Gallery

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

 

Godwin Assenga, Tamwa.

Dar es Salaam. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA) kinatoa pongezi za dhati kwa mwanaharakati wa masuala ya haki za binadamu na Mkurugenzi wa Taasisi ya Msichana Initiative, Rebecca Gyumi kwa kushinda tuzo ya Umoja wa Mataifa katika kipengele cha utetezi wa haki za binadamu kwa mwaka 2018.

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Maria Fernanda alimtangaza Gyumi pamoja na washindi wengine, Octoba 25 mwaka huu.

Washindi wengine ni marehemu Asma Jahangir , mwanasheria wa Haki za Binadamu wa Pakistan, Joenia Wapichana, mwanaharakati wa haki za watu wa jamii za pembezoni wa Brazil na  taasisi ya Front Line Defenders, inayojihusisha na ulinzi wa haki za binadamu, Ireland.

“TAMWA inaamini kuwa, ushindi wa Gyumi ni ushindi kwa watoto na wanawake wote nchini ambao haki zao zimekuwa zikikandamizwa,” anasema Edda Sanga, Mkurugenzi, TAMWA.

Wengine waliowahi kushinda tuzo hii miaka ya nyuma ni pamoja na aliyewahi kuwa mke wa Rais wa Marekani, Franklin Roosevelt, Eleanor Roosevelt, mwanaharakati wa haki za binadamu na kiongozi wa dini wa Marekani, Martin Luther King.

 Wengine ni  aliyewahi kuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela na  Kamati ya Kimataifa ya Shirika la Msalaba Mwekundu(ICRC)

 Sherehe za utoaji wa tuzo hizi zitafanyika Desemba huko New York, Marekani.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) leo Agosti 27, kimefanya uchaguzi wake Mkuu wa mwaka na kumchagua Joyce Shebe kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.
 
Shebe ambaye ni Mhariri Mkuu wa Clouds Media Group, ataongoza kwa miaka mitatu. Huu ni muhula wa pili kwa Shebe baada ya kuongoza miaka mitatu ya mwanzo kuanzia 2019. Katika uchaguzi huo, Shebe alikuwa akichuana na Mwasisi wa TAMWA, Lyela Sheikh.
 
