya wazazi inayohujumu watoto.

“Ndiyo maana tuliingia mikataba kati ya serikali na mzazi, kwamba hata mtoto akifeli, mzazi awajibike kwa kutoa maelezo kwa nini kijana amefeli,” alisema.

Alisema hali ya mwamko wa elimu kwa ukanda wa kusini hasa vijiji vya Nambilanje, Namichiga, Nachienjele na Nanjaro bado ni ndogo  na inahitajika elimu ya kutosha.

Alisema hata katika ziara zake alizofanya katika vijiji 81 vya Wilaya ya Ruangwa, alibaini suala la unyago ndilo linachochea kufifia kwa elimu wilayani humo.

“Watoto wanatolewa kupelekwa unyago kipindi cha masomo. Nilikamata wazazi waliokaidi agizo langu pamoja na watoto 22 waliokuwa wanachezwa huo unyago,”alisema Mgandilu.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Call For the Consultancy Services to Conduct Survey on Current Prevalence and Mechanisms to Prevent or Deal with Sexual Harassment, Sexual Corruption and Efforts of Gender Mainstreaming in the Media of Tanzania

 

1.0 BRIEF DESCRIPTION OF TAMWA

Tanzania Media Women’s association (TAMWA) is a non-partisan, non-profit sharing professional media membership association registered in 1987 under the society’s ordinance cap 337 of 1954 with registration number so 6763. The association also in 2004 complied with the new non-governmental organizations’ (NGO) law of 2002 with 0NGO1886 registration number. Our mission is to advocate for women and children’s rights by conducting awareness raising activities for cultural, policy and legal transformations in the society through the use of media. We envision having peaceful Tanzania environment which respects human rights from a gender perspective.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Florence Majani, TAMWA.

Ruangwa, Lindi. Kinamama katika kata ya Likunja, wilayani Ruangwa wamelaumiwa kuwa wao  ndicho chanzo cha kuvunjika kwa ndoa kila kukicha katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo, kasi ya wanandoa kuachana ni kubwa na hata ile ya kuoana nayo ni kubwa hasa msimu wa mavuno.

Hayo yameelezwa jana, wakati wa mafunzo ya wanakamati za ulinzi za kata hiyo, yaliyotolewa na Chama cha Wanahabari Wanawake(TAMWA) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mwalimu wa Shule ya Msingi Likunja, Maria Lilai, alisema ndoa zinavunjika kila siku kwa sababu ya mfumo wa  mwanamke kuwa na madaraka kwenye familia zaidi ya baba.

“Mfumo  wa ‘matrilinneal’ ambao unampa mama madaraka ya kuwa kichwa cha familia, ndiyo unaofanya ndoa nyingi zinavunjika. Kwa sababu wanaume wengi hawapendi kuwa chini ya mwanamke, hivyo  migogoro  mingi inaishia kwenye talaka,” alisema.

Alisema kesi zinazotolewa talaka ni za kila kukicha lakini zipo kesi ambazo wanandoa wanatengana lakini  mwanaume anakataa kutoa talaka.

“Akikataa kutoa talaka inabidi uinunue, wapo wanaume ambao hukataa kutoa talaka hadi uwape hela. Ukiwapa hela wanakupa talaka yako,” alisema.

 

Ofisa Maendeleo ya Jamii kata ya Likunja, Sarah Pongolela alisema kwa mila za Wamwera mwanaume anapooa ni lazima amjengee mke wake nyumba.

“Mara nyingi migogoro hii inaanzia kwenye mgawanyo wa mali, au pale ambapo kipato kinaongezeka,” alisema

 Alisema hakuna takwimu rasmi za matukio ya talaka kwa sababu mengi yanamalizika katika ngazi ya familia.

“Kesi nyingi zinamalizwa baada ya wanandoa kugawana mali, lakini kama kesi hiyo ina mgogoro zaidi, ndipo zinapofikishwa kwenye ofisi za kata au Bakwata au mahakamani,” alisema.

