News/Stories

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) leo Agosti 27, kimefanya uchaguzi wake Mkuu wa mwaka na kumchagua Joyce Shebe kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.
 
Shebe ambaye ni Mhariri Mkuu wa Clouds Media Group, ataongoza kwa miaka mitatu. Huu ni muhula wa pili kwa Shebe baada ya kuongoza miaka mitatu ya mwanzo kuanzia 2019. Katika uchaguzi huo, Shebe alikuwa akichuana na Mwasisi wa TAMWA, Lyela Sheikh.
 
Nafasi nyingine katika uchaguzi huo ni wajumbe wa bodi, ambapo Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Tumaini, Mary Kafyome, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha St Augustine, Dk Kaanaeli Kaale nao walichaguliwa kuwa wajumbe wa bodi ya Tamwa.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Sekretarieti ya Chama cha Wanahabri Wanawake Tanzania – TAMWA, inapenda kuwakumbusha wanachama wake kuwa mkutano mkuu wa Chama kwa mwaka 2022, utahusisha uchaguzi wa wajumbe wa Bodi, hivyo tunawahimiza wanachama wanaowiwa kuwania nafasi hizo kutuma maombi yao mapema kupitia barua pepe This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. Cc: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Fomu za maombi zinapatikana katika tovuti ya Chama www.tamwa.org

Mwisho wa kutuma maombi ni Machi 11, 2022.

Kelvin Mtewele - Afisa Utawala, TAMWA.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinapenda kukanusha taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zikionyesha kuwa tumelishukuru Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uamuzi wa kumchukulia hatua Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima.

Pia taarifa hizo zimekwenda mbali zaidi zikionyesha TAMWA imemtaka Askofu Gwajima kumuomba radhi Rais Samia  Suluhu na Waziri wa Afya, Doroth Gwajima kwa niaba ya wanawake wote nchini.

Tunapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa taarifa hizo ambazo zimewekwa katika nembo za vyombo vya habari kama ITV, AYO TV na katika tamko linaloonyesha kusainiwa na Mkurugenzi wa TAMWA Dkt. Rose Reuben, si za kweli. 

TAMWA haijafanya mkutano wa kihabari, haijatoa tamko wala kuzungumza na chombo chochote cha habari kuhusu sakata la Askofu Gwajima na Bunge. 

TAMWA inafanya kazi kwa kufuata maadili na taratibu za kiuandishi  na ina taratibu  zake pindi inapotakiwa kuzungumzia masuala ya jinsia, habari na afya.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive
Machi 18, 2021. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli.
 
TAMWA inaungana na watanzania wote kuomboleza kifo cha kiongozi  huyo mahiri, Rais John Pombe Magufuli. 
Kwa niaba ya wanachama wa TAMWA, bodi ya TAMWA, Wanahabari, Wanawake, na wapigania haki za jinsia, tunatoa pole kwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu,  familia ya Rais Magufuli, Mama Janeth Magufuli viongozi wa serikali na watanzania wote kwa kumpoteza kiongozi wa nchi. 
 
TAMWA inaomboleza msiba huu kwa kukumbuka mafanikio yaliyofanywa na Rais Magufuli katika kipindi cha uongozi wake tangu mwaka 2015. 
 
Rais Magufuli alikuwa na juhudi katika kujenga miundombinu ambayo kwa kiasi kikubwa ilisaidia kumkomboa mwanamke kuanzia ngazi za chini. 
Miundombinu aliyojenga kuanzia ya maji, barabara na mingineyo, ilikuwa inalenga kumkomboa mwanamke, kumtua mama ndoo kichwani na kumsaidia mjasiriamalia mwanamke kufanya shughuli zake kwa umakini na ufasaha, 
Aliwahi kusema kuwa, katika wizara inayomnyima raha  ni wizara ya maji, na hivyo akaamua kuimairisha eneo hilo ili kuhakikisha adha ya maji inatoweka. Kwa kufanya hivyo alimsaidia sana mwanamke wa kijijini na mjini, mwanamke na mtoto wa kike, kwa sababu ukosefu wa maji ulichangia kwa kiasi kikubwa ukatili wa kijinsia, ukosefu wa masomo na ufinyu wa kipato. 
 
Rais Magufuli alikuwa akijipambanua kuwa rais wa wanyonge na kweli alijitahidi kuimarisha miundombinu ya maji, umeme na kuwatazama wajane waliodhulumiwa kwa namna moja au nyingine, kuondoa riba kwa mikopo ya wanawake ya Halmashauri. 
 
TAMWA tulitamani Rais Magufuli, akamilishe kipindi chake  cha uongozi ili Watanzania tupate hasa kile alichodhamiria kukamilisha, kwa sababu alikuwa na maono makubwa.
TAMWA itamkumbuka Rais Magufuli kwa kuwa rais wa kwanza kumteua mwanamke kuwa Makamu wa Rais. 
Kwa hili aliweka historia nchini, ya kuwepo Makamu wa kwanza wa Rais mwanamke, hata kama hatujaifikia ile asilimia 50 kwa 50 ya ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi, 
 
Rais Magufuli atakumbukwa kama kiongozi aliyekuwa anatamani kuwakomboa wananachi kwa ujumla na sio kuwepo kwa mafanikio ya mtu mmoja mmoja. 
 