Nafasi nyingine katika uchaguzi huo ni wajumbe wa bodi, ambapo Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Tumaini, Mary Kafyome, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha St Augustine, Dk Kaanaeli Kaale nao walichaguliwa kuwa wajumbe wa bodi ya Tamwa.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Na Edina Salila
Rushwa ya ngono ni tatizo linalowatesa watu wengi hasa wanawake na wasichana kazini na katika taasisi za elimu yaani vyuo na vyuo vikuu.
Chanzo kikuu cha rushwa hiyo kinatajwa kuwa ni mmomonyoko wa maadili na matumizi mabaya ya madaraka kwa baadhi ya wahadhiri na viongozi na watumishi katika maeneo ya kazi.
Ingawa rushwa hii huwaathiri zaidi wanawake, kumekuwapo madai kutoka kwa watu na vyanzo mbalimbali kuwa, baadhi ya wasichana wamekuwa kichocheo na ushawishi kwa wahusika ili wapate upendeleo kwa malipo ya ngono.
Katika moja ya semina za hivi karibuni zilizoandaliwa na Tamwa kwa wahariri na wandishi wa habari Dar es Salaam, washiriki walisema kutokana na uwezo mdogo kimasomo, baadhi ya wanafunzi wa kike wanajenga mazoea ‘yanayovuka mipaka’ kwa wakufunzi na wahadhiri wa kiume ili wapewe upendeleo wa alama za juu katika mitihani.
Utafiti uliofanywa na Mfuko wa Udhamini wa Wanawake Tanzania (WFT- T) kwa kushirikiana na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) mwaka 2020 katika baadhi ya vyuo vikuu nchini, ulibaini kuwa, zaidi ya asilimia 50 ya waliohojiwa walieleza kuwepo kwa rushwa ya ngono vyuoni.
Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma wa TAKUKURU, Joseph Mwaiselo, anasema kutokana na kuwapo rushwa ya ngono, mwaka 2007 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilitunga Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na katika sheria hiyo, kiliwekwa Kifungu cha 25 ili kuharamisha rushwa ya ngono.
Kwa mujibu wa sheria hiyo, ni kosa kwa mtu mwenye mamlaka kutoa sharti lolote la kutaka rushwa ya ngono katika ili kutoa huduma husika.
“Tuligundua kuna rushwa ya ngono katika vyuo vikuu na kwamba, wapo wanaotumia mamlaka yao vibaya kwa kudai rushwa ya ngono, lakini pia wapo wanafunzi wanaowashawishi wahadhiri ili wapewe alama za kuwafanya wafaulu mitihani,” alisema.
Kwa mujibu wa utafiti huo, mifumo dhaifu na isiyo rafiki kwa waathirika kutoa taarifa na kushughulikia tatizo hilo, ni miongoni mwa mambo yanayokwamisha mafanikio katika vita dhidi ya rushwa ya ngono.
Mkaguzi wa Polisi kutoka Dawati la Jinsia Wilaya ya Ubungo, Evetha John, anasema: “Tumeshapokea kesi za wanafunzi wa vyuo wakilalamikia rushwa ya ngono, lakini kwa sababu tunashirikiana na taasisi nyingine husika ikiwemo Takukuru; waathirika tunawaunganisha na maofisa wa Takukuru ili kupata usaidizi zaidi wa kisheria.”
Mkufunzi wa Masuala ya Mawasiliano ya Jamii, Mary Kafyome, anasema kikwazo kingine katika mafanikio dhidi ya tatizo hilo, ni taasisi nyingine zikiwamo za elimu ya juu kutokuwa na sera zilizo wazi kuhusu masuala ya usawa wa kijinsia.
“Baadhi ya vyuo vikuu havina sera za kuzuia ukatili wa kingono na usawa wa kijinsia, hivyo ni ngumu kuzuia vitendo hivyo vyuoni, lakini pia vyuo vingine tumeona sera wanazo lakini hazijulikani kwa wafanyakazi na wanafunzi, hii huchangia kushamiri kwa vitendo hivyo,'' anasema Kafyome.
Kwa mujibu wa uchunguzi, ukimya wa wanawake wengi katika jambo hili hufanya lisisikike huku waathirika wengine wakiamini kuwa, wakifichua uovu huo, jamii itawanyanyapaa.
“Waathirika wengi wanahofia kusema kwa sababu hawana uhakika wa kupata haki yao na kuhofia mtuhumiwa kusikilizwa zaidi kuliko wao,” anasema Kafyome.
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) aliyeomba jina lake lisitajwe anasema: “Wasichana tunateseka sana na hili tatizo maana sasa kiwango cha juu cha alama ndio dili na si elimu yenyewe… Ndio maana wengine hutumbukia katika huo mtego kwani hata wahadhiri wenyewe wanajali maksi na si elimu hali inayosababisha rushwa hii kuonekana jambo la kawaida vyuoni.”
Anaongeza: “Nashauri tupewe mbinu za kuripoti matukio haya."
Naye Anna Hangwa, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini (TUDARCo) kilichopo Dar es Salaam, anasema: “Tunatakiwa kujithamini, kuwajibika… Mwalimu akitaka kukurudisha nyuma kimasomo, kama umewajibika na kusoma ipasavyo utakuwa na uhakika wa ufaulu wako."
Wadau mbalimbali wa usawa wa kijinsia wanashauri kuwapo madawati ya kjinsia yaliyo rafiki zaidi kwa wanafunzi kuripoti matukio ya unyanyasaji yanayofanyika vyuoni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tamwa, Dk Rose Reuben, anasema: “Ni wakati sasa wa madawati ya kijinsia kuwa hai katika kila upande.”

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania,(TAMWA), tumepokea kwa masikitiko kifo cha mmiliki wa kampuni za IPP nchini, Dk Reginald Mengi ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa wamiliki wa vyombo vya habari MOAT.

 

Kifo hiki ni pigo kubwa kwa tasnia ya habari nchini, pia kwa jamii ya Watanzania hasa kwa watu wenye ulemavu.

 

Dk Mengi ameacha alama katika tasnia ya habari kwa kuanzisha vyombo vya habari na alibeba dhamana ya kuwa mlezi kwa wanahabari nchini, na alileta heshima katika tasnia hii nchini.

 

Atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika tuzo za umahiri wa habari za Ejat hasa katika maudhui kuhusu watu wenye ulemavu, ambako amekuwa akidhamini tuzo hizo.

Atakumbukwa kwa upendo wake  mkubwa kwa wenye ulemavu. Dk Mengi amekuwa muumini mzuri wa masuala ya usawa wa kijisia katika taasisi zake ambapo ametoa nafasi za ajira na za uongozi kwa wanawake na wanaume.

 

Pia Dk Mengi alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa Shirikisho la wenye Viwanda nchini.

Dk Mengi alikuwa na ndoto nyingi, mojawapo ni ya kushirikiana  na serikali kutokomeza  umaskini kama alivyoandika kwenye ukurasa wake wa twitter Machi 19, ''Ndoto yangu ni kushirikiana na serikali kutokomeza kabisa umaskini Tanzania''

 

Ulale salama Dk Mengi, tutaendelea kuyaishi maneno yako kwa mfano nukuu yake ya Januari 7 aliyotuma kupitia mtandao wake wa twitter akisema: ''Kwa unyenyekevu ninawashauri  watanzania wenzangu kuufanya mwaka 2019 kuwa mwaka wa upatanisho na msamaha, chuki ni mzigo mzito kuubeba mioyoni mwetu, kupendana ni njia peee ya kusonga mbele''.

