Gallery

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active
June 10th, 2022, Dar es Salaam. The Tanzania Media Womens Association (TAMWA) calls on the Tanzanian government to continue to use the negotiation, and reconciliation process and to follow the procedures for the transfer of land and national resources.
 
The request comes after reports from June 8, 9 and today 10, 2022, showing pastoralists of the Loliondo Maasai tribe and army forces protesting the implementation of the border marking of 1500 square kilometers of their villages for natural resource conservation trending in social media. 
 
We understand and agree with the Prime Minister Kassimu Majaliwa that the loss of peace in any area is causing inconvenience to women, the elderly and children and therefore calls on the government to return to the negotiating table to end the Loliondo conservation crisis with the Maasai community.
 
TAMWA have witnessed many conflicts being resolved through dialogue and reconciliation in this country so we believe that even this conflict can also be resolved without resorting to force or inciting violence that is smearing the nation with human rights abuses.
 
Dr Rose Reuben,
 
 
Executive Director
 
TAMWA

User Rating: 4 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Inactive

Novemba 25, 2024.Dar es Salaam.Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na watanzania, wadau wa maendeleo, mashirika yasiyo ya kiserikali na watanzania kwa ujumla katika kuadhimisha Siku 16 za Ukatili wa Kijinsia.

Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zina adhma ya kukumbusha jamii kuhusu mienendo na mitazamo inayochagiza vipigo, ukeketaji, ubakaji, ulawiti, mimba za utotoni na rushwa ya ngono katika jamii. 

Kadhalika,siku hizi 16 zinatumika kutafakari kwa Pamojani wapi tulipofanikiwa, wapi penye mapengo nnikwa namna gani tutayaziba mapengo yaliyopo katika kupunguza ukatili wa kijinsia. 

Kauli mbiu ya maadhimisho haya kwa mwaka huu ni: Kuelekea miaka 30+ ya Beijing: Tuungane kumaliza ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto

Kauli mbiu hii inalenga kuwakumbusha viongozi, wanaharakati na wadau wa masuala ya ukatili wa kijinsia hasa serikali, sekta binafsi na kampuni kuchukua hatua ili kumaliza ukatili huu.

Kama dhima ya mkutano wa Beijing, ilivyokuwa, kadhalika TAMWA kwa miaka 37 sasa kimebeba ajenda ya kumaliza ukatili wa kijinsia katika Nyanjazote, nakatika msimu huu bado kinaikumbusha jamii kuondokana na dhana potofu zote zinazomdunishakumnyima fursa , kumuharibia utu na kumwondolea staha, na wakati mwingine kusababisha ulemavu nhatakifo mwanamke na mtoto wa kike

Dhana hizo ni Pamojana mwanamke hawezi kuwa kiongozi, mtoto wa kike hana haja ya kupata elimu, ukeketaji, ubakaji na ulawiti.

Katika miaka 37 ya kufanya kazi katika eneo hili, tumeona mafanikioambayo kwa kushirikiana na serikali, tumeweza kupiga hatua na sauti zikasikika kuhusu nafasi ya mwanamke katika jamii,” Dr Rose Reuben, Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA.

Tumefanikiwa kupata sheria ya makosa ya kujamiiana ya SOSPA na tumefanikisha kuingizwa kwa kipengele cha rushwa ya ngono katika sheria ya rushwa. 

“Haya ni mafanikio ambayo tunajivunia katika miaka hii 37 ya uwepo wa TAMWA” Dr Rose

Hata hivyo bado kuna changamoto zinazoibuka ambazo zinachagizwa na kukua kwa teknolojia, sisi tumeona ongezeko kubwa la unyanyasaji wa kijinsia kwa njia ya mitandao ya kijamii.

Matumizi ya mitandao ya kijamii licha ya kuwa yameleta maendeleo lakini wanawake wamekuwa wakiathiriwa na mitandao hiyo kwa picha zao kusambazwa, au picha mjongezinazowadhalilisha zikisambazwa.

