News/Stories

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active
 
BACK GROUND:
 
Tanzania Media Womens Association (TAMWA) is a non-profit, non-partisan, non-governmental and human rights organization founded and registered on 17th  November, 1987 under the Societies Ordinance Cap 337 of 1954 with registration number (SO 6763) and the Association complied with the 2002, NGO Act of the United Republic of Tanzania in 2006. 
 
ABOUT THE CALL
TAMWA under African Women Development Fund (AWDF) is looking for an experienced RADIO AND TV producer who will be responsible to produce a radio spot and or Television Spot which will highlights Challenges, success and women political inclusion landscape in Tanzania 
 
The produced spots will be aired in Televisions and Community radio based in Arusha, Dodoma, Zanzibar and Dar es Salaam. 
The documentary will showcase challenges facing women politicians during the electoral process, successes achieved in women inclusion in all aspect of politics and the current political situation towards the coming election. 
 
Activity Duties 
Gathering content for radio and /TV spot
Looking for best scene for a spot
Editing the drafts
Producing a creative audio clip of a radio spot
Producing a creative visual spot for  TV
Submit first draft of a radio/TV draft spot 
Editing and designing
 
 
Activities Time Frame
Gathering Content for radio/Tv spot should be done from August 25
Editing drafts should be done  by early September
Sharing first draft of the audio/Tv spots should be done by 5th September
Final editing should be done by 10th  September
Submitting final draft by 15th September
 
The interested consultant/company should submit the budget offer, profoma invoice and attach a sample of the previous work and/or link electronically to This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. cc This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.;  by Monday 24th August 2020, before end of business.
 

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Mwandishi Wetu, TAMWA

Dar es Salaam. Wanahabari Wanawake 52 wamefanikiwa kujiunga na Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania -TAMWA mwaka huu hatua inayodhihirisha kuwa wigo wa kuripoti habari za ukatili wa kijinsia na usawa wa kijinsia, utaendelea kupanuka.

Wanachama  hao wapya  kutoka Tanzania Bara(26) na Visiwani(26)  wamejiunga kwa ajili ya kuongeza wigo katika harakati za kuondoa mifumo yote ya ukatili wa kijinsia na kuwawezesha kitaaluma wanahabari wanawake nchini.

Akizungumzia kujiunga kwa wanahabari wapya katika chama hicho Mkurugenzi wa TAMWA, Rose Reuben amesema kujiunga kwa wanahabari hao kunaongeza jitihada za kutetea haki za wanawake na watoto zenye mrengo wa kijinsia.

“Wakati huu tunapaswa kuwa na taarifa mbalimbali zenye mrengo wa kijinsia zitakazosaidia wananchi , watunga sera na  jamii kwa ujumla  kuelewa kwamba jamii yetu inahitaji sera na taarifa za kiuchumi na kijamii.”alisema

Reuben amesema,  wanahabari ambao hawajajiunga wakati ni sasa ili kuungana pamoja katika kuinuana kitaaluma, kuungana na wanawake kutetea haki za wanawake na watoto na kuongeza wingo wa wanawake kuungana na kuwa na sauti moja.

 Amesesitiza faida za kuwa mwanachama wa TAMWA ni kupata mkopo wa kujiendeleza kitaaluma katika stashahada ya kwanza au ya pili na baadae kurudisha mkopo huo bila riba.

“Pia kuna mafunzo ya kubadilishana taaluma (exchange program) zinazopatikana nchini na hata nje ya nchi, kumuongezea uwezo wa kitaaluma kwa mafunzo yanayotolewa na TAMWA kwa wanahabari, pamoja na kuandika taarifa mbalimbali za kijamii ambazo zitaweza kumuongeza zaidi katika taaluma yake,” alisema

 Ili kupitishwa  kuwa mwanachama unatakiwa kuwa na Diploma ya Habari, uzoefu katika fani ya uanahabari usiopungua miaka mitatu na kisha kupata wadhamini watatu ambao ni wanachama wa TAMWA.

Mwanachama mpya wa TAMWA, Bupe Mwakyusa, Mwandishi wa Mlimani TV ameelezea matarajio yake baada ya kuchaguliwa kuwa mwanachama  kuwa ni pamoja na kupata uzoefu zaidi katika taaluma ya habari na kushiriki katika miradi mbalimbali ya masuala ya kijinsia.