 

Pumzika kwa amani Dk Mengi.

 

Rose Reuben

MKurugenzi TAMWA

 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

TAMWA AGM April 25-26, 2024

Mkutano Mkuu wa Wanachama wa TAMWA unafanyika kesho, Aprili 25 na Aprili 26. Njoo ukiwa umevaa sare yako ya miaka 36 ya TAMWA, njoo tuzungumze, njoo tufahamiane, njoo ukijue chama chako. #TAMWAAGM2024 #ZuiaUkatili #WomenInMediaTz

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

November 28, 2014

On-going Events This November and December

December 25, 2014 Public rally from Mnazi Mmoja ground to Karimjee hall. Nationally this has been organised by WiLDAF, TAMWA is among the major stakeholders and will fully participate.

This year theme is “OPEN UP! DISCLOSE GENDER BASED VIOLENCE FOR THE HEALTH OF THE COMMUNITY

December 2, 2014 CRC –TAMWA one day education awareness session with Kinondoni and Kitunda-Kivule paralegals at TAMWA conference centre.

December 5,2014 CRC will hold a one day counselling for clients at TAMWA grounds, (counselling will be in a form of group and one by one).(Bring your neighbour, sons and daughters)-We are going to invite a Specialist Counsellor who is going to team with CRC. Click here for more activities.

July 17,2014

 SUMMARY REPORT ON PARALEGAL TRAINING HELD ON 15TH  – 16TH  JULY 2014 AT  TAMWA OFFICE DAR ES SALAAM

 1.  About Training

CRC - TAMWA conducted two days training to twelve Paralegals from Newala, Ruanga,Lindi Rural and  Kinondoni - Dar es salaam.

This took place  on 15th  and 16th July 2014 at TAMWA Conference Room, Sinza Mori.

2.  OBJECTIVES

  • To know their challenges especially in providing Legal Aid services and counselling;
  • To raise awareness on Laws relating to public issues like the ’Marriage Act’, ’Land Law,’ ’Inheritance Law’ etc. and
  • To overcome  challenges and  improve better services.

3. Training Team

The Facilitators for the training were the Excecutive Director of TAMWA, Ms.Valeria Msoka; CRC-Coordinator – TAMWA Ms. Gladness Hemedi Munuo, Social Worker CRC- TAMWA Ms. Marcella Lungu and Legal Officer of CRC – Tamwa Ms.  Loyce Gondwe

4.  Areas Covered

  • Training Objectives;
  • The Law of Marriage Act of 1971;
  • Ward Tribunal and Village Council;
  • Probate Act and administration of the Deceased Estate;
  • Court System;
  • By Laws;
  • How to provide counseling; and
  • General duties and obligation of Paralegals.

July 14,2014

Up coming events this July,2014

  1. Crisis Resolving centre (CRC) will conduct Paralegal Training that will commence on 15th to 16th of July, 2014 at TAMWA Resource Centre where by Paralegals from Kindondoni, Newala, Lindi rural and Ruangwa districts will come together to learn and share legal issues related to Gender based Violence (GBV) facilitated by GEWE II:GBV component project.
  2. Crisis Resolving centre (CRC) provide Legal Aid Services every Monday to Wednesday and is opened at  09:00 AM and closed at 03:00 PM.

20.12.2013

CRISIS RESOLVING CENTRE (CRS)

From January to December 2013 CRC attended a total of 2878 clients for the three districts of Dar es Salaam region. Of these, 2470 were from Kinondoni district, 250 from Ilala district and 158 clients from Temeke district. These cases were on matrimonial disputes, Probate, Child maintenance, child abduction, land disputes, rape and family abandonment.

With TAMWA being recognized in its fight against GBV, the CRC received 30 cases clients from other regions seeking services. These included two young girls who had run away from Hanang’, Arusha to escape FGM and child marriage.

In building the capacity of the response mechanisms, CRC trained police gender desk officer from different police posts in Kinondoni district on handling of domestic violence cases. Another training was conducted for 60 paralegals from Kinondoni, Newala, Ruangwa and Lindi Rural district on handling gender based violence cases in their villages.

On a daily basis CRC has managed to:

1. Support women and children survivors of gender based violence in terms of food, cloths shelter and education.

2. Reunite children with their mothers – those who were forcibly taken from their mothers.

3. Provide capacity building to women to enable them to defend their rights in public.

4. Reach both the perpetrators and survivors of domestic violence/gender based violence and educate them on the rights of women and children and the negative effects of GBV on their children and the society.

5. Protect survivors of domestic violence especially underage girls who were forced to stop school in order to get married.

Search