Mungu ailaze roho ya Hayati John Pombe Magufuli Mahali pema Amina!
 
Rose Reuben
Mkurugenzi Mtendaji 
TAMWA.

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active
Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinawatangazia wanahabari wanawake wenye uwezo wa kufanya habari za uchunguzi, kuwasilisha maombi kupitia barua pepe ya TAMWA This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. Mwombaji anatakiwa  kuambatanisha habari mbili za uchunguzi zilizowahi  kuchapishwa/kurushwa  katika chombo cha habari kinachotambulika. 
Habari hizo ni sehemu ya mradi wa Wanawake katika Vyombo vya habari, unaolenga kuwajengea uwezo wa wanahabari wa kike kupambana na ukatili wa kijinsia, ikiwamo rushwa ya ngono, haki sawa ndani ya vyumba vya habari na ufinyu wa maslahi kwa wanahabari wa kike ndani ya taasisi za habari. 
Mwisho wa kutuma maombi hayo, ni Machi 22, 2021 saa 6 kamili usiku.

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Sauda Msangi, TAMWA.

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA)kimefanya midahalo miwili iliyolenga kuwajengea uwezo wanawake na vijana namna ya kuzuia ukatili wa kijinsia, rushwa ya ngono na kuwepo kwa usawa wa kijinsia ndani ya vyombo vya habari.

Midahalo hiyo iliwalenga wanahabari na wabunge wanawake ili kuongeza idadi ya viongozi wanawake pamoja na kutengeneza mazingira salama yatakayowawezesha kufikia malego yao ya kiuongozi. Midahalo hiyo iliwashirikisha wabunge wanawake na wanahabari kutoka katika mikoa mitatu nchini.

TAMWA inatekeleza mradi wa miaka miwili wa kuwajengea uwezo wanawake na vijana katika vyumba vya habari unaofadhiliwa na International Media Support IMS.

Akizungumza wakati akifungua mdahalo wa wabunge, Naibu Spika wa Bunge Dk Tulia Ackson aliipongeza TAMWA na kusem imekuja mapema, wakati ndiyo mwanzo wa miaka mitano kukiwa na mambo mengi ya kuyaweka vizuri.

“Tuna mambo mengi ya kuyaweka vizuri na wanawake wenzetu, idadi hii ya wabunge inatakiwa kuongezeka walioko katika viti maalumu waende kugombea majimboni na wengine kuingi viti maalumu, amesema Dk Tulia amesema wanawake wabunge waliochaguliwa na kuteuliwa jukumu lao sio tu kuwakilisha vyama bungeni bali pia katika kuwatumikia wananchi ili kuongeza idadi ya wanawake viongozi zaidi nchini kufikia 50/50. “

Wakati ni sasa wa kujiwekea mipango madhubuti ya kuendelea kuwa viongozi, amesema Akizungumzia hofu ya wanawake kujitokeza kuzungumza mbele ya vyombo vya habari Dk Tulia amesema ni kutokanana hofu ya jinsi watakavoandikwa na kuzungumziwa.

Kwa upande wake, Mkurungezi wa TAMWA, Rose Reuben amesema wanawake waliopata nafasi za uongozi wapange mikakati ya kuangalia kuendelea kuwepo na wengine waongezeke kwa kuonyesha wigo mpana wa uongozi, kuonyesha ujasiri na kujitokeza kuzungumzia masuala ya wanawake katika vyombo vya habari.

Reuben amesema wabunge wanawake hawajitokezi kwa wingi katika vyombo vya habari hivyo ni vyema kijitokeza na kuzungumza ikiwa ni njia mathubuti za kujiinua zaidi kisiasa na kiuongoz. Wabunge wanawake waache kuhofia vyombo vya habari kwa kuwa mkiwa bungezi mna nafasi kubwa kuzungumzia na kutilia mkazo masuala ya ukatiki wa kijinsia hivyo kupunguza unyanyasaji dhidi ya wanawake,alisema Reuben amesema TAMWA iko tayari kushirikiana na wabunge wanawake katika kuwaelimisha namna ya kuvitumia vyombo vya habari pamoja na kutumia mitandao ya kijamii.

Kadhalika ameiomba Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo iwe na Dawati la Jinsia litakalowasaidia wanahabari wanawake kupata kwa urahisi, eneo la kusemea pindi wanapokabiliwa na ukatili wa kijinsia, pia litakalowezesha masula ya kijinsia kuzungumziwa katika mikutano ya wafanyakazi.

Katika mdahalo wa waandishi wa habari, wanahabari walionyesha kutokuwepo kwa usawa wa kijinsia na kuwepo wa vitendo vya rushwa ya ngono katika vyumba vya habari Wanahabari wamesema zipo sera za jinsia ndani ya vyombo vya habari hazifuatwi wala kuzungumziwa ndani ya vyumba vya habari.

Pia katika mdahalo huo wanahabari wametoa mapendekezo ya kuwepo kwa madawati ya kijinsia kwenye vyumba vya habari ili kutoa taarifa kwa uhuru iwapo vitendo vya ukatili wa kijinsia vitatokea.

Latest News and Stories

Search