“Kilichonishawishi zaidi kujiunga TAMWA nikiwa mwanahabari ni kujifunza zaidi kuhusu taaluma ya habari pamoja na kupata maarifa zaidi kutoka kwa waliofanikiwa katika taaluma ya habari kupitia TAMWA, pia naamini kupitia TAMWA ntafika mbali zaidi”, alisema

TAMWA ilianzishwa mwaka 1987 na wanahabari wanawake nchini na mpaka sasa kina wanachama zaidi ya 100.  

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

MUUNGANO WA ASASI ZA KIRAIA ZINAZOSHAWISHI MABORESHO YA SHERIA YA USALAMA BARABARANI

 

TAREHE: 23 MEI 2020

 

UKUMBI: PIUS MSEKWA DODOMA

 

KONGAMANO LA USALAMA BARABARANI

 

Ndugu Waheshimiwa Wabunge;

Ndugu wawakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani Ya Nchi;

Ndugu wawakilishi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto;

Ndugu Wakurugenzi Asasi za Kiraia zinazoshawishi Maboresho ya Sheria ya Usalama Barabarani;

Ndugu Waandishi wa habari na wadau wote wa Usalama Barabarani, Mabibi na Mabwana;

Ndugu Waandaaji wa hafla hii Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) na Mwananchi Communication; - Habari za asubuhi.

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

HOTUBA YA MKURUGENZI WA TAMWA KATIKA KONGAMANO LA USALAMA BARABARANI LILILOANDALIWA NA TAMWA

HOTUBA

 

YA

 

BI ROSE REUBEN - MKURUGENZI MTENDAJI (TAMWA)

  

KWENYE

 

KONGAMANO LA USALAMA BARABARANI

 

 

MADA: USALAMA BARABARANI KWA AFYA NA MAENDELEO YA UCHUMI

 

 

UKUMBI: UKUMBI WA BUNGE PIUS MSEKWA- DODOMA

 

 

TAREHE: 23 MEI 2020

 

Kipengele cha 1: Mtandao wa asasi za kiraia/zisizokuwa za kiserikali zinazoshawishi maboresho ya sheria ya usalama barabarani.

 

"Mtandao wa Usalama Barabarani Tanzania ni nini?. Kitu gani mtandao umefanya kuhusiana na Usalama barabarani?. Dhumuni kuu ni nini?"

I.Utangulizi

 

Ndugu Mgeni Rasmi, Waheshimiwa Wabunge, wawakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani Ya Nchi, wawakilishi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto, Viongozi wa Serikali, Wawakilishi Asasi za Kiraia zinazoshawishi Maboresho ya Sheria ya Usalama Barabarani, Washirika wa Maendeleo, Wanahabari na Vyombo vya habari mliopo, Waathirika wa ajali za barabarani, Wageni waalikwa Mabibi na Mabwana,

Ni heshima kubwa kwangu kutoa hotuba hii, kwa niaba ya mtandao katika kongamano hili muhimu.

Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa uhai na kutuwezesha kukutana hapa siku ya leo. Napenda kuwapongeza TAMWA na Mwananchi communications kwa maandalizi bora ya mkutano huu.

Napenda pia kulishukuru Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukubali kuwa mwenyeji wa hafla hii.

Napenda pia kushukuru na kutambua juhudi kubwa za wajumbe wa Mtandao ambao wamefanya kazi kwa bidii kutayarisha hafla hii, haswa katika kufikia adhma ya

 

Naomba nianze kwa kutoa historia fupi ya mtandao huu wa asasi za kiraia unaoshawishi maboresho ya sheria ya usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kazi na mafanikio yake;

II.Shirikisho la Usalama BarabaraniTanzania

 

Mabibi na Mabwana,

Shirikisho la Usalama Barabarani Tanzania (CSO's) lilizinduliwa mnamo Mei 2016, na wanachama sita tu chini ya uratibu wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA), lakini umeongezeka hadi leo hadi wanachama wapatao kumi na tano ambao ni pmaoja na Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA), Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), Mabalozi wa Usalama Barabarani (RSA), Amend Tanzania, Shirikisho la Vyama vya Watu wenye ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (TABOA), Taasisi ya Taifa ya Usafirishaji (NIT), Tanzania Media Foundation (TMF), Safe Speed Foundation, Women Legal Aid Centre (WLAC), WILDAF, Mwanza Youth and Children Network (MYCN), Media Space Tanzania, pamoja na watu binafsi wenye utaalamu na mapenzi na usalama barabarani.