“Tumepata kesi kadhaa za Watotowa kike kutishiwa kutoa kiasi cha fedha kwa sababu wenza wao waliwarekodi picha za utuputunapokea kesi ambapo wanawake wanabakwa na kisha kupigwa picha zinazosambazwa mitandaoni,” Dr Rose 

Pamoja na hayo, kadhalika tumeona wanawake wanasiasa wakidhalilishwa mitandaoni hali inayochagiza kuacha kushiriki katika siasa au kuacha kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwenye jamii.

Hivyo basi TAMWA, katika kipindi hiki cha Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia, tunakemea udhalilishaji wa wanawake kwa kutumia mitandao ya kijamii

Tunawahimiza wanawake na Watotowa kike,wasiogope kutoa taarifa kwa mamlaka husika ikiwamo TAMWA, ambayo chini ya kitengo cha Usuluhisi wa Migogoro, (CRC) imekuwa ikisaidia wanawake/Watotowa kike wanaokumbana na udhalilishaji wa ain azote.

CRC itasikiliza kesi yako kwa hali ya faragha na kutoa msaada wa kisheria ili mwathirika apate haki yake” Dk Rose Reuben. 

TAMWA inatathmini miaka yake 37 ya harakati za kumaliza ukatili wa kijinsia katika mifumo yote na hata sasa inaendelea kuihimiza jamii kutathminimiaka 30 ya mkutano wa Beijing, kwa kuangazia nafasi ya wanawake wanasiasa, wanahabari na wanawake wote ambao wamekuwa walengwa katika ukatili wa kijinsia kwa njia ya mtandao. 

Kwa kuwa kauli mbiu ya mwaka huu ina neno ‘Kuungana’ hivyo basi TAMWA tunahimiza  tuungane, wanaofanya ukatili huo wachukuliwe hatua bila kujali nafasi zao, ikiwezekana mikakati ya kitaifa ifanyike kuwasaidia wanawake na Watotowa kike wanaodhalilishwa mitandaoni

TAMWA inawaita wanawake na Watotowa kike wanaokumbana na ukatili mtandaoni na ukatili mwingine wowote, kuwasiliana kwa namba:  au kufika ofisi za TAMWA, Sinza, Mori kuanzia leo Novemba 25 hadi Desemba 10, kupata msaada wa kisheria bure. 

Mkurugenzi Mtendaji

DkRose Reuben

TAMWA

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na mashirika mbalimbali dunianikuadhimisha Siku ya Haki za Binadamuyenye kauli mbiu Haki Zetu, Mustakabali WetuHatma Yetu, NSasa” (Our Rights, Our Future, Right Now) kwa kuzingatia maadili, kujali usawa na kulinda haki za wanawake na watoto kwa maendeleo endelevu.

Katika maadhimisho hayo leo ndio kilele cha kampeni ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia Duniani yenye Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inasema, “Kuelekea Miaka 30+ ya Beijing: Tuungane Kumaliza Ukatili wa Kijinsia kwa Wanawake na Watoto.”

Ni umuhimu jamii kushirikiana kuimarisha maadili ya watoto na kupinga ukatili wa kijinsia, ambao bado ni changamoto kubwa hasa mauaji ya wenzakuwekeza katika ustawi wa watoto kwa mustakabali ymaendeleo ya taifa.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali zinazohusu makuzi ya watoto, inaonyesha kuwa watoto wanapopewa msingi mzuri wa maadili, wanakua wenye utu, heshima, na kuwa nmchango mkubwa kwa jamii. Hata hivyo, kutokana na changamoto mbalimbali za kiuchumi, teknolojiakuporomoka kwa maadili, ukatili wa kijinsia, na unyanyasaji katika jamii au familia ukuaji wa watoto katika kujiamini, ubunifu vinaathiriwa. 

Katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatii wa jinsia, TAMWA tunaendelea kuwasisitiza wazazi, walezi, walimu, na jamii kwa ujumla juu ya umuhimu wa kuwajenga watoto katika misingi ya maadili, kuwafundisha kuheshimu haki za binadamu, kujua hatari za ukatili wa kijinsia na jinsi ya kuripoti matukio ya ukatili wanapokabiliana nayo.

Ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto ni kikwazo chamaendeleo ya kijamii, kiuchumi, na kisiasa kwa kuwa ndo waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia ambao unajumuisha ndoa za utotoni, ukeketaji, vipigo, ulawiti, na unyanyasaji wa kingono.

Huku tukihitimisha siku 16 za kupinga ukatili, na siku ya Haki za Binadamu, TAMWA tunasisitiza kuwa vita dhidi ya ukatili wa kijinsia kuendelea kukemewna wahusika wa vitendo vya kukatili kuchukuliwanahatuaza sheria ili kujenga jamii inayoheshimu haki za binadamu.

Kwa heshima ya siku hii muhimu, TAMWA inatoa wito kwa jamii nzima kushirikiana kwa dhati katika kuhakikisha kuwa watanzania wote na hasa wanawake na watoto wanalindwa dhidi ya ukatili na sauti za waathirika wa ukatili zinasikilizwa

Dkt. Rose Reuben

Mkurugenzi Mtendaji

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Dar Es Salaam, Oktoba 11, 2022. Watanzania leo wanaungana na dunia nzima kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Kike. Siku hii inaadhimishwa  ifikapo Oktoba 11 kila mwaka kama wakati wa kukumbushana kuhusu nafasi ya mtoto wa kike katika nyanja mbalimbali, za kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.
 
 Hivyo basi kwa kuzingatia umuhimu wa siku hii, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, (TAMWA) kwa kushirikiana na Mfuko wa Wanawake Tanzania (WFT) tunaikumbusha jamii, wadau na serikali kuwa bado matukio ya ukatili wa kijinsia kwa watoto wa kike yanaendelea kushika kasi nchini.
 
Kadhalika, kwa kuzingatia kauli mbiu ya mwaka huu isemayo: Muda Wetu ni sasa, haki zetu, Mustakabali Wetu”. TAMWA na WFT tunalenga kuikumbusha jamii kuendelea kuibua na kuchukua hatua dhidi ya vitendo hivi vya ukatili wa kijinsia, hasa rushwa ya ngono, ubakaji, ulawiti, vipigo na ndoa za mapema kwa watoto wa kike. 
 
TAMWA na WFT tumebaini kuwa licha ya  vyombo vya dola kuchukua hatua na kupinga vikali vitendo hivyo dhidi ya watoto wa kike lakini bado matukio ya rushwa ya ngono, ubakaji, ulawiti, mimba za mapema na udhalilishaji yanazidi kushamiri huku watuhumiwa wengi wakiwamo wazazi, walezi, walimu pamoja na watu wao wa karibu ambao ndio wamepewa jukumu la kulinda watoto hao.
 
Imeshuhudiwa kuwepo kwa matukio kadhaa ya ukatili wa kijinsia kwa  watoto  wa kike katika kipindi cha  Julai hadi  Septemba mwaka huu  jambo ambalo linatupa wasiwasi kuwa huenda elimu ya kulinda haki za mtoto wa kike bado haijawafikia wengi.
 
Baadhi ya matukio hayo ni pamoja na lile la mwanafunzi wa darasa la saba, Shule ya msingi Shahende, Geita, Helena Mashaka (13) anayedaiwa kuchomwa  moto mikononi na mama yake hali iliyosababisha kushindwa kufanya mitihani yake ya darasa la saba. 
 
Kadhalika, mtoto Farida Makuya (16)  anadaiwa kuuwawa usiku wa Jumanne, Oktoba 4, 2022 nyumbani kwao Mtumba jijini Dodoma na watu wasiojulikana. 
 
Wakati huo huo, Padri wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwabaka na kuwalawiti watoto zaidi ya 10 wa mafundisho ya kipaimara na kisha kuwapa fedha kiasi cha kati ya Sh 3,000 hadi 5, 000. 
 
Tukio jingine ni la mwanafunzi wa darasa la sita, (12), wa Shule ya Msingi Mbagala Kuu, Dar es Salaam,  anadaiwa kubakwa na Mwalimu wake, ambapo  Mwalimu huyo amekuwa akimpatia binti huyo ufunguo wa makazi yake binafsi ili endapo akimuhitaji aweze kufika kwake kwa urahisi.
 
