News/Stories

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Sauda Msangi, TAMWA.

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA)kimefanya midahalo miwili iliyolenga kuwajengea uwezo wanawake na vijana namna ya kuzuia ukatili wa kijinsia, rushwa ya ngono na kuwepo kwa usawa wa kijinsia ndani ya vyombo vya habari.

Midahalo hiyo iliwalenga wanahabari na wabunge wanawake ili kuongeza idadi ya viongozi wanawake pamoja na kutengeneza mazingira salama yatakayowawezesha kufikia malego yao ya kiuongozi. Midahalo hiyo iliwashirikisha wabunge wanawake na wanahabari kutoka katika mikoa mitatu nchini.

TAMWA inatekeleza mradi wa miaka miwili wa kuwajengea uwezo wanawake na vijana katika vyumba vya habari unaofadhiliwa na International Media Support IMS.

Akizungumza wakati akifungua mdahalo wa wabunge, Naibu Spika wa Bunge Dk Tulia Ackson aliipongeza TAMWA na kusem imekuja mapema, wakati ndiyo mwanzo wa miaka mitano kukiwa na mambo mengi ya kuyaweka vizuri.

“Tuna mambo mengi ya kuyaweka vizuri na wanawake wenzetu, idadi hii ya wabunge inatakiwa kuongezeka walioko katika viti maalumu waende kugombea majimboni na wengine kuingi viti maalumu, amesema Dk Tulia amesema wanawake wabunge waliochaguliwa na kuteuliwa jukumu lao sio tu kuwakilisha vyama bungeni bali pia katika kuwatumikia wananchi ili kuongeza idadi ya wanawake viongozi zaidi nchini kufikia 50/50. “

Wakati ni sasa wa kujiwekea mipango madhubuti ya kuendelea kuwa viongozi, amesema Akizungumzia hofu ya wanawake kujitokeza kuzungumza mbele ya vyombo vya habari Dk Tulia amesema ni kutokanana hofu ya jinsi watakavoandikwa na kuzungumziwa.

Kwa upande wake, Mkurungezi wa TAMWA, Rose Reuben amesema wanawake waliopata nafasi za uongozi wapange mikakati ya kuangalia kuendelea kuwepo na wengine waongezeke kwa kuonyesha wigo mpana wa uongozi, kuonyesha ujasiri na kujitokeza kuzungumzia masuala ya wanawake katika vyombo vya habari.

Reuben amesema wabunge wanawake hawajitokezi kwa wingi katika vyombo vya habari hivyo ni vyema kijitokeza na kuzungumza ikiwa ni njia mathubuti za kujiinua zaidi kisiasa na kiuongoz. Wabunge wanawake waache kuhofia vyombo vya habari kwa kuwa mkiwa bungezi mna nafasi kubwa kuzungumzia na kutilia mkazo masuala ya ukatiki wa kijinsia hivyo kupunguza unyanyasaji dhidi ya wanawake,alisema Reuben amesema TAMWA iko tayari kushirikiana na wabunge wanawake katika kuwaelimisha namna ya kuvitumia vyombo vya habari pamoja na kutumia mitandao ya kijamii.

Kadhalika ameiomba Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo iwe na Dawati la Jinsia litakalowasaidia wanahabari wanawake kupata kwa urahisi, eneo la kusemea pindi wanapokabiliwa na ukatili wa kijinsia, pia litakalowezesha masula ya kijinsia kuzungumziwa katika mikutano ya wafanyakazi.

Katika mdahalo wa waandishi wa habari, wanahabari walionyesha kutokuwepo kwa usawa wa kijinsia na kuwepo wa vitendo vya rushwa ya ngono katika vyumba vya habari Wanahabari wamesema zipo sera za jinsia ndani ya vyombo vya habari hazifuatwi wala kuzungumziwa ndani ya vyumba vya habari.

Pia katika mdahalo huo wanahabari wametoa mapendekezo ya kuwepo kwa madawati ya kijinsia kwenye vyumba vya habari ili kutoa taarifa kwa uhuru iwapo vitendo vya ukatili wa kijinsia vitatokea.

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Godwin Assenga, TAMWA.

Septemba 22, 2020. Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), Rose Reuben amewataka wanafunzi kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na kuzingatia maadili.