Akizungumzia kesi za talaka, Mwenyekiti wa Chama cha kinamama katika kata hiyo, Shelly Nachinuku,  alisema zipo kesi nyingi za ndoa kuvunjika lakini yeye alikuwa na maoni tofauti na Maria akidai kuwa chanzo ni wanaume.

“Kesi hizo zinaanzia kwa wanaume, mfano mwanaume akishaona amemzalisha mwanamke anamuacha, au akiona kuna watoto wengi ndani ya nyumba anamuacha na anaenda kwa mwanamke mwingine,” alisema

Alisema suala la talaka linachangiwa na wanaume kutokukaa nyumbani na kutotimiza majukumu yao  kwenye familia.

“Wanaume wanapoona msimu wa mavuno, wanazikimbia familia zao na kudai wanakwenda kuangalia mazao kumbe, wanayauza na kuanza kutumia fedha na wanawake wengine,” alisema

 Alisema hata huko shuleni imebainika kuwa wanafunzi wengi wanalelewa na mzazi mmoja au bibi  baada ya wazazi wao kuachana.

Katekisti wa Kanisa Katoliki, kigango cha Likunja, Erick Akwilambo alisema kesi hizo za wanandoa kuachana zipo nyingi katika kata hiyo na kueleza kuwa zinasababishwa na mfumo jike ambapo wanawake wanakuwa  na madaraka makubwa kwenye familia.

“Ndiyo maana hata hizi kesi za wanaume kupigwa ni nyingi, huku wanaume hawana la kusema, hata mtoto akizaliwa anakuwa ni wa ukoo wa kwa mama,” alisema

Ofisa Elimu wa Kata ya Likunja, Mwajuma Ibadi alisema sio talaka tu, bali hata ndoa nazo zinafungwa kwa wingi kama ilivyo talaka. Alisema tatizo kubwa ni kuwa wakazi wa eneo hilo wanafunga ndoa za mashindano.

“Kwa mfano, wanandoa wakiachana, basi kila mmoja atataka aoe au aoelewe tena ili kumkomoa mwenza waliyeachana,”alisema

Ibadi alisema asilimia 70 ya wanafunzi kwenye shule za msingi, wanalelewa na bibi au babu baada ya wazazi kutengana.

Alisema ndiyo maana kuna mmomonyoko wa maadili ikiwamo mimba za utotoni na elimu duni kwa kuwa watoto wengi wanakosa malezi ya wazazi wote wawili.

Mtendaji Kata ya Likunja, Hassan Kalembo alisema kesi hizo za ndoa kuvunjika zipo kwa wingi lakini hana takwimu rasmi.

“Tunapokea malalamiko hayo kila siku, lakini chanzo cha haya yote ni tamaa. Wanawake wa kabila hili(wamwera) wakiona mume amechuma mali kadhaa wanataka kuachana ili wagawane mali,” alisema.

Ofisa Maendeleo wilaya ya Ruangwa, Rashid Namkulala alisema matukio ya wazazi kutengana au kuachana ndiyo yanayosababisha malezi duni kwa watoto.

“Sisi viongozi tutaendelea kutoa elimu ya kina kwa wakazi wa eneo hili ili kesi za talaka zipungue. Tumeshuhudia kuwa watoto wanakosa malezi bora pindi tu wazazi wanapotengana,” alisema

Hata hivyo, Ofisi ya Ustawi wa Jamii ya wilaya ya Ruangwa, walisema hawana takwimu za talaka.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinatangaza nafasi kwa makampuni ya udalali na madalali binafsi kuuza magari yake mawili kama yanavyoonekana katika tangazo hapo chini.

 

Tafadhali tuma barua ya maombi kupitia barua pepe This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. kwa maelezo zaidi tembelea ofsi zetu au piga simu namba +255222772681 au  0719485006 au 0754462632

 

 

 

 

Search