- TAMWA
- Hits: 1322

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania,(TAMWA), tumepokea kwa masikitiko kifo cha mmiliki wa kampuni za IPP nchini, Dk Reginald Mengi ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa wamiliki wa vyombo vya habari MOAT.
Kifo hiki ni pigo kubwa kwa tasnia ya habari nchini, pia kwa jamii ya Watanzania hasa kwa watu wenye ulemavu.
Dk Mengi ameacha alama katika tasnia ya habari kwa kuanzisha vyombo vya habari na alibeba dhamana ya kuwa mlezi kwa wanahabari nchini, na alileta heshima katika tasnia hii nchini.
Atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika tuzo za umahiri wa habari za Ejat hasa katika maudhui kuhusu watu wenye ulemavu, ambako amekuwa akidhamini tuzo hizo.
Atakumbukwa kwa upendo wake mkubwa kwa wenye ulemavu. Dk Mengi amekuwa muumini mzuri wa masuala ya usawa wa kijisia katika taasisi zake ambapo ametoa nafasi za ajira na za uongozi kwa wanawake na wanaume.
Pia Dk Mengi alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa Shirikisho la wenye Viwanda nchini.
Dk Mengi alikuwa na ndoto nyingi, mojawapo ni ya kushirikiana na serikali kutokomeza umaskini kama alivyoandika kwenye ukurasa wake wa twitter Machi 19, ''Ndoto yangu ni kushirikiana na serikali kutokomeza kabisa umaskini Tanzania''
Ulale salama Dk Mengi, tutaendelea kuyaishi maneno yako kwa mfano nukuu yake ya Januari 7 aliyotuma kupitia mtandao wake wa twitter akisema: ''Kwa unyenyekevu ninawashauri watanzania wenzangu kuufanya mwaka 2019 kuwa mwaka wa upatanisho na msamaha, chuki ni mzigo mzito kuubeba mioyoni mwetu, kupendana ni njia peee ya kusonga mbele''.
Pumzika kwa amani Dk Mengi.
Rose Reuben
MKurugenzi TAMWA
November 28, 2014
On-going Events This November and December
December 25, 2014 Public rally from Mnazi Mmoja ground to Karimjee hall. Nationally this has been organised by WiLDAF, TAMWA is among the major stakeholders and will fully participate.
This year theme is “OPEN UP! DISCLOSE GENDER BASED VIOLENCE FOR THE HEALTH OF THE COMMUNITY”
December 2, 2014 CRC –TAMWA one day education awareness session with Kinondoni and Kitunda-Kivule paralegals at TAMWA conference centre.
December 5,2014 CRC will hold a one day counselling for clients at TAMWA grounds, (counselling will be in a form of group and one by one).(Bring your neighbour, sons and daughters)-We are going to invite a Specialist Counsellor who is going to team with CRC. Click here for more activities.

SUMMARY REPORT ON PARALEGAL TRAINING HELD ON 15TH – 16TH JULY 2014 AT TAMWA OFFICE DAR ES SALAAM
1. About Training
CRC - TAMWA conducted two days training to twelve Paralegals from Newala, Ruanga,Lindi Rural and Kinondoni - Dar es salaam.
This took place on 15th and 16th July 2014 at TAMWA Conference Room, Sinza Mori.
2. OBJECTIVES
3. Training Team
The Facilitators for the training were the Excecutive Director of TAMWA, Ms.Valeria Msoka; CRC-Coordinator – TAMWA Ms. Gladness Hemedi Munuo, Social Worker CRC- TAMWA Ms. Marcella Lungu and Legal Officer of CRC – Tamwa Ms. Loyce Gondwe
4. Areas Covered
From January to December 2013 CRC attended a total of 2878 clients for the three districts of Dar es Salaam region. Of these, 2470 were from Kinondoni district, 250 from Ilala district and 158 clients from Temeke district. These cases were on matrimonial disputes, Probate, Child maintenance, child abduction, land disputes, rape and family abandonment.
With TAMWA being recognized in its fight against GBV, the CRC received 30 cases clients from other regions seeking services. These included two young girls who had run away from Hanang’, Arusha to escape FGM and child marriage.
In building the capacity of the response mechanisms, CRC trained police gender desk officer from different police posts in Kinondoni district on handling of domestic violence cases. Another training was conducted for 60 paralegals from Kinondoni, Newala, Ruangwa and Lindi Rural district on handling gender based violence cases in their villages.
On a daily basis CRC has managed to:
1. Support women and children survivors of gender based violence in terms of food, cloths shelter and education.
2. Reunite children with their mothers – those who were forcibly taken from their mothers.
3. Provide capacity building to women to enable them to defend their rights in public.
4. Reach both the perpetrators and survivors of domestic violence/gender based violence and educate them on the rights of women and children and the negative effects of GBV on their children and the society.
5. Protect survivors of domestic violence especially underage girls who were forced to stop school in order to get married.
TAMWA AGM April 25-26, 2024
Mkutano Mkuu wa Wanachama wa TAMWA unafanyika kesho, Aprili 25 na Aprili 26. Njoo ukiwa umevaa sare yako ya miaka 36 ya TAMWA, njoo tuzungumze, njoo tufahamiane, njoo ukijue chama chako. #TAMWAAGM2024 #ZuiaUkatili #WomenInMediaTz

Godwin Assenga, Tamwa.
Dar es Salaam. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA) kinatoa pongezi za dhati kwa mwanaharakati wa masuala ya haki za binadamu na Mkurugenzi wa Taasisi ya Msichana Initiative, Rebecca Gyumi kwa kushinda tuzo ya Umoja wa Mataifa katika kipengele cha utetezi wa haki za binadamu kwa mwaka 2018.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Maria Fernanda alimtangaza Gyumi pamoja na washindi wengine, Octoba 25 mwaka huu.
Washindi wengine ni marehemu Asma Jahangir , mwanasheria wa Haki za Binadamu wa Pakistan, Joenia Wapichana, mwanaharakati wa haki za watu wa jamii za pembezoni wa Brazil na taasisi ya Front Line Defenders, inayojihusisha na ulinzi wa haki za binadamu, Ireland.
“TAMWA inaamini kuwa, ushindi wa Gyumi ni ushindi kwa watoto na wanawake wote nchini ambao haki zao zimekuwa zikikandamizwa,” anasema Edda Sanga, Mkurugenzi, TAMWA.
Wengine waliowahi kushinda tuzo hii miaka ya nyuma ni pamoja na aliyewahi kuwa mke wa Rais wa Marekani, Franklin Roosevelt, Eleanor Roosevelt, mwanaharakati wa haki za binadamu na kiongozi wa dini wa Marekani, Martin Luther King.
Wengine ni aliyewahi kuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela na Kamati ya Kimataifa ya Shirika la Msalaba Mwekundu(ICRC)
Sherehe za utoaji wa tuzo hizi zitafanyika Desemba huko New York, Marekani.
Ofisa Maendeleo Wilaya ya Ruangwa, Rashid Namkulala amekemea vikali Mila na desturi zinazochochea ukatili wa wanawake na watoto wilayani humo.