Gallery

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Florence Majani, TAMWA.

Ruangwa, Lindi. Kinamama katika kata ya Likunja, wilayani Ruangwa wamelaumiwa kuwa wao  ndicho chanzo cha kuvunjika kwa ndoa kila kukicha katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo, kasi ya wanandoa kuachana ni kubwa na hata ile ya kuoana nayo ni kubwa hasa msimu wa mavuno.

Hayo yameelezwa jana, wakati wa mafunzo ya wanakamati za ulinzi za kata hiyo, yaliyotolewa na Chama cha Wanahabari Wanawake(TAMWA) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mwalimu wa Shule ya Msingi Likunja, Maria Lilai, alisema ndoa zinavunjika kila siku kwa sababu ya mfumo wa  mwanamke kuwa na madaraka kwenye familia zaidi ya baba.

“Mfumo  wa ‘matrilinneal’ ambao unampa mama madaraka ya kuwa kichwa cha familia, ndiyo unaofanya ndoa nyingi zinavunjika. Kwa sababu wanaume wengi hawapendi kuwa chini ya mwanamke, hivyo  migogoro  mingi inaishia kwenye talaka,” alisema.

Alisema kesi zinazotolewa talaka ni za kila kukicha lakini zipo kesi ambazo wanandoa wanatengana lakini  mwanaume anakataa kutoa talaka.

“Akikataa kutoa talaka inabidi uinunue, wapo wanaume ambao hukataa kutoa talaka hadi uwape hela. Ukiwapa hela wanakupa talaka yako,” alisema.

 

Ofisa Maendeleo ya Jamii kata ya Likunja, Sarah Pongolela alisema kwa mila za Wamwera mwanaume anapooa ni lazima amjengee mke wake nyumba.

“Mara nyingi migogoro hii inaanzia kwenye mgawanyo wa mali, au pale ambapo kipato kinaongezeka,” alisema

 Alisema hakuna takwimu rasmi za matukio ya talaka kwa sababu mengi yanamalizika katika ngazi ya familia.

“Kesi nyingi zinamalizwa baada ya wanandoa kugawana mali, lakini kama kesi hiyo ina mgogoro zaidi, ndipo zinapofikishwa kwenye ofisi za kata au Bakwata au mahakamani,” alisema.

Akizungumzia kesi za talaka, Mwenyekiti wa Chama cha kinamama katika kata hiyo, Shelly Nachinuku,  alisema zipo kesi nyingi za ndoa kuvunjika lakini yeye alikuwa na maoni tofauti na Maria akidai kuwa chanzo ni wanaume.

“Kesi hizo zinaanzia kwa wanaume, mfano mwanaume akishaona amemzalisha mwanamke anamuacha, au akiona kuna watoto wengi ndani ya nyumba anamuacha na anaenda kwa mwanamke mwingine,” alisema

Alisema suala la talaka linachangiwa na wanaume kutokukaa nyumbani na kutotimiza majukumu yao  kwenye familia.

“Wanaume wanapoona msimu wa mavuno, wanazikimbia familia zao na kudai wanakwenda kuangalia mazao kumbe, wanayauza na kuanza kutumia fedha na wanawake wengine,” alisema

 Alisema hata huko shuleni imebainika kuwa wanafunzi wengi wanalelewa na mzazi mmoja au bibi  baada ya wazazi wao kuachana.

Katekisti wa Kanisa Katoliki, kigango cha Likunja, Erick Akwilambo alisema kesi hizo za wanandoa kuachana zipo nyingi katika kata hiyo na kueleza kuwa zinasababishwa na mfumo jike ambapo wanawake wanakuwa  na madaraka makubwa kwenye familia.

“Ndiyo maana hata hizi kesi za wanaume kupigwa ni nyingi, huku wanaume hawana la kusema, hata mtoto akizaliwa anakuwa ni wa ukoo wa kwa mama,” alisema

Ofisa Elimu wa Kata ya Likunja, Mwajuma Ibadi alisema sio talaka tu, bali hata ndoa nazo zinafungwa kwa wingi kama ilivyo talaka. Alisema tatizo kubwa ni kuwa wakazi wa eneo hilo wanafunga ndoa za mashindano.

“Kwa mfano, wanandoa wakiachana, basi kila mmoja atataka aoe au aoelewe tena ili kumkomoa mwenza waliyeachana,”alisema

Ibadi alisema asilimia 70 ya wanafunzi kwenye shule za msingi, wanalelewa na bibi au babu baada ya wazazi kutengana.

Alisema ndiyo maana kuna mmomonyoko wa maadili ikiwamo mimba za utotoni na elimu duni kwa kuwa watoto wengi wanakosa malezi ya wazazi wote wawili.