Reuben, ameyasema hayo hivi karibuni wakati akiwakabidhi vyeti wahitimu wa darasa la saba na kidato cha nne wa Shule ya Filbert Bayi, jijini Dar es Salaam wakati wa mahafali ya 16 ya shule hiyo.

Akiwa mgeni rasmi katika mahafali hayo, Reuben aliwaasa wanafunzi hao kuwa makini na matumizi ya teknolojia ikiwamo mitandao ya kijamii kwa kuzingatia maadili waliyofunzwa na walimu, wazazi ili wafikie ndoto zao.

"Mimi ni Mwanahabari, natambua kwamba sasa hivi teknolojia imekua kiasi kwamba kuna mitandao. Mitandaoni kuna mambo mazuri sana, lakini pia yapo mabaya. Mitandaoni kunaweza kukupoteza, mitandaoni kunaweza kukujenga,” amesema.

Amewaasa wanafunzi hao kuwa, pindi watakapoitumia mitandao hiyo wakumbuke kuzingatia maadili waliyofunzwa na wazazi pamoja na walimu wao.

"Sina namna ya kuwazuia kutumia mitandao ya kijamii kwa sababu ndiyo dunia ya sasa, lakini itumieni mkijua kwamba mnaingia mitandaoni masikio yenu na macho yenu yakiwa wazi kwamba wewe ni mtu unaetegemewa na Taifa letu, unaetegemewa na wazazi wako" amesisitiza Reuben.

Kadhalika, amewasisitiza  wanafunzi kutumia vyema vipaji maalum walivyo navyo huku akiwakumbusha kwamba kila wanachokifanya, wakifanye katika ubora huku wakitumia vyema muda wao vizuri ili kuhakikisha wanafikia malengo na ndoto zao.

Amewapongeza wazazi kwa  kujitoa vyema kimalezi na kielimu licha ya kuwepo kwa janga la Corona, lililoathiri uchumi.

Wakati huo huo, uongozi wa shule ya Filbert Bayi, ulitoa punguzo la ada la Sh500, 000 kwa wanafunzi waliohitimu darasa la saba walioamua kuendelea na kidato cha kwanza katika shule hiyo.

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Chama Cha Waandishi Habari Wanawake (TAMWA) kimepewa mafunzo ya siku nne kwa ajili ya kujengewa uwezo kuhusu   masuala ya usalama wa kimtandao  ili kuwezesha kufanya kazi kwa ufanisi na kwa usalama.

 
Mafunzo hayo yametolewa na taasisi ya Jamii Forum Jijini Dar-es-Salaam ambayo kwa sasa inasimamia masuala ya demokrasia, utawala bora na usalama wa kimtandao. 
 
 Mkurugenzi wa Jamii Forum Maxence Mello amesema mafunzo hayo ni muhimu kwa TAMWA kwani taasisi hiyo inahitaji kuwa na ujuzi wa masuala ya usalama wa kimtandao ili kuepusha kupoteza takwimu muhimu.
 
Mello amesisitiza umuhimu wa mafunzo ya usalama wa kimtandao kwa kuwa dunia ya sasa imekuwa kwa kasi kiteknolojia hivyo kila wakati inapaswa kupewa mafunzo ili kuwa katika usalama zaidi.
 
“TAMWA na Jamii Forum tuna uhusiano wa muda mrefu na hivyo daraja hili liwe imara na tuendelee kuwasiliana na ikiwezekana muwe mabalozi wetu’’ alisema Mello
 
Kwa upande wake, Mkufunzi wa Mafunzo hayo, John Kaoneka   ameiomba TAMWA kuboresha vifaa vyake ili viwe katika mfumo wa kisasa zaidi kwa ajili ya kuboresha mawasiliano na usalama wa takwimu na taarifa muhimu.

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active
 
BACK GROUND:
 
Tanzania Media Womens Association (TAMWA) is a non-profit, non-partisan, non-governmental and human rights organization founded and registered on 17th  November, 1987 under the Societies Ordinance Cap 337 of 1954 with registration number (SO 6763) and the Association complied with the 2002, NGO Act of the United Republic of Tanzania in 2006. 
 
