Gallery

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Aprili 11, 2020. Wakati huu ambapo dunia nzima inapambana na ugonjwa wa Covid -19 unaosababishwa na virusi vya Corona, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinawakumbusha wanahabari na wamiliki wa vyombo vya habari kufuata miongozo ya kutekeleza majukumu yao kwa kujilinda na maambukizi ya ugonjwa huu, na kutumia zaidi teknolojia ya mawasiliano.  Ugonjwa wa Covid-19 unaweza kumuathiri mtu yeyote, hivyo wanahabari, wamiliki wa vyombo vya habari na wadau wote wa habari wanapaswa kukubaliana na mabadiliko ya kiutendaji kazi yatakayowaepusha dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huu. TAMWA inawashauri wanahabari na wamiliki wa vyombo vya habari kujikita katika kutumia maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano kupata habari badala ya kwenda katika mikusanyiko isiyo ya lazima kwani taarifa zinaweza kutumwa kimtandao au mahojiano kwa njia ya simu. “Bila shaka hofu ya ugonjwa wa Covid 19 itabadili mfumo wa utendaji kazi wa tasnia ya habari kama taasisi inayohudumia jamii na kuanza kujiona kuwa na wao pia ni sehemu ya jamii,” TAMWA tunathamini usalama wa wanahabari kwa kuwa sisi ni sehemu na mdau wa vyombo vya habari ambavyo vimekuwa chanzo cha ufikishaji wa taarifa za kutetea haki za wanawake na watoto zenye lengo la kuwa na Tanzania inayoheshimu misingi ya usawa wa jinsia.  Wanahabari wanaoripoti kuhusu COVID-19 na wanahabari wengine, wanashauriwa kufanya maandalizi kabla ya kwenda katika mikutano, kwa kufuata mbinu za kujikinga na maambukizi. 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) leo Aprili 5, kwa kushirikiana na Hospitali ya Narayani India wametoa  elimu ya afya pamoja na ushauri wa kitaalamu kwa wanahabari wanawake kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kwa lengo la kuwajengea uwezo juu ya afya ya uzazi na magonjwa na magonjwa ya saratani.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika  jijini Dar es salaam, mwenyekiti wa TAMWA, Bi. Alakok Mayombo alisema washiriki wa mafunzo hayo watajengewa uwezo kuhusu afya ya uzazi pamoja na matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii.

“Katika kipindi cha siku mbili za mkutano mkuu wa chama chetu,  Tulizungumza na marafiki wa TAMWA Narayana hospital ambao walikubali kutoa elimu ya afya uzazi kwa wakina mama kupitia kipengele chao cha awareness kuhusu hasa magonjwa ya kansa" Alisema Bi. Mayombo. 

Alisema kupitia elimu ambayo itatolewa kwa washiriki hao itawawezesha kuwasaidia kujilinda na kupambana  kansa kwa akina mama. 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA Rose Reuben, alisema, mbali na mafunzo hayo ya afya ya uzazi pia watatoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya ya mitandao ya kijamii.

“Ni lazima jamii itambue sheria ya maudhui ya mtandao pamoja na sheria za vyombo vya habari katika mitandao ya kijamii.  Lengo letu ni kujiongezea ujuzi katika maeneo haya, hivyo  watu wa TCRA watakuja kutusaidia kutoa mafunzo kuhusu  matumizi ya mtandao ni”. Alisema Rose.

Nae daktari kutoka Hospitali ya Narayana, Bwana Limbanga Freddie alisema, tafiti zinaonyesha kumekuwepo na ongezeko kubwa la wagonjwa wa kansa kutokana na mabadiliko ya mfumo wa maisha pamoja na kutofanya mazoezi, kutokufanya kazi ngumu na kutumia vyakula ambavyo ni hatari kwa afya.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake nchini – TAMWA kimesikitishwa na kulaani vitendo na matukio ya ukatili uliopindukia unaofanywa na baadhi ya walimu kuwapiga wanafunzi bila kufuata sheria zinavyoelekeza na kupelekea baadhi yao kuathirika kisaikolojia na hata kupoteza maisha kutokana na vipigo hivyo.

Miongoni mwa matukio ya kusikitisha ni lile la tarehe 27 Agost ambapo MWANAFUNZI wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kibeta, Bukoba mkoani Kagera, Sperius Eradius (13) alifariki dunia baada ya kupigwa na mwalimu wake kwa kutuhumiwa kuiba pochi ya mwalimu.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Wakati dunia ikisherehekea Siku ya Wanawake Duniani, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA) kinakuletea wanahabari wakongwe waanzilishi wa TAMWA. Hiki ndicho wanachokisema katika maadhimisho haya ya Siku ya Wanawake Duniani.

Ummy Mahfoudh.  Ni mwanahabari mkongwe, Mwanachama wa Chama cha Wanahabari  Wanawake tangu 1988. Amewahi kufanya kazi katika taasisi zisizo za kiserikali za kitaifa na kimataifa katika nchi za Uingereza, Denmark, Tunisia na Afrika Kusini.
Ni miongoni mwa walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika mkutano wa kidunia wa haki za mwanamke, maarufu mkutano wa Beijing mwaka 1995. Amewahi kushiriki utafiti wa chanzo cha mauaji ya wanawake wazee kutokana na imani za kishirikina na mauaji ya albino Tanzania. 
 Kwa sasa ni mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya magazeti Zanzibar
Ni mshairi, ana mume na watoto wanne. 
Anachokisema katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Tanzania;
“Katika kuadhimisha Siku ya Mwanamke  Duniani, tukumbushane kushughulika na kizazi cha sasa. Tupo kisasa kiasi cha kusahau sisi tulilelewa vipi. Watoto wa kike wafundishwe masuala chanya ya kimila badala ya kufikiri kila kitu cha kimila ni kibaya,”
“Mimi watoto wangu wote nawalea sawa bila kujali wa kike au wa kiume. Wale wa kiume wote wakifikisha miaka 14 wanajua kukuna nazi, kupika nk” (Ummie Mahfoudh)
 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Mkurugenzi wa Chama Cha Wanahabari Wanawake (TAMWA) aliyemaliza muda wake, Edda Sanga, amepewa tuzo ya heshima ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake katika Asasi za kiraia. Tuzo hiyo imetolewa leo na Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP), wakati wa tamasha la 14 la Jinsia. 

“Nimefurahi kupokea tuzo hiyo nawashukuru sana na kuwapongeza pia wale ambao wameona nimestahili kupokea tuzo hiyo,” Amesema Edda Sanga. Pia amewataka wengine waliopata tuzo hiyo kuendeleza mapambano ya kumkomboa mtoto wa kike, kumlinda na kumpa haki yake.

TAMWA tunampongeza Edda Sanga kwa kutwaa tuzo hii adhimu na pia tunawapongeza TGNP Mtandao kwa kuona umuhimu wa kuandaa tuzo hizi.

Search