Wajumbe wa umoja huo wamekuwa wakifanya kazi na Serikali (haswa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Uchukuzi na idara / mashirika chini ya wizara hizi), Shirika la Afya Duniani (WHO), Wabunge na watendaji wengine kuunga mkono utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Mabadiliko ya Sheria, haswa juu ya mabadiliko ya sera kwa marekebisho kamili ya Sheria ya Sheria ya Usalama Barabarani (RTA). Sekretarieti ya Ushirikiano kwa sasa upo chini ya usimamizi wa TAWLA.

III.Kazi ya mtandao kuhusiana na usalamabarabarani

 

Mtandao huu ulianzishwa kwa malengo kadhaa ikiwa ni pamoja na kuwa na sauti ya pamoja katika kuendesha kampeni ya kushawishi maboresho ya sheria ya usalama barabarani pamoja na kuongeza uelewa kwa umma juu ya masuala mbalimbali ya usalama barabarani.
vilevile mtandao huu uliundwa kwa lengo la kuwa kama kiungo kati ya watumiaji wa barabara pamoja ba viongozi wa serikali/watunga sera ili kushawishi kuwepo kwa mfuno wa kisheria na kisera unaoendana na viwango vya kimataifa.

Mtandao umerekodi mafanikio kadhaa ikiwa ni pamoja na kuongeza uelewa kwa watumiaji wa barabara juu ya ukubwa wa tatizo hasa kwenye viashiria vitano vinavyochangia ongezeko ajali.

Mtandao umefanya kazi kwa karibu na kamati mbalimbali za bunge, hii ilipelekea wao kushawishika na kuamua kuanzisha mtanao wa kibunge unaojihusisha na masuala ya usalama barabarani ambao una takribani ya wabunge 120.

IV.Masuala ambayo Mtandao unayafanyiauchechemuzi;

 

Mtandao unafanya uchechemuzi juu ya mfumo bora wa kisheria juu ya usalama barabarani ili kuhakikisha kuwa ajali za barabarani zinapungua, ikiwa ni pamoja na majeraha yatokanayo na ajali za barabarani pamoja na vifo. Pia shirikisho linatetea na kupigania uwepo wa Sheria ya Usalama Barabarani (RTA) ya mwaka 1973. Kuna mapungufu ambayo yalitambuliwa katika Sheria ya Usalama Barabarani (RTA) na kwamba ikiwa yataboreshwa, ajali za barabarani zitapungua, idadi ya majerahi na vifo vitokanavyo na ajali za barabarani zitapungua.

Mapungufu yaliyotambuliwa yanahusiana na visababishi vitano hatarishi ambavyo ni; Mwendo kasi, Matumizi ya vilevi wakati wa kuendesha chombo cha moto, Kutotumia kofia ngumu (helmet) kwa abiria na dereva wa pikipiki, Kutokufunga mikanda wakati wa safari, na kutotumia vizuizi vya watoto.