ABOUT THE CALL
TAMWA under African Women Development Fund (AWDF) is looking for an experienced RADIO AND TV producer who will be responsible to produce a radio spot and or Television Spot which will highlights Challenges, success and women political inclusion landscape in Tanzania 
 
The produced spots will be aired in Televisions and Community radio based in Arusha, Dodoma, Zanzibar and Dar es Salaam. 
The documentary will showcase challenges facing women politicians during the electoral process, successes achieved in women inclusion in all aspect of politics and the current political situation towards the coming election. 
 
Activity Duties 
Gathering content for radio and /TV spot
Looking for best scene for a spot
Editing the drafts
Producing a creative audio clip of a radio spot
Producing a creative visual spot for  TV
Submit first draft of a radio/TV draft spot 
Editing and designing
 
 
Activities Time Frame
Gathering Content for radio/Tv spot should be done from August 25
Editing drafts should be done  by early September
Sharing first draft of the audio/Tv spots should be done by 5th September
Final editing should be done by 10th  September
Submitting final draft by 15th September
 
The interested consultant/company should submit the budget offer, profoma invoice and attach a sample of the previous work and/or link electronically to This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. cc This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.;  by Monday 24th August 2020, before end of business.
 

User Rating: 5 / 5

Star ActiveStar ActiveStar ActiveStar ActiveStar Active

Mwandishi Wetu, TAMWA

Dar es Salaam. Wanahabari Wanawake 52 wamefanikiwa kujiunga na Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania -TAMWA mwaka huu hatua inayodhihirisha kuwa wigo wa kuripoti habari za ukatili wa kijinsia na usawa wa kijinsia, utaendelea kupanuka.

Wanachama  hao wapya  kutoka Tanzania Bara(26) na Visiwani(26)  wamejiunga kwa ajili ya kuongeza wigo katika harakati za kuondoa mifumo yote ya ukatili wa kijinsia na kuwawezesha kitaaluma wanahabari wanawake nchini.

Akizungumzia kujiunga kwa wanahabari wapya katika chama hicho Mkurugenzi wa TAMWA, Rose Reuben amesema kujiunga kwa wanahabari hao kunaongeza jitihada za kutetea haki za wanawake na watoto zenye mrengo wa kijinsia.

“Wakati huu tunapaswa kuwa na taarifa mbalimbali zenye mrengo wa kijinsia zitakazosaidia wananchi , watunga sera na  jamii kwa ujumla  kuelewa kwamba jamii yetu inahitaji sera na taarifa za kiuchumi na kijamii.”alisema

Reuben amesema,  wanahabari ambao hawajajiunga wakati ni sasa ili kuungana pamoja katika kuinuana kitaaluma, kuungana na wanawake kutetea haki za wanawake na watoto na kuongeza wingo wa wanawake kuungana na kuwa na sauti moja.

 Amesesitiza faida za kuwa mwanachama wa TAMWA ni kupata mkopo wa kujiendeleza kitaaluma katika stashahada ya kwanza au ya pili na baadae kurudisha mkopo huo bila riba.

“Pia kuna mafunzo ya kubadilishana taaluma (exchange program) zinazopatikana nchini na hata nje ya nchi, kumuongezea uwezo wa kitaaluma kwa mafunzo yanayotolewa na TAMWA kwa wanahabari, pamoja na kuandika taarifa mbalimbali za kijamii ambazo zitaweza kumuongeza zaidi katika taaluma yake,” alisema

 Ili kupitishwa  kuwa mwanachama unatakiwa kuwa na Diploma ya Habari, uzoefu katika fani ya uanahabari usiopungua miaka mitatu na kisha kupata wadhamini watatu ambao ni wanachama wa TAMWA.

Mwanachama mpya wa TAMWA, Bupe Mwakyusa, Mwandishi wa Mlimani TV ameelezea matarajio yake baada ya kuchaguliwa kuwa mwanachama  kuwa ni pamoja na kupata uzoefu zaidi katika taaluma ya habari na kushiriki katika miradi mbalimbali ya masuala ya kijinsia.

“Kilichonishawishi zaidi kujiunga TAMWA nikiwa mwanahabari ni kujifunza zaidi kuhusu taaluma ya habari pamoja na kupata maarifa zaidi kutoka kwa waliofanikiwa katika taaluma ya habari kupitia TAMWA, pia naamini kupitia TAMWA ntafika mbali zaidi”, alisema

TAMWA ilianzishwa mwaka 1987 na wanahabari wanawake nchini na mpaka sasa kina wanachama zaidi ya 100.  

Latest News and Stories

Search