Hata hivyo, tunaipongeza serikali kupitia vyombo vya sheria kwa kutumia muda mfupi kusimamia na kutoa hukumu dhidi ya mwalimu wa shule ya msingi ya Global, Dar es Salaam, aliyehukumiwa kifungo cha maisha kwa kubaka na kulawiti mwanafunzi wa miaka minane. 
 
Utafiti uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto (UNICEF) umebaini kuwa wasichana milioni 120, duniani wamewahi kulazimishwa kufanya ngono bila ridhaa yao.
 
Pamoja na ukatili huo kwa watoto wa kike, WFT na TAMWA  bado wanasisitiza jamii kuepuka rushwa ya ngono hasa kwa watoto wa kike. 
 
Mwaka 2020, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ilichapisha ripoti ya utafiti na kuibua kuwepo kwa rushwa ya ngono katika Vyuo Vikuu viwili vya umma nchini, ambavyo ni Chuo kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM) na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
 
Kadhalika, mwaka 2021, TAMWA kwa kushirikiana na (WFT) ilitekeleza mradi wa kuangazia rushwa ya ngono kwa wanahabari. TAMWA ilifanya utafiti na kubaini wanahabari wanakabiliwa kwa kiasi kikubwa na rushwa ya ngono na ukatili mwingine ndani ya vyombo vyao vya habari. 
 
TAMWA tumebaini kuwa wasichana wanahabari vyuoni  hukumbana na vitendo vya rushwa ya ngono na kusababisha wengi kuikimbia taaluma  hiyo wakihofia vitendo vya rushwa ya ngono ambayo hukumbana navyo kuanzia wakiwa vyuoni Mkurugenzi wa TAMWA, Dk Rose Reuben. 
 
TAMWA na WFT bado tunaendelea kuipongeza TAKUKURU kwa kufanya mabadiliko ya kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya Mwaka 2007.  Hii ni dhamira chanya kwa serikali katika kushughulikia uovu huu katika nchi yetu. Kwa njia hii, inabakia kuwa sheria ya msingi katika kujenga msingi wa maadili ya taifa katika ngazi na taasisi zote. 
 
“Hata hivyo katika kifungu kidogo cha 2,cha sheria hii,  tumeona kuwa uchambuzi wa sheria unachanganya  neno ukahaba na ngono: Pale ambapo kuna makubaliano ya pande zote, ya kubadilishana ngono kwa ajili ya huduma, au pesa, (katika kesi hii hakuna unyang'anyi wa mamlaka). Hivyo tunaomba kuondolewa kwa kifungu kinacholeta utata kati ya rushwa ya ngono na ukahaba Rose Marandu, Mkurugenzi Mtendaji, WFT
 
Hivyo basi tunapoadhimisha siku hii ya mtoto wa kike, tunatamani dunia itambue thamani yao katika maendeleo, afya yao, elimu yao, uchumi wao na ushiriki wao katika siasa, jamii ikiutambua mchango wao, itasimamia katika ulinzi wao na hivyo kupunguza matukio haya ya rushwa ya ngono. 
Tunaomba serikali kupitia Takukuru, kuendelea kujikita katika mapambano haya wakishirikiana na wadau, ili jamii iwe na taarifa za kutosha kuhusu usalama wa watoto wa kike Rose Marandu,WFT
Hatutaacha, hatutanyamaza, hadi uwepo usalama wa watoto wa kike Tanzania!
 
 
Dkt. Rose Reuben
Mkurugenzi Mtendaji
Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA)
 
 
Rose  Marandu
Mkurugenzi Mtendaji
Mfuko wa Wanawake Tanzania (WFT)
Mwisho

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Machi 8, 2023, Dar Es Salaam. Leo dunia inaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani.

Kwa mwaka huu, Siku hii inaadhimishwa ikipambwa na kauli mbiu isemayo, “Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia: Chachu Katika Kuleta Usawa wa Kijinsia”

Kauli mbiu hii inatukumbusha pengo lililopo katika teknolojia, kwa upande wa wanawake na watoto wa kike hasa nafasi ya teknolojia katika kuhakikisha usalama, amani, na usawa kwa kundi hilo.

Search