- TAMWA
- Hits: 510
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




Dar es Salaam, Novemba 5, 2025.Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinatoa pole za dhati kwa Watanzania wote waliopata madhila kwa ndugu, jamaa, Tasnia ya Habari na marafiki kutokana na vurugu zilizojitokeza wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.
TAMWA inawapa pole maalum familia zote zilizopoteza wanawake, watoto, na wanahabari, sambamba na wale wote walioumia au kuathirika kwa namna yoyote kutokana na matukio hayo ya kusikitisha.
Wakati Taifa likipita katika kipindi hiki kigumu, TAMWA inaungana na Watanzania wote wanaofanya jitihada za kuijenga upya hali ya utulivu, mshikamano na amani nchini. Tunaendelea kusisitiza umuhimu wa kulinda utu, kuheshimu haki za binadamu, na kudumisha mazungumzo ya amani kama nguzo ya taifa letu.
Dkt. Rose Reuben
Mkurugenzi Mtendaji.
Chama Cha Waandishi Habari Wanawake (TAMWA) kimepewa mafunzo ya siku nne kwa ajili ya kujengewa uwezo kuhusu masuala ya usalama wa kimtandao ili kuwezesha kufanya kazi kwa ufanisi na kwa usalama.
Dar es Salaam, Novemba 14, 2025. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA) kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ujerumani(GIZ) leo wanazindua mradi wa ‘Sauti Zetu’ wenye lengo la kupaza sauti ili kuzuia, kupunguza ukatili wa kijinsia na kutoa elimu kwa kutumia vyombo vya habari .
Sambamba na uzinduzi huu, TAMWA na GIZ kwa pamoja tunapaza sauti zetu ili kuwasaidia wanawake na watoto dhidi ya ukatili wa kidijitali.
Haya yote yanafanyika wakati dunia inaelekea katika kuadhimisha Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, kuanzia Novemba 25 hadi Desemba 1.
Hivyo basi, TAMWA tunaamini kuwa, uzinduzi wa mradi huu unafanyika huku kukiwa na haja kubwa ya kuwasaidia wanawake na watoto dhidi ya madhila ya ukatili unaofanyika mtandaoni.
Ukatili wa mtandaoni unawaathiri wanawake na watoto sambamba na makundi mengine kwa kiasi kikubwa kwani kundi hili bado halina uelewa wa kutosha wa kujilinda na kulinda taarifa zao.
TAMWA kwa uzoefu na kwa tafiti tulizowahi kufanya tumebaini kuwa faida na hasara za matumizi ya dijitali ni sawa na shilingi yenye pande mbili kwani wanawake na watoto wanatumia vifaa vya kidijitali na kupata faida lukuki lakini kwa upande mwingine mitandao ya kidijitali inawaathiri.
Na leo tunayo furaha kubwa kuzindua mradi huu adhimu wa ‘Sauti Zetu’ wakati ambapo tumebakiza siku chache tu kabla ya kuadhimisha Siku hizi 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia.
Tukirejea kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, ambayo mwaka huu inasema: ‘Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia 2025: Maliza ukatili wa kijinsia kupitia majukwaa ya kidijitali kwa wanawake na wasichana wote’.
TAMWA tunasisitiza kuwa wanawake na watoto wanapaswa kulindwa dhidi ya ukatili huu wa kidijitali.
Kwani tumeshuhudia madhara ya afya ya akili na ya kimwili yanayosababishwa na matumizi yasiyo sahihi ya mitandao ya kijamii.
Kumekuwa na juhudi za dhati za serikali, Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya na wanaharakati wa masuala ya jinsia.
Kwa mfano, Mkataba wa Kidijitali wa Kimataifa wa 2024 (Global Digital Compact)uliweka viwango vya kwanza vya Umoja wa Mataifa kuhusu usalama wa kidijitali na utawala wa akili bandia (AI governance).
Mwezi Desemba 2024, nchi Wanachamazilipitisha Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Uhalifu wa Mtandaoni (UN Cybercrime Convention), chombo cha kwanza cha kisheria cha kimataifa chenye athari katika kukabiliana na ukatili wa kidijitali.
Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN General Assembly)pia ulipitishaazimio kuhusu Ukatili Dhidi ya Wanawake katika Mazingira ya Kidijitali mwaka 2024, likizitaka nchi kuchukua hatua za haraka na madhubuti za kuzuia na kutokomeza ukatili wa kidijitali, pamoja na kuimarisha udhibiti na uwajibikaji wa majukwaa ya mtandaoni.
Lakini bado TAMWA imeona kuna uelewa mdogo juu ya matumizi sahihi ya majukwaa ya kidijitali hali inayochagiza madhara kwa kundi hili la wanawake na watoto.
Kwa mfano, kusambaza picha au video za faragha bila ridhaa, mara nyingi hutumika kuwaaibisha, kuwabambikizia makossa, au kuwatala wanawake na wasichana.
Mengine ni kufichua taarifa binafsi kwa kuweka namba ya simu, mahala pa kazi au sura ya mwanamke mitandaoni kwa lengo la kumtisha.
Lakini pia kuna ukatili wa mitandaoni ambapo watu huunda akaunti bandi kwa kutumia jina au picha ya mwanamke ili kuharibu sifa yake au kudanganya watu wengine.
Ukatili mwingine ambao kimsingi unafanyika sana hapa nchini ni kauli za chuki au maudhui ya chuki ambapo watu huandika au kutamka maneno ya matusi yanayochochea ubaguzi au ukatili dhidi ya wanawake na wasichana.
Mengine ni wadhalilishaji kutumia vitisho kwa kusambaza picha au video za faragha na kisha kudai pesa au upendeleo wa kingono.
Wasichana wadogo wanaotumia mitandao kama Whatsap, Tiktok na Snapchat wapo katika hatari kubwa zaidi.
Madhara ya ukatili huu ni makubwa kwani vifo, kukosa haki, kutengwa na athari kubwa za kisaikolojia zimewakumba wanawake na wasichana.
Hivyo basi TAMWA tunapozindua mradi huu na tunapoelekea katika kuadhimisha Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia, tunapaza sauti zetu kwa kufundisha na kukemea vitendo vyovyote vya ukatili wa kijinsia kwa njia ya kidijitali.
Katika kuanza utekelezaji wetu, tumeandaa ‘ Mwongozo wa Kanuni 10 za Kujilinda na Ukatili wa Kidijitali’.
Uzinduzi wa Mwongozo huu unakwenda sambamba na safari yetu ya ‘Kupaza sauti’ ili kupunguza ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto kupitia vyombo vya habari.
KUHUSU MRADI WA SAUTI ZETU
Mradi huu unalenga kutumia vyombo vya habari kama nyenzo ya kuelimisha jamiikuhusu masuala ya Ukatili wa Kijinsia (GBV),ikiwemo kueleza maana ya GBV, chanzo chake katika jamii, na kutoaelimu kuhusu huduma zilizopo kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia.
Kupitia utoaji wa ujumbe muhimu kuhusu masuala ya GBV, mifumo ya kisheria, haki za waathirika na njia za kupata haki, mradi huu utawawezesha waathirika kupataufahamu wa haki zao na huduma za msaada zilizopo.
Aidha, mradi huu utalenga kuongeza uelewa wa umma, kupinga mila na desturi kandamizi, na kuhamasisha wadau mbalimbali kuchukua hatua dhidi ya ukatili wa kijinsia.
Mradi huu unatekelezwa katika mikoa minne ya Tanzania Bara, ambayo ni Dar es Salaam (Kinondoni, Temeke), Dodoma (Chamwino, Bahi) na Tanga (Lushoto na Tanga Mjini).
Vyombo vya habari vitakuwa ndicho chombo kikuu cha kufikisha taarifa, kuongeza uelewa na kutumika kama daraja kati ya jamii, asasi, waathirika na jamii nzima.
Background
Tanzania Media Women’s Association (TAMWA) is a non-governmental organization committed to advocating for gender equality, women’s rights, children’s rights, and social justice through media engagement, strategic communication, and community outreach. As part of its ongoing advocacy and public awareness initiatives, TAMWA seeks to engage a qualified consultant or production firm to develop creative audio and video spots aimed at raising awareness on key social issues and promoting positive behavioral change.