Mtendaji Kata ya Likunja, Hassan Kalembo alisema kesi hizo za ndoa kuvunjika zipo kwa wingi lakini hana takwimu rasmi.

“Tunapokea malalamiko hayo kila siku, lakini chanzo cha haya yote ni tamaa. Wanawake wa kabila hili(wamwera) wakiona mume amechuma mali kadhaa wanataka kuachana ili wagawane mali,” alisema.

Ofisa Maendeleo wilaya ya Ruangwa, Rashid Namkulala alisema matukio ya wazazi kutengana au kuachana ndiyo yanayosababisha malezi duni kwa watoto.

“Sisi viongozi tutaendelea kutoa elimu ya kina kwa wakazi wa eneo hili ili kesi za talaka zipungue. Tumeshuhudia kuwa watoto wanakosa malezi bora pindi tu wazazi wanapotengana,” alisema

Hata hivyo, Ofisi ya Ustawi wa Jamii ya wilaya ya Ruangwa, walisema hawana takwimu za talaka.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
  1. Tuliweza kufanya mahojiano na Mwanaharakati, Waziri na Balozi wa zamani, Mama Getrude Mongela: Finya hapa kupata zaidi: https://www.instagram.com/p/C4DCBDJNGr4/
  1. Tuliweza kufanya mahojiano na Mkurugenzi wa TAMWA, Dk Rose Reuben: Finya hapa kusikiliza zaidi: https://www.instagram.com/p/C4M_5NHtZO3/
  1. Tuliweza kufanya mahoajino na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Ana Makakala: Kusikiliza zaidi. Finya hapa: https://www.instagram.com/p/C5IOVDJNSnh/
  1. Tuliweza kufanya mahoajino na Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo, Doroth Semu: Kusikiliza zaidi finya hapa: https://www.instagram.com/p/C4qSGabtrrZ/
  1. Tulikuwa na Makala fupi ya video ya Dereva wa Bodaboda Singida, Marry Kalambwa” Finya hapa kumfahamu: https://www.instagram.com/p/C4ulIZvNZpF/
  1. Tulikuwa na Makala fupi ya video ya Semeni Kalori: Semeni: Mama wa watoto watano, anayeendesha bodaboda, kusomba mkaa milimani. Finya hapa kumjua zaidi: https://www.instagram.com/p/C4hyRrmtevi/
  1. Tulikuwa na Makala fupi ya video ya Paulina Mathayo, anayeponda kokoto, huko Dodoma; Finya hapa kumfahamu: https://www.instagram.com/p/C5ILJSSthYu/

Tembelea mitandao yetu:

       1.Twitter: https://twitter.com/TAMWA_ 

  1. Instagram: https://www.instagram.com/tamwa_/
  2. Facebook: https://www.facebook.com/media.womenassociation

       4. TAMWA TV: //www.youtube.com/@tamwaonlinetv7655 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Sekretarieti ya Chama cha Wanahabri Wanawake Tanzania – TAMWA, inapenda kuwakumbusha wanachama wake kuwa mkutano mkuu wa Chama kwa mwaka 2022, utahusisha uchaguzi wa wajumbe wa Bodi, hivyo tunawahimiza wanachama wanaowiwa kuwania nafasi hizo kutuma maombi yao mapema kupitia barua pepe This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. Cc: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Fomu za maombi zinapatikana katika tovuti ya Chama www.tamwa.org

Mwisho wa kutuma maombi ni Machi 11, 2022.

Kelvin Mtewele - Afisa Utawala, TAMWA.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake nchini – TAMWA kimesikitishwa na kulaani vitendo na matukio ya ukatili uliopindukia unaofanywa na baadhi ya walimu kuwapiga wanafunzi bila kufuata sheria zinavyoelekeza na kupelekea baadhi yao kuathirika kisaikolojia na hata kupoteza maisha kutokana na vipigo hivyo.

Miongoni mwa matukio ya kusikitisha ni lile la tarehe 27 Agost ambapo MWANAFUNZI wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kibeta, Bukoba mkoani Kagera, Sperius Eradius (13) alifariki dunia baada ya kupigwa na mwalimu wake kwa kutuhumiwa kuiba pochi ya mwalimu.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinatangaza nafasi kwa makampuni ya udalali na madalali binafsi kuuza magari yake mawili kama yanavyoonekana katika tangazo hapo chini.

 

Tafadhali tuma barua ya maombi kupitia barua pepe This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. kwa maelezo zaidi tembelea ofsi zetu au piga simu namba +255222772681 au  0719485006 au 0754462632

 

 

 

 

Search