  1. Kwenye upande wa Mwendokasi – Mtandao unashawishi uendeshaji wa vyombo vya moto kwa spidi ya kilomita 50 kwa saa katika maeneo ya mijini na makazi, na kilomita 30 kwa saa mahali ambapo kuna alama za watembea kwa miguu na wanyama, Utafiti umeonyesha kuwa hatari ya kufa ni chini ya asilimia 20 wakati gari liko chini ya kasi ya kilomita 50 kwa saa na asilimia 60 wakati gari liko kwenye kasi ya kilomita 80 kwa saa. Inakadiriwa kuwa kupunguzwa kwa asilimia 5 kwa mwendokasi, kunapunguza asilimia 30 ya ajali mbaya ambazo zinazowezakutokea.
  1. Kwenye upande wa kuendesha chombo cha moto ukiwa umelewa – Mtandao unashawishi kupunguzwa kwa kiwango cha kilevi kutoka kwa miligramu 80 kwa kila mililita 100 za damu (0.08g / dl) hadi miligramu 50 kwa kila mililita 100 za damu (0.05g / dl) kwa angalau dereva mwenye uzoefu, na kutofautisha kati ya dereva mwenye uzoefu na asiye na uzoefu ambaye kiwango cha pombe cha damu kinapaswa kisizidi miligramu 20 kwa kila mililita 100 za damu (0.02g / dl.) Lazima kuwe na utekelezaji mzuri wa sheria inayohusiana na kunywa hadi kupitiliza mipaka iliyowekwa. Inakadiriwa kuwa asilimia 5 ya vifo vyote vya barabarani vilivyoripotiwa ulimwenguni kote vinahusiana na ulevi (Ripoti ya hali halisi ya Shirika la Afya Ulimwenguni ya 2018). Sheria yetu inaruhusu hadi kiwango cha pombe cha miligramu 80 kwa kila mililita 100 za damu (08g / dl.) Kuwa ndiyo Kiwango cha juu cha pombe kinachohitajika. Hatari ya ajali huongezeka mara tatu kwa madereva ambao hutumiavilevi.
  1. Kwenye matumizi ya kofia ngumu (helmet) – Mtandao unashawishi utumiaji wa lazima wa kofia ngumu kwa wote yaani, dereva na abiria kwa kwa sasa shiria inamtaja dereva pekee. Inakadiriwa kuwa asilimia 22 ya vifo vya ajali za barabarani uimwenguni kote vinatokana na pikipiki na bajaji. Imeelezwa kuwa majeraha mabaya yanajumuisha wapanda pikipiki ni yaleyaliyohusisha kichwa na shingo. Matumizi sahihi ya kofia ngumu yanaweza kusaidia kuzuia majeraha haya kwa asilimia 42 na kupunguzwa kwa asilimia 69 ya jeraha la kichwa (Ripoti ya hali halisi ya Shirika la Afya Ulimwenguni ya 2018).
  1. Kwa upande wa matumizi ya mikanda – Mtandao unashawishi uwepo wa vifungu vinavyohitaji abiria wote wa gari kufunga mikanda ya kiti katika gari bila kujali wamekaa kiti cha mbele au nyuma. Takwimu zinaonyesha kuwa kufunga mkanda kunapunguza hatari ya ajali kwa abiria wa kiti cha mbele kwa asilimia 45-50 katika tukio la ajali. Vivyo hivyo, hatari ya majeraha madogo na makubwa hupunguzwa kwa asilimia 25 na 45 kwa abiria wa viti vya nyuma. Kiwango cha kimataifa kinachokubalika kinahitaji matumizi ya mikanda ya kiti kwa viti vya mbele na nyuma. Sheria yetu inahitajikiti cha abiria wa mbele tu kufungaMkanda.
  1. Kwa upande wa kuwakinga watoto - Mtandao unapigania uwepo wa sheria ambayo itaweka matumizi ya lazima ya vifaa vya kukinga watoto (Vizuizi vya watoto). Ushahidi unaonyesha kwamba wakati watoto wameketi katika viti vyao vyenye vizuizi, kulingana na uzito na saizi ya mwili wao, hatari ya majeraha na kifo hupunguzwa kwa karibu asilimia 70. Viwango vya kimataifa vinahitaji kuwa watoto wa umri wa miaka chini ya 7 wanapaswa kutumia vizuiziili kuzuia majeraha na vifo ikiwa ajali itatokea. Hakuna toleo juu ya vizuizi vya watoto katika Sheria ya Usalama Barabarani sura ya 168.

Kwa mara nyingine ninawashukuru na kuwapongeza wote ambao wamefanikisha tukio hili. Ni matumaini yangu kuwa maazimio yote tutakayoafikiana hapa katika kongamano hili, yatafanyiwa kazi na kuja na njia ambazo ni bora na sahihi zaidi katika kupunguza ajali za barabarani .

 

USALAMA BARABARANI NI JUKUMU LETU SOTE.!

“Ahsanteni sana kwa kunisikiliza”

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Aprili 11, 2020. Wakati huu ambapo dunia nzima inapambana na ugonjwa wa Covid -19 unaosababishwa na virusi vya Corona, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinawakumbusha wanahabari na wamiliki wa vyombo vya habari kufuata miongozo ya kutekeleza majukumu yao kwa kujilinda na maambukizi ya ugonjwa huu, na kutumia zaidi teknolojia ya mawasiliano.  Ugonjwa wa Covid-19 unaweza kumuathiri mtu yeyote, hivyo wanahabari, wamiliki wa vyombo vya habari na wadau wote wa habari wanapaswa kukubaliana na mabadiliko ya kiutendaji kazi yatakayowaepusha dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huu. TAMWA inawashauri wanahabari na wamiliki wa vyombo vya habari kujikita katika kutumia maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano kupata habari badala ya kwenda katika mikusanyiko isiyo ya lazima kwani taarifa zinaweza kutumwa kimtandao au mahojiano kwa njia ya simu. “Bila shaka hofu ya ugonjwa wa Covid 19 itabadili mfumo wa utendaji kazi wa tasnia ya habari kama taasisi inayohudumia jamii na kuanza kujiona kuwa na wao pia ni sehemu ya jamii,” TAMWA tunathamini usalama wa wanahabari kwa kuwa sisi ni sehemu na mdau wa vyombo vya habari ambavyo vimekuwa chanzo cha ufikishaji wa taarifa za kutetea haki za wanawake na watoto zenye lengo la kuwa na Tanzania inayoheshimu misingi ya usawa wa jinsia.  Wanahabari wanaoripoti kuhusu COVID-19 na wanahabari wengine, wanashauriwa kufanya maandalizi kabla ya kwenda katika mikutano, kwa kufuata mbinu za kujikinga na maambukizi. 