Objective of the Assignment
The main objective of this consultancy is to conceptualize, script, produce, and deliver high-quality audio and video spots that effectively communicate TAMWA’s advocacy messages to diverse audiences through television, radio, digital, and social media platforms
Scope of Work
The consultant is expected to:
• Develop creative concepts and scripts for the audio and video spots.
• Production:
o One (1) video spot.
o Two (2) audio/radio spots.
• Conduct filming, voice recording, editing, subtitling, and post-production.
• Ensure the content is audience-friendly, gender-sensitive, and culturally appropriate.
• Incorporate TAMWA branding and key campaign messages.
• Deliver final products in formats suitable for television, radio, and social media platforms.
Expected Deliverables
The consultant shall deliver:
• Approved scripts/storyboards.
• Final edited video spot in high-resolution format.
• Final edited audio/radio spot.
• Short social media cut versions (optional if applicable).
• All raw footage and editable files.
Duration of Assignment
The consultancy is expected to be completed within [10] days from the date of signing the contract
Qualifications and Experience
The ideal consultant/firm should have:
• Proven experience in audio-visual production and storytelling.
• Experience producing advocacy or social impact communication materials.
• Strong understanding of gender, human rights, and development communication.
• Ability to produce high-quality and creative multimedia content.
• Previous work samples related to similar assignments.
Application Requirements
Interested consultants/firms should submit:
• Technical proposal outlining understanding of the assignment and methodology.
• Financial proposal with detailed budget.
• Company profile or CV.
• Portfolio/sample links of previous audio and video productions.
• Proposed work plan and timeline.
Submission Details
Applications should be submitted via email to: [This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.]
Subject Line: Consultancy for Audio and Video Spot Production
Deadline for submission: May 30, 2026.
Only shortlisted candidates will be contacted.
TAMWA Commitment
Tanzania Media Women’s Association (TAMWA) promotes equal opportunity and encourages applications from qualified individuals and firms committed to ethical and inclusive communication
Tanzania Media Women’s Association (TAMWA) is a non-governmental organization committed to advocating for gender equality, women’s rights, children’s rights, and social justice through media engagement, strategic communication, and community outreach. As part of its ongoing advocacy and public awareness initiatives, TAMWA seeks to engage a qualified consultant or production firm to develop creative audio and video spots aimed at raising awareness on key social issues and promoting positive behavioral change.
Objective of the Assignment
The main objective of this consultancy is to conceptualize, script, produce, and deliver high-quality audio and video spots that effectively communicate TAMWA’s advocacy messages to diverse audiences through television, radio, digital, and social media platforms
Scope of Work
The consultant is expected to:
• Develop creative concepts and scripts for the audio and video spots.
• Production:
o One (1) video spot.
o Two (2) audio/radio spots.
• Conduct filming, voice recording, editing, subtitling, and post-production.
• Ensure the content is audience-friendly, gender-sensitive, and culturally appropriate.
• Incorporate TAMWA branding and key campaign messages.
• Deliver final products in formats suitable for television, radio, and social media platforms.
Expected Deliverables
The consultant shall deliver:
• Approved scripts/storyboards.
• Final edited video spot in high-resolution format.
• Final edited audio/radio spot.
• Short social media cut versions (optional if applicable).
• All raw footage and editable files.
Duration of Assignment
The consultancy is expected to be completed within [10] days from the date of signing the contract.
Qualifications and Experience
The ideal consultant/firm should have:
• Proven experience in audio-visual production and storytelling.
• Experience producing advocacy or social impact communication materials.
• Strong understanding of gender, human rights, and development communication.
• Ability to produce high-quality and creative multimedia content.
• Previous work samples related to similar assignments.
Application Requirements
Interested consultants/firms should submit:
• Technical proposal outlining understanding of the assignment and methodology.
• Financial proposal with detailed budget.
• Company profile or CV.
• Portfolio/sample links of previous audio and video productions.
• Proposed work plan and timeline.
Submission Details
Applications should be submitted via email to: [This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.]
Subject Line: Consultancy for Audio and Video Spot Production
Deadline for submission: May 20, 2026.
Only shortlisted candidates will be contacted.
TAMWA Commitment
Tanzania Media Women’s Association (TAMWA) promotes equal opportunity and encourages applications from qualified individuals and firms committed to ethical and inclusive communication.