Star InactiveStar InactiveStar InactiveStar InactiveStar Inactive

Aprili 7, 2020. Wakati dunia nzima ikigubikwa na mshtuko kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya Corona, Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinapenda kuihadharisha jamii juu ya ongezeko la ukatili wa wanawake na watoto unaoweza kukithiri wakati wa janga la ugonjwa huu.

“Watoto wapo nyumbani wakati huu ambapo serikali imezifunga shule, lakini iwapo wazazi na walezi hawatakuwa makini basi huenda wakaathirika na ubakaji na mimba za utotoni katika kipindi hiki ambacho macho na masikio yapo katika kudhibiti virusi vya Corona,”

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto(UNICEF) linasema, ukatili wa watoto aghalabu hufanyika nyumbani, mtoto akielekea au akitoka shule wakati anapokuwa peke yake bila msaada.

TAMWA inaipongeza serikali kwa kuchukua hatua za haraka za kufunga shule ili kupunguza msongamano unaoweza kusababisha maambukizi, hata hivyo ni muhimu kuihadharisha jamii kuhusu ukatili wa kijinsia na ule wa watoto unaoweza kuongezeka wakati huu.

Endapo wazazi/walezi hawatawasimamia vizuri watoto katika kipindi hiki cha siku 30 zilizotolewa na serikali kupitia Waziri Mkuu, basi tunaweza kutengeneza kizazi kingine kilichoathirika na ukatili wa aina mbalimbali ikiwamo ubakaji, ulawiti na mimba zisizotarajiwa.

Kwa mfano, Ripoti ya UNICEF 2016 inaonyesha kuwa, wakati wa mlipuko wa Ebola Afrika Magharibi 2014 hadi 2016, ulisababisha ongezeko la ajira kwa watoto, ukatili kwa wanawake na watoto na mimba za utotoni. Kwa mfano, mimba za utotoni nchini Sierra Leone ziliongezeka kufikia 14,000 kutoka 7,000.

“Ni muhimu kwa wazazi na walezi kuwalinda watoto na virusi vya Corona lakini wakati huo huo tuangalie madhara wanayoweza kuyapata watoto wa kike na wa kiume wanapokuwa nyumbani au mitaani”

Tunapaswa kujiuliza iwapo watoto wetu wapo salama wawapo nyumbani au mitaani wanapotembea wakati huu wa likizo ndefu. Je, Mafataki hawawanyemelei? Je ndugu na jamaa wanaobaki na watoto hawa wanawalinda au wanawaharibu? Je watoto hawa hawatakuwa katika hatari ya kuozwa mapema?

Si hivyo tu, janga hili la Corona linaathiri zaidi wanawake kwani shule zinapofungwa, mzigo mkubwa wa malezi unawaangukia kinamama nyumbani ambao ndiyo walezi wakuu wa familia.

Takwimu za Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) zinaonyesha kuwa, dunia nzima, asilimia 70 ya watoa huduma za jamii na za afya ni wanawake. Majukumu haya huwaweka mstari wa mbele katika utoaji wa huduma, Je katika janga hili la Covid-19, wanawake wanalindwa ipasavyo wasidhurike?

TAMWA inaiomba serikali, wadau na watunga sera kwanza, kutosahau hatari nyingine zinazoweza kuwapata wanawake na watoto katika kipindi cha janga la Covid-19.

Pili, wadau wa afya, elimu na watoto kutoa mafunzo kuhusu namna ya kujilinda na ya kuripoti kuhusu ukatili kwa watoto wakati huu wa mlipuko.

Tatu, kuongeza upatikanaji wa taarifa na misaada mingine kwa watoto.

Nne, kubuni mfumo wa kuwapa watoto elimu wawapo nyumbani.

Tano, wahudumu wa afya wanawake wawekewe mazingira salama ya kutoa huduma ili wasiathirike.

Sita, wazazi na walezi kuimarisha ulinzi na kuzuia matembezi yasiyo ya lazima kwa watoto.

Rose Reuben

Mkurugenzi Mtendaji,

TAMWA.

Latest News and